Ni zaidi ya kinga ya UKIMWI - TAFAKARI

Katika survey moja, wanawake walisema wanalazimika kukataa ku... na waume zao kwa sababu waume wanakataa kutumia kinga ilhali wana nyumba ndogo.

Baadhi ya hao wanawake walienda mbali zaidi na kudai kuwa kwa vile nao ni binadamu wenye mahitaji kama walivyo wanaume, na kwa vile wanaume wanakataa kutumia kinga kwenye ndoa, basi nao hulazimika kutoka je ya ndoa.

Huko ni rahisi ku negotiate matumizi ya kondomu! Sasa kwanini wanandoa wasikubali kutumia kinga ili kuzuia cheating kwenye ndoa?
 
Katika survey moja, wanawake walisema wanalazimika kukataa ku... na waume zao kwa sababu waume wanakataa kutumia kinga ilhali wana nyumba ndogo.

Baadhi ya hao wanawake walienda mbali zaidi na kudai kuwa kwa vile nao ni binadamu wenye mahitaji kama walivyo wanaume, na kwa vile wanaume wanakataa kutumia kinga kwenye ndoa, basi nao hulazimika kutoka je ya ndoa.

Huko ni rahisi ku negotiate matumizi ya kondomu! Sasa kwanini wanandoa wasikubali kutumia kinga ili kuzuia cheating kwenye ndoa?

Mama wa sabusitensi hebu nifafanulie hapo kwenye red. Hivi kungonoka kwa kondomu siyo cheating a.k.a Infidelity? hebu niambie fasta nianze kushangilia na hili vuvuzela langu hapa lol!
 
Dawa ni kutubu na kufuata mapenzi ya Mungu.

...He he heee..... Mutu ya lojistiks... point lakini (sasa tunaanza kuelewana)

Hakyanani huu ugonjwa umeingia pahala pabaya, pachafu na patamu sana..... Hakuna njia ya kuukabili huu mdude zaidi ya kuepuka ngono zembe. Uaminifu kwa sasa lazima tukubali umeshashindikana. Unaweza kuwa mwaminifu wewe lakini mwenzio asiwe.

Infidelity, ambayo kwa sasa ni kama sheria lazima ifanyike kwa kinga... Vinginevyo kama nilivyosema. Tutubu na tumrudie Muumba wetu

Hivi maaskofu wanaupataje huu ugonjwa?

Kwenye Kontamineted Divai

Mama wa sabusitensi hebu nifafanulie hapo kwenye red. Hivi kungonoka kwa kondomu siyo cheating a.k.a Infidelity? hebu niambie fasta nianze kushangilia na hili vuvuzela langu hapa lol!

hapa kuna mtu ameiba aidii ya x-pin!....
OTHERWISE IT CAN'T BE HIM
 
Enyi Wanadamu, Mtafakarini Mungu na kuachana na Tamaa za Mwili. Hata ukifanya Ngono vipi huwezi kuridhika na utatamani zaidi tu! Hebu mwangalie suleimani aliyekuwa na wanawake 1000 lakini mwishoni alikiri ni kama kufukuza Upepo! Kuna aliyepata medali ya kuzini isipokuwa Mauti tu?
 
Mama wa sabusitensi hebu nifafanulie hapo kwenye red. Hivi kungonoka kwa kondomu siyo cheating a.k.a Infidelity? hebu niambie fasta nianze kushangilia na hili vuvuzela langu hapa lol!
Hebu stopisha vuvuzela kwanza kisha usikilize kwa maakini.
Ni hivi, watu wanakosa huduma nyumbani kwa kuogopa maambukizi ( watu hawatumii kondomu kwenye ndoa si ndio?) .. sasa anapotafuta huduma nje, huko nje hutumia hiyo kinga! Hoja yangu ni kuwa, ili mtu asitoke nje, je afadhali wanandoa wakubali kutumia kinga.
 
TAKWIMU HIZI ZIMENIFANYA NITAFAKARI.NDOA HUWEZA KULETA HATARI ZAIDI KULIKO KINGA DHIDI YA UKIMWI:
"According to the data from Tanzania HIV AIDS and Malaria Indicator Survey (THMIS) 2007-2008, the national prevalence among the sexually active populations (between 15 and 49 years of age) is reported to be 5.7 %. The data shows more women (6.6 %) are infected than men (4.6%). HIV prevalence is higher among women than men in both urban and rural areas and highest among married couples. Amongst ‘HIV-discordant couples', there are more male-positive-female-negative couples than vice versa. Among certain older age groups, men have higher HIV prevalence than women."

Hapo kwenye blue hapo!
1. Inaonekana walio kwenye ndoa ndio wenye kuambukizwa/kuambukizana zaidi kuliko baina ya wasio na ndoa.
2. Walio kwenye ndoa, kuna wanandoa ambao mmoja ameambukizwa wakati mwingine hana maambukizi.Na wengi wasio na maambukizi kati ya wana ndoa wanawake ndio wengi.
3. Katika makundi yenye umri mkubwa, wanaume wengi wameambukizwa kuliko wanawake.

Kuna dhana kwamba waliooana wanalindana dhidi ya UKIMWI kwa vile kutakua na uhakika wa mpenzi mmoja, asiye na maambukizi! Lakini kwa ukweli wa maisha ya siku hizi, inaonekana dhahiri kuwa ndoa yaweza kuwa chanzo kikubwa cha kuangamia kwa gonjwa la UKIMWI.

Je nini kifanyike? watu wasioane? waliooana watumie kinga? au inakuwaje? TUJADILI



Jirani, watu hawawezi kuacha kuoana au kuishi pamoja kama mke na mume kwa miaka mingi, pia swala la kutumia kinga ndani ya ndoa halipo kabisa...maana Wanaume wengi hawaelewi wala hawalikubali na hata baadhi ya Wanawake hawalikubali. Mama mmoja alikuwa analalamika kwamba anatoa mimba nyingi kwa kuwa walikuwa hawataki watoto zaidi baada ya kujaliwa watatu. Nikamwambia kwanini hutumii kinga? akasema kinga nyingi za kuzuia mimba zina athari mbaya sana kwake hivyo ameamua kuachana nazo. Nikamwambia basi tumieni condom akaniambia EBO! Mume wangu aende nje atumie condom aje nyumbani nimwambie atumie condom hili haliwezekani kabisa...akatumie condom nje. Nikabaki nimepigwa na mshangao wa hali ya juu na wala sikuwa tena na la kuongeza. Sasa katika ndoa zetu za Kitanzania mke amwambie mume kwamba Baba fulani naomba utumie condom...si mama atakuwa anatafuta balaa ndani ya nyumba. Pagumu hapa jirani.
 
kumbe asilimia ya wenye ngoma ni ndogo hivyo?
Ndugu Funzadume,sio idadi ya wenye ngoma bali prevalence
"According to the data from Tanzania HIV AIDS and Malaria Indicator Survey (THMIS) 2007-2008, the national prevalence among the sexually active populations (between 15 and 49 years of age) is reported to be 5.7 %. The data shows more women (6.6 %) are infected than men (4.6%)
Definition ya prevalence
Medicine: The total number of cases of a disease in a given population at a specific time.

prevalence - (epidemiology) the ratio (for a given time period) of the number of occurrences of a disease or event to the number of units at risk in the population
Na ndio maana huyo mwandishi hapo kataja muda maalum(mwaka mmoja),kwa hiyo hizo ni cases za ukimwi kwa mwaka wa 2007-2008.(however,I remain to be corrected)

Sababu zinazopelekea cheating katika ndoa ziko nyingi,miongoni mwazo ni watu(hususwan wa nchi maskini) wanaoana bila ya kupendana kwa dhati,wanaume huenda ni hulka ya maumbile fulani kwa mwanamke ambayo as she becomes older yanapoteza mvuto ule wa awali hivyo kupelekea jamaa kutafuta mbadala nje,na ndio maana huwa wanakimbilia visichana.
Wanawake nao:Huenda ni kwa vile anayempenda kwa dhati hajamuoa,kwa hiyo just anaamua kuolewa na yoyoyte aliyekuja hata kama hampendi kiviile.Sometimes anaoelewa ili ku sustain life kutokana na ugumu wa life etc.

Pia kukosa mapenzi ya wazazi wetu katika hatua fulani ya ukuaji wetu:Kuna cohort study ilifanywa USA ikaonekana kuwa teenagers ambao walipata sincere and true love from their mothers,walikuwa so romantic na honest to their partners.Kwa hiyo kukosekana kwa mapenzi ya wazazi katika ukuaji wetu kunaweza kuleta athari in our marriages.

All in all,tushikamane na makatazo ya Mola Muumba na tufangamane na mafundisho Yake.Ukitaka kuoa au kuolewa omba Mungu akupatie Wa Ukweli,MchaMungu,muadilifu,Hottie(according to u..maana hii ni relative term) make sure mnapendana ki ukweli kutoka moyoni na siyo just material love,...then wewe kuwa determined kumuogopa Mungu kwa ukweli wa kumuogopa.Trust me,wewe ukiwa muadilifu wa kutosha huwezi kuishi na mzinifu hata kidogo,but ukiwa mzinifu aidha huyo mwenza hatakubali kuishi nawe ama naye atakuwa mzinifu(talking of majority)
 
Jirani, watu hawawezi kuacha kuoana au kuishi pamoja kama mke na mume kwa miaka mingi, pia swala la kutumia kinga ndani ya ndoa halipo kabisa...maana Wanaume wengi hawaelewi wala hawalikubali na hata baadhi ya Wanawake hawalikubali. Mama mmoja alikuwa analalamika kwamba anatoa mimba nyingi kwa kuwa walikuwa hawataki watoto zaidi baada ya kujaliwa watatu. Nikamwambia kwanini hutumii kinga? akasema kinga nyingi za kuzuia mimba zina athari mbaya sana kwake hivyo ameamua kuachana nazo. Nikamwambia basi tumieni condom akaniambia EBO! Mume wangu aende nje atumie condom aje nyumbani nimwambie atumie condom hili haliwezekani kabisa...akatumie condom nje. Nikabaki nimepigwa na mshangao wa hali ya juu na wala sikuwa tena na la kuongeza. Sasa katika ndoa zetu za Kitanzania mke amwambie mume kwamba Baba fulani naomba utumie condom...si mama atakuwa anatafuta balaa ndani ya nyumba. Pagumu hapa jirani.
MAKUBWA MADOGO YANA NAFUU!
Huyu mdada/mama ameniacha mdomo wazi! Ina maana anamjali sana huyo mumewe kiasi kuwa hajali kabisa usalama wake?Huko nje ana uhakika gani mumewe anatumia condom?
 
Mama mmoja alikuwa analalamika kwamba anatoa mimba nyingi kwa kuwa walikuwa hawataki watoto zaidi baada ya kujaliwa watatu. Nikamwambia kwanini hutumii kinga? akasema kinga nyingi za kuzuia mimba zina athari mbaya sana kwake hivyo ameamua kuachana nazo. Nikamwambia basi tumieni condom akaniambia EBO! Mume wangu aende nje atumie condom aje nyumbani nimwambie atumie condom hili haliwezekani kabisa...akatumie condom nje. Nikabaki nimepigwa na mshangao wa hali ya juu na wala sikuwa tena na la kuongeza. Sasa katika ndoa zetu za Kitanzania mke amwambie mume kwamba Baba fulani naomba utumie condom...si mama atakuwa anatafuta balaa ndani ya nyumba. Pagumu hapa jirani.

Dah...Mkuu BAK unataka kuniambia huyo mama anajua kwamba mumewe ana cheat na anakubaliana na hali hiyo!!!!!!!!....Kaazi Kweli Kweli.
Sitamani kujua kwamba majority ya ndoa zetu Tz ziko hivyo.Au hiyo ni majuu mkuu?
 
zingatia haya:-

.kuishi bila ngono haiwezekani (NB:hata ikiwa ndani ya ndoa bado inaitwa ngono)
.una uhakika wa wewe kuwa mwaminifu lakini huna uhakika wa mwenza wako kuwa mwaminifu.
.this is to say as long as una mwenza ambae hujui moyoni mwake anaficha nini UKIMWI is out of of your control (just play your part and keep your hopes up).

TO ME: siwezi kutumia kondom kwa waifu wangu kwa ajili ya kujikinga na ukimwi.
 
Dah...Mkuu BAK unataka kuniambia huyo mama anajua kwamba mumewe ana cheat na anakubaliana na hali hiyo!!!!!!!!....Kaazi Kweli Kweli.
Sitamani kujua kwamba majority ya ndoa zetu Tz ziko hivyo.Au hiyo ni majuu mkuu?

Naam kwa jibu hilo ina maana mama anajua Mzee ana nyumba ndogo, vinginevyo asingetoa kauli hiyo ya "mume wangu aende nje atumie condom." Hujasikia akina mama huwafungia waume zao condoms wanapokuwa wanasafiri kikazi ndani ya Tanzania au hata nje? na hili linafanywa na akina mama ambao wapo ndani ya ndoa ndani ya Tanzania yetu. Nilipohadithiwa hili nilibaki mdomo wazi.

Mkuu unadhani katika Tanzania yetu kwanini nyumba ndogo zinashamiri ndani ya ndoa nyingi nchini kama wahusika katika ndoa hawazifagilii? Hata yule Kilaini alitamka hivi karibuni kwamba anadhani katika 95% ya ndoa zetu wahusika wanatembea nje. Kama sikosei alikuwa anajibu swali kuhusiana na condom lakini pamoja na kuwa na hisia hiyo bado hakuona umuhimu wa kuwaomba waumini watumie kinga kwa sababu dini zetu zote mbili ni haramu kutumia condoms.

Na data zilizowekwa hapo juu hazidanganyi maana zinaonyesha maambukizi ni makubwa mno katika wana ndoa ukilinganisha na wale ambao hawamo katika ndoa.
 
MAKUBWA MADOGO YANA NAFUU!
Huyu mdada/mama ameniacha mdomo wazi! Ina maana anamjali sana huyo mumewe kiasi kuwa hajali kabisa usalama wake?Huko nje ana uhakika gani mumewe anatumia condom?

Ndiyo hapo jirani, sijui ana uhakika gani huko nje jamaa anatumia kinga.
 
Hii inakuwa hivi kwa kuwa wanandoa wengi hawatumii kinga wakiamini kuwa wote ni waaminifu kumbe kuna mmoja wao ama waote ambaye sio mwaminifu.Chakushangaza wakitoka pia nje ya ndoa hawatumii kinga pia.
 
TAKWIMU HIZI ZIMENIFANYA NITAFAKARI.NDOA HUWEZA KULETA HATARI ZAIDI KULIKO KINGA DHIDI YA UKIMWI:
"According to the data from Tanzania HIV AIDS and Malaria Indicator Survey (THMIS) 2007-2008, the national prevalence among the sexually active populations (between 15 and 49 years of age) is reported to be 5.7 %. The data shows more women (6.6 %) are infected than men (4.6%). HIV prevalence is higher among women than men in both urban and rural areas and highest among married couples. Amongst ‘HIV-discordant couples’, there are more male-positive-female-negative couples than vice versa. Among certain older age groups, men have higher HIV prevalence than women."

Hapo kwenye blue hapo!
1. Inaonekana walio kwenye ndoa ndio wenye kuambukizwa/kuambukizana zaidi kuliko baina ya wasio na ndoa.
2. Walio kwenye ndoa, kuna wanandoa ambao mmoja ameambukizwa wakati mwingine hana maambukizi.Na wengi wasio na maambukizi kati ya wana ndoa wanawake ndio wengi.
3. Katika makundi yenye umri mkubwa, wanaume wengi wameambukizwa kuliko wanawake.

Kuna dhana kwamba waliooana wanalindana dhidi ya UKIMWI kwa vile kutakua na uhakika wa mpenzi mmoja, asiye na maambukizi! Lakini kwa ukweli wa maisha ya siku hizi, inaonekana dhahiri kuwa ndoa yaweza kuwa chanzo kikubwa cha kuangamia kwa gonjwa la UKIMWI.

Je nini kifanyike? watu wasioane? waliooana watumie kinga? au inakuwaje? TUJADILI



WOS, the statistics a stunning especially pale ambapo wanasema married men are more [positive]... yaani hapa ndiyo cilinical knowledge yangu inashangaa maana ukiangalia clinically mwanamke yuko more at rist kupata infection kutokana na anatomy yake. mwanaume anaweza ku-engage a positive woman na asipate kama hakuna mchubuko

the only possible reason for the discordance nadhani itakua kwamba hawa wanandoa wameshaacha kufanya mapenzi muda mrefu sana

i guess its more of a sociological issue aisee
 
naam kwa jibu hilo ina maana mama anajua mzee ana nyumba ndogo, vinginevyo asingetoa kauli hiyo ya "mume wangu aende nje atumie condom." hujasikia akina mama huwafungia waume zao condoms wanapokuwa wanasafiri kikazi ndani ya tanzania au hata nje? Na hili linafanywa na akina mama ambao wapo ndani ya ndoa ndani ya tanzania yetu. Nilipohadithiwa hili nilibaki mdomo wazi.

mkuu unadhani katika tanzania yetu kwanini nyumba ndogo zinashamiri ndani ya ndoa nyingi nchini kama wahusika katika ndoa hawazifagilii? Hata yule kilaini alitamka hivi karibuni kwamba anadhani katika 95% ya ndoa zetu wahusika wanatembea nje. Kama sikosei alikuwa anajibu swali kuhusiana na condom lakini pamoja na kuwa na hisia hiyo bado hakuona umuhimu wa kuwaomba waumini watumie kinga kwa sababu dini zetu zote mbili ni haramu kutumia condoms.

na data zilizowekwa hapo juu hazidanganyi maana zinaonyesha maambukizi ni makubwa mno katika wana ndoa ukilinganisha na wale ambao hawamo katika ndoa.

astonishing~~~
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom