Ni wapi wanakopokea rushwa?

Wamnetu

Member
Apr 29, 2012
11
4
Nimebahatika kuingia katika ofisi mbalimbali za serikali na hata baadhi ya mahakama zetu jijini Dar es salaam na nilishangaa kuona matangazo mbalimbali katika kuta za ndani za baadhi ya ofisi hizo yakisema kwa maandishi makubwa "HATUPOKEI RUSHWA".

Jambo la kushangaza ni kuwa hata wakuu wa ofisi hizo wameafiki kuwepo kwa matangazo hayo. Jambo lingine la kushangaza ni kuwa baadhi ya ofisi hizo ndizo zimekuwa zinalalamikiwa sana na wananchi kuhusu ulaji/upokeaji rushwa.

Swali langu ni kuwa je kuna yeyote anayefahamu ofisi ambayo inatangaza kuwa wanapokea rushwa? Ningependa kuitembelea kama ipo!
 
mkuu we unadhani rushwa inatolewa vipi,bandiko ukutani ni kuzugia tu,but unapoanza kuongea nao kama una tatizo utajua tu wanavyoomba rushwa
 
waulize waendesha mashtaka na makarani wa mahakama watakueleza ziliko ofisi za kupokelea rushwa.
 
Pale kwenye hicho kibandiko ndipo unapotakiwa kusalimisha rushwa yako,baada ya kumalizana na wakuu walio ndani,ama unaandika namba ya simu unaichomeka pale,maisha yanaendelea, we ofisini kwenu hakuna sanduku la maoni?

mimi nilitakiwa kuchomeka rushwa ya 250,000/= kwenye sanduku hilo,ikiwa ndani ya bahasha,nikajua kumbe sanduku hili lina umuhimu mkubwa kiasi hiki, hii ndio Bongo.
 
It is the other way round. Kule wanakoandika hatupokei ina maana wanapokea zaidi. Pale pasipoandikwa wanapokea kdg kutokana na umuhimu wa huduma yao. TAKUKURU yenyewe iko kama daktari anayemtibu mgonjwa wa kansa na kumshauri aache sigara wakati yeye ana sigara mdomoni. RUSHWA NI UGONJWA WA HATARI MUNGU APISHE MBALI
 
Tanzania kama hatujaweka sheria ya kuwatandika watu risasi hadharani kwa kutoa au kupokea rushwa basi haitaisha.

Wapokea na watoa rushwa wa kwanza ni watunga sheria, nao ni wabunge wa bunge la JMT. Kwanini hawatungi sheria kali za kupambana na rushwa?
 
Tanzania kama hatujaweka sheria ya kuwatandika watu risasi hadharani kwa kutoa au kupokea rushwa basi haitaisha.

Wapokea na watoa rushwa wa kwanza ni watunga sheria, nao ni wabunge wa bunge la JMT. Kwanini hawatungi sheria kali za kupambana na rushwa?

tayari wamekula rushwa ili wasitunge sheria hiyo, ushahidi ni huu, siku walipoiita rushwa kwa jina la takrima.
 
tayari wamekula rushwa ili wasitunge sheria hiyo, ushahidi ni huu, siku walipoiita rushwa kwa jina la takrima.

Hapana, takrima ilishawekwa kwenye kundi la rushwa.

Sheria zipo lakini adhabu ni ndogo sana. Zirudishwe zikafanyiwe marekebisho adhabu ya rushwa hata kama umeomba soda tu, iwe ni kifo.
 
Hayo ni matangazo ya kuvutia biashara...Kha! mbona kichwa kigumu wewe? Huelewi?
 
Back
Top Bottom