Ni kweli kwamba Jamii forums, inaandika mambo mengi tena kwa uwazi.Pongezi kubwa sana. Lakini je, ni wangapi wanasoma? Ni wangapi wana uwezo wa kuingia internet? Wale wanaoingia, mbali na kubishana na kutoa hoja mbali mbali ni kiasi gani wanafikisha ujumbe kwa watanzania wengine?
Kuna wakati ninasita kuweka mawazo yangu hapa. Ninafikiri kuna haja yakutafuta njia nyingine ya kufikisha ujumbe. Kuna haja ya kuwafundisha watanzania wakafika mahali pa kusema hapana. Mfano, waseme hapana hatutaki Foleni! Kuna mambo mengi yanawakera watanzania, lakini eti wao ni Amani na utulivu. Foleni ni kero, foleni ni usumbufu na muda mwingi unapotea. Badala ya kufanya kazi watu wanashinda kwenye magari. Leo hii hauna anayeongea namna ya kutanzua tatizo hili. Maana yake ni miaka mingine zaidi ya 5. Kama barabara za kupita juu hazijengwi leo, ni ndoto kwamba zitajengwa ndani ya mwaka mmoja.
Tunaimba kilimo kwanza, kwa mvua zipi? Hakuna mpango wa umwagiliaji. tuna maana ya wawekezaji kuja na kulima? Kuja na kuchukua ardhi yetu?
Nasikitika kuandika haya hapa, maana ningependa watanzania wengi wasikie na kujifunza kusema hapana!
Watanzania waseme hapana kwa Bunge lao, waseme hapana kwa wabunge wasiofika kwenye vikao vya Bunge, waseme hapana kwa maamuzi ya kijinga kama tulivyoshuhudia leo hii; ni lazima wafundishwe! Ni lazima waelekezwe!
Kuna wakati ninasita kuweka mawazo yangu hapa. Ninafikiri kuna haja yakutafuta njia nyingine ya kufikisha ujumbe. Kuna haja ya kuwafundisha watanzania wakafika mahali pa kusema hapana. Mfano, waseme hapana hatutaki Foleni! Kuna mambo mengi yanawakera watanzania, lakini eti wao ni Amani na utulivu. Foleni ni kero, foleni ni usumbufu na muda mwingi unapotea. Badala ya kufanya kazi watu wanashinda kwenye magari. Leo hii hauna anayeongea namna ya kutanzua tatizo hili. Maana yake ni miaka mingine zaidi ya 5. Kama barabara za kupita juu hazijengwi leo, ni ndoto kwamba zitajengwa ndani ya mwaka mmoja.
Tunaimba kilimo kwanza, kwa mvua zipi? Hakuna mpango wa umwagiliaji. tuna maana ya wawekezaji kuja na kulima? Kuja na kuchukua ardhi yetu?
Nasikitika kuandika haya hapa, maana ningependa watanzania wengi wasikie na kujifunza kusema hapana!
Watanzania waseme hapana kwa Bunge lao, waseme hapana kwa wabunge wasiofika kwenye vikao vya Bunge, waseme hapana kwa maamuzi ya kijinga kama tulivyoshuhudia leo hii; ni lazima wafundishwe! Ni lazima waelekezwe!