Ni vigezo au kanuni gani zinaweza kutumiwa kumg'oa spika au manaibu wake.

Jan 16, 2007
721
176
Tangu bunge ili lianze baada ya uchaguzi wa mwaka 2010 chini ya Spika wa bunge Mh.Anne Makinda,tumeshuhudia vituko kutoka kwa baadhi ya wabunge kwa upande mwingine ubabe wa spika na manaibu wake kwa kupendelea upande wa chama tawala CCM na kuzima hoja muhimu kwa maslahi ya nchi zinazotolewa na upande wa upinzani.Hali hii imesababisha muda mwingi kutumika katika marumbano yasiyo na tija kwa mustakabara wa taifa.Ukichunguza kwa undani hali hii inachangiwa na jinsi spika Anna Makinda na wasaidizi wake wanavyoliendesha bunge hili.Hii haijulikana kama ni kutokana na uwezo mdogo wa Spika na wasaidizi wake au ni makusudi wanatumiwa na chama chao tawala ili kuzima hoja za msingi na zenye manufaa kwa taifa kwa sababu chama tawala hakina hoja na majibu kwa jinsi nchi inavyoenda ndivyo sivyo.Naomba kuuliza ilikulinusuru taifa NI VIGEZO AU KANUNI ZIPI ZINAWEZA KUTUMIKA KUWANG'OA VIONGOZI HAO?MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Vigezo vitakavyotumika ni kuvunja bunge na serikali kisha kuingia kwenye uchaguzi.
 
Back
Top Bottom