Ni vifaa gani vinahitajika ili kurusha Live Matangazo ya TV(Tanzania)

Rutunga M

JF-Expert Member
Mar 16, 2009
1,769
1,382
Jamani wadau
kama mmefuatilia matangazo mengi ya uchaguzi katika TV za Tanzania hasa matokeo ya mikoani yamekuwa yakifanywa kwa njia ya simu badala ya kutuonesha picha za video.

hivi ni vifaa gani,vinapatikanaje,gharama zake ili tuvisaidie vituo hivi.Ayu tujue kama wanashindwa kuvinunua kwa sabbu ya ukata au hawaoni umuhimu.

kwa kuwa jukwaa hili halishindwi kitu,tujulishane,tatizo ni nini hasa kwa TV zetu na waandishi wao wa mikoani
 
jamaa vifaa wanavyo vya kutosha, isipokuwa tatizo lipo kwenye njia ya transmission. mara nyingi matangazo hurushwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa kutumia microwave link, satellite au internet.satellite link ya 30 minutes inaweza kugharimu up to $1500, ingawa broaband internet inaweza kuwa $2000 kwa mwezi.

ingawa gharama ni kikwazo kikubwa, kwa kiasi fulani kukosekama kwa ubunifu ndiyo tatizo. watu wanaamua kutumia njia rahisi, kwasababu hakuna broadcaster anayependa kuwa creative.
 
Back
Top Bottom