Ni uwoga kukosa uvumilivu kukosa imani ama!?

Ame

JF-Expert Member
Mar 14, 2011
6,190
5,214
Nipo katika tafakuri kuu!

Ninaamini kuwa invention ni process ambayo inaanza na wazo hatimae wazo kujaribiwa na baada ya kuonekana kuwa lafaa kuendelezwa hadi kufikia level ya consumption. Hii inahitaji resources, political will pamoja na cooperation kati ya mwenye wazo, wanasiasa na raia ambao ni walaji.

Nimekuwa na wazo la muda mrefu la jinsi ya kuleta maendeleo kwa walala hoi wenzangu tatizo langu kubwa nikuwa siamini chama kilicho madarakani kama ni mtu sahihi wa kubeba maono yangu moja likiwa tabia yao ya ufisadi.

Nilitenga muda wa miezi 4 mwaka huu kushirikiana na hao nilioona wafaa kubeba maono yangu katika kuona ni jinsi gani yaweza kuwa reality, tatizo inaonekana viongozi wao wako very busy kiasi ambacho hatuwezi kufanya yale niliyopanga kufanya kwa mwaka huu na muda wangu ndo umefika ukingoni.

Sasa ndipo nikarudi kujiuliza kwa sauti hivi nikuwa nimeogopa bure kuwapa maono waliopo madarakani; ama nimekosa uvumilivu kwa hawa niliowachagua; ama nimekosa imani kwa Mungu aliyenipa haya maono?

Ebu nisaidieni mwenzenu kunipa uwezekano wa lipi la weza kuwa jibu sahihi kwangu ili nisije ingiwa na Ibilisi wa kukata tamaa!
 
Duuh hapa hakuna msamaria hata mmoja aliyejali kuwa kuna mzalendo mmoja yuko katika hatari ya kukata tamaa? Kumbe ndiyo maana hawa wenzangu nao hawakunijali inaonekana impact yangu ndogo....Acha nijipe moyo; 'Jiwe lililokataliwa na waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni'
 
Asanteni sana CDM you gave me chance lakini maadui wakawahi kwakuniwekea mbigiri kwenye njia.... Any way you have got my two silver bullets to shot at the enemy.... If you do it careful and with the invisible supports am extending be assured it is worthy to be in a position which I am in now; God's time is best time as I am told by one of your seniors.

kila laheri makamanda.....
 
Back
Top Bottom