Ni uwendawazimu kupandisha bei ya mafuta ya taa, maji

Kaaazi kweli kweli!
Hadi mwanga wa vibatari mgao!
Umeme juu (japo haupatikani)
Mafuta ya taa juu.
Pole bibi na babu, nawaomba mlale mapema zaidi. Ila msishabikie tena Magamba.com.

Bora ya jana!
 
Tuanzishe umoja wa watumiaji wa mafuta ya taa.
Tuwe na sauti moja, la sivyo inamega upande wetu.
 
Yaani jamani umefika wakati wa kuwa na mjadala wa kitaifa kuhusu mustakabari wa maisha yetu watanzania. Haingii akilini kabisa kuzuia mwizi hasifanye wizi kwa kuwahukumu wanyonge wa nchi hii, kupandisha kodi ya mafuta ya taa ni kuwahukumu wanyonge wa nchii ambao ni zaidi ya wananchi milioni 32 ambao wanategemea nishati hii, ambao kwao umeme wanausikia tu, nadhani idadi hii inaweza kuongezeka kutokana na mgao wa masaa zaidi 18 ambao umikumba nchi yetu sasa. Kwa kifupi zaidi ya wananchi milioni 38 wa nchii sasa wanategemea mafuta ya taa ili kupata mwanga hadimu katika nyumba zao, wengi wa wananchi hawa ni wakulima weanaoishi vijijijini ambao ni zaidi ya 80%. Hii ni ujuma inayofanywa na wadau hawa wanishati kwa wananchi wa nchi hii, kwasababu sasa soko la mafuta haya ya taa ni kubwa kweli, watanzania sasa wanategemea mafuta ya taa badala ya umeme.

Ina maana wataalamu wetu hawa wa EWURA na Wizara ya Nishati hawakuona hili? hii ni ujuma tunafanyiwa mchana kweupe, sasa tumlilie nani? kama hawa tuliowapa dhamana ya kuongoza taasisi hizi hawaoni hili jambo ambalo lipo wazi nani mwingine ataona!. Wanaochakachua mafuta ni wezi, na ni kazi ya vyombo vya Ulinzi na Usalama kuwakamata wezi hawa na kuwapeleka Mahakamani ili wapewe adhabu kali. Vyombo hivyo tunavyo na vipo kwa shughuli hiyo kwa mujibu wa Katiba, sasa inashangaza vipi wanadhibiti wizi huu kwa kuwanyonga wanachi maskini, kwa kuwapandishia bei katika bidhaa ambayo sasa ni mkombozi katika nishati, maana umeme sasa nchi hii umekuwa historia. Hii si sawa kabisa na haikubaliki. Nini kazi ya vyombo vya Usalama katika nchi hii? hatuwezi kutatua matatizo yanayotukabili kwa kuongeza matatizo zaidi kwa wananchi wetu maskini, hii si sawa kabisa. Kazi ya kupambana na WACHAKACHUAJI wapawe vyombo vyetu vya Usalama, nadhani vina Itelegensia ya hali ya juu na kuweza kuwabaini wachakachuaji na kuwafikisha katika vyombo vya Sheria. Hii inawezekana na Wachakachuaji hawa wanajulikana, suala hapa ni kufanya MAAMUZI MAGUMU na kuwatia ndani Wachakajuaji hawa. Kwa mafuta ya TAA sasa = UMEME kwa walalahoi wa nchi hii ambao hatuna uwezo wa kununua Jenereta.

Matatizo ya nchii yatakwisha tu, pale kwa wale wote waliopewa dhamana ya kutuongoza, kama watatuongoza kwa kutumia HEKIMA na si MATUMBO yao.
 
Bila shaka ujumbe unazidi kutufikia taratiibu Watanzania kuhusu wenyewe hasa wenye Serikali yao. Ni ndoto kutegemea serikali iliyopo kuwa na uwezo wa kuwadhibiti "wafanyabiashara wakubwa" wenye kuendesha kila aina ya hujuma dhidi ya nchi kuanzia ukwepaji kodi, uingizaji wa madawa ya kulevya, bidhaa feki, uchakachuaji mafuta, mauaji ya albino, n.k. Hawa ndio makada na wafadhili wakuu wa chama. Hawagusiki. Tushapewa dondoo kadhaa kuhusu mfumo uliopo tangu Sumaye aliporopoka kwa wanaotaka mambo yawaendee mswano waelekee wapi hadi hivi leo katika harakati za kuvuana magamba wanapojisahau na kujiumbua kwa madhambi makubwa.

Na wananchi... hatuna kisingizio wala haja ya kulialia. Uchaguzi ni wetu. Tuendelee na status quo au tuanze kuingiza mabadiliko? Hali ikibaki ilivyo basi tusidanganyane; tuache unafiki; tunaipenda!
 
Nimesoma kwa masikitiko makubwa mojawapo ya magazeti ya leo kuwa kodi ya mafuta ya taa itapanda toka toka sh 52 hadi kufikia sh 400 kwa lita hivyo wamachi watarajie kununua lita moja kwa wastani wa shilingi 1900 sawa na bei ya petroli,sababu hasa ya kupandishwa ni kuzuia uchakachuaji wa diesel unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara!my take: kweli uyu mtu wa ewura hapo ndio mwisho wake wa kufikiria namna ya kuwabana watu hao... Amejaribu hata kuwaza ni watanzania wangapi wanatumia mafuta hayo pengine kuliko hata watumiaji wa dieasel yenyewe? HIVI kweli ni akili hii...........nakuuliza wewe mtu wa ewura na hali hii ya uchumi kuwa ngumu,hatuna umeme tunategemea mafuta hayo umetafakari vyema kweli?hivi tunaelekea wapi jamani...tutaendelea kulia hivi hadi lini,....lini tutaingia barabarani....naona bado freedom ipo mbali sana!!nimeandika kwa uchungu nikiwaza wazazi wangu kule kijijin wanotegemea mafuta hayo kwa taa na kajiko ka mchina ....omg
Mimi mpaka sasa sija amini kama kweli wabunge wote wameona hii ni sawa!!!Yaani hakuna namna nyingine kuzuia uchakachuaji zaidi ya kupandisha bei ya nishati hiyo muhimu kwa watu wa chini???Kweli?Yaani wenzetu toa ushuru kwenye mafuta ya taa sisi tunaongeza eti kuondoa uchakachuaji!!Kweli serikali yetu iko out of touch na maisha yetu halisi, wanajua wote tunapikia gesi na na tuna majenereta!Inauma sana!
 
KWA KWELI NIMELIPOKEA HILI KWA MASIKITIKO MAKUBWA SANA KWA SABABU WANASEMA ETI WAMEPANDISHA KODI ILI KUDHIBITI UCHAKACHUAJI WA MAFUTA SASA HII SERIKALI HAIONI NIKUMKANDAMIZA MTANZANIA WA KIPATO CHA CHINI?KWA HIYO EWURA WAMESHINDA KUWADHIBITI WACHAKACHUAJI WA MAFAUTA?SASA KUNA UMUHIMU GANI WA KUWA NA EWURA NA TBS?

MIMI NADHANI MTU AKICHAKACHUA MAFUTA HUYU NI MUHUJUMU UCHUMI ANATAKIWA KUFUNGWA JELA MIAKA 30 NA KUFILISIWA.jE KWA HILI LIKITENDEKA KUNA MTU ATACHAKACHUA AU WACHAKACHUAJI NI WATU WA SYSTEM NDIO MANA WANAOGOPWA NA WANALINDWA ILI KUMTESA MTANZANIA WA KIPATO CHA CHINI?

UKIENDA KIJIJINI NISHATI INAYOTUMIKA KAMA TAA NI MAFUTA YA TAA HATA HAPA MJINI WATU WALIO WENGI WANAPIKIA MAFUTA YA TAA.SAS JE MITI ITATUNZWA KWELI?WAKATI BEI YA GESI IPO JUU.
 
KWA KWELI NIMELIPOKEA HILI KWA MASIKITIKO MAKUBWA SANA KWA SABABU WANASEMA ETI WAMEPANDISHA KODI ILI KUDHIBITI UCHAKACHUAJI WA MAFUTA SASA HII SERIKALI HAIONI NIKUMKANDAMIZA MTANZANIA WA KIPATO CHA CHINI?KWA HIYO EWURA WAMESHINDA KUWADHIBITI WACHAKACHUAJI WA MAFAUTA?SASA KUNA UMUHIMU GANI WA KUWA NA EWURA NA TBS?MIMI NADHANI MTU AKICHAKACHUA MAFUTA HUYU NI MUHUJUMU UCHUMI ANATAKIWA KUFUNGWA JELA MIAKA 30 NA KUFILISIWA.jE KWA HILI LIKITENDEKA KUNA MTU ATACHAKACHUA AU WACHAKACHUAJI NI WATU WA SYSTEM NDIO MANA WANAOGOPWA NA WANALINDWA ILI KUMTESA MTANZANIA WA KIPATO CHA CHINI?UKIENDA KIJIJINI NISHATI INAYOTUMIKA KAMA TAA NI MAFUTA YA TAA HATA HAPA MJINI WATU WALIO WENGI WANAPIKIA MAFUTA YA TAA.SAS JE MITI ITATUNZWA KWELI?WAKATI BEI YA GESI IPO JUU,.

Ndugu, Aliyenacho huongezewa! HAyo yote ni biashara zao. Mwananchi wa kawaida lazima awaongezee hao jamaa. Suala la ari zaidi, kasi zaidi, nguvu zaidi ndo hilo!
 
This is another lobying, nahakika hili limeamriwa na wauza mafuta wenyewe ili waendelee kuchakachua. Nani asiyejua kuwa mafuta mengi yanayouzwa hapa nchini hukwepa kodi kwa kisingizio kuwa yanaenda nchi za jirani, sasa ndo watachakachua vizuri na wakiulizwa watasema hakuna haja ya kuchakachua kwani bei ya mafuta inalingana.
 
Ni kweli . Wamekurupuka kama kawaida yao. Wanafikiri mzigo wa ndani ndio unatumika kuchakachua kumbe sifuri. Dealers wa mafuta wana network kubwa . Mzigo wa Zambia unarudishwa Tanzania na ndio unatumika kiulainiii? Walala hoi wanaendelea kuumia huku uchakachuaj uko i pale pale.

Nani aliyesema Lori la mafuta haliwezi kwenda Zambia na kurudi na hayo hayo mafuta Tanzania bila shida? Tumieni hizo bongo zenu finyu na sio kutafuta cheap solutions complicated game.
 
Mimi mpaka sasa sija amini kama kweli wabunge wote wameona hii ni sawa!!!Yaani hakuna namna nyingine kuzuia uchakachuaji zaidi ya kupandisha bei ya nishati hiyo muhimu kwa watu wa chini???Kweli?Yaani wenzetu toa ushuru kwenye mafuta ya taa sisi tunaongeza eti kuondoa uchakachuaji!!Kweli serikali yetu iko out of touch na maisha yetu halisi, wanajua wote tunapikia gesi na na tuna majenereta!Inauma sana!
Mkuu, unaongelea wabunge hawa wa ccm! Wao kila jambo linalokuja toka serikalini wanaliunga mkono kwa asilimia 100, wanaogopa wakihoji watavuliwa gamba.
 
Kwa wenye ufahamu vizuri naomba mnisaidie ktk hili swala nililosikia kuwa serikali ilipandisha bei/kodi ya mafuta ya taa ili kuzuia uchakachuaji?

Hainiingii akilini kuwa kupandisha bei ya mafuta taa on expense ya watumiaji ili kuzuia makosa yanayofanywa na wengine...naomba mnifahamishe kwa uzuri sijalifahamu jambo hili linawezekana vipi? Pla JF
 
Kwa wenye ufahamu vizuri naomba mnisaidie ktk hili swala nililosikia kuwa serikali ilipandisha bei/kodi ya mafuta ya taa ili kuzuia uchakachuaji?

Hainiingii akilini kuwa kupandisha bei ya mafuta taa on expense ya watumiaji ili kuzuia makosa yanayofanywa na wengine...naomba mnifahamishe kwa uzuri sijalifahamu jambo hili linawezekana vipi? Pla JF

limeshawezekana mkuu! lita nilikuwa nanunua 1700/= asaivi 2800/=, nategemea zaidi jiko la mchino, sijanunua jiko la gesi bado. mmh! nashindwa kuelewa kwanini wasingeweka bei flat kwa bidhaa yote ya mafuta km ni kupunguza uchakachuaji?
 
Mleta mada ndo utajua kuwa taifa linaongozwa na 'majuha'wa uchumi. Hapa sijamtukana mtu ila kama yeyote ni juha basi nimempa haki yake. Kama yeyote si juha basi usikasirike. Wanachokifanya wachumi wetu majuha ni kwamba wanatumia principle ya kudiskareji bidhaa flani kama wafanyavo kwa pombe na sigara,ila hawakumbuki kuwa hii bidhaa muhimu. Yani kama wangeamua kumlinda mlaji wa kitanzania ambaye hajaona umuhimu wa bidhaa yao matajiri/petrol wala wasingepandisha bei. Narudia watawala wetu ni 'majuha' waliofeli uchumi. Na kwa kuwa tunacheka cheka mbele ya maboksi ya kura ngoja tukome,ifikipo 2015 labda tutaelewa umuhimu wa kura!
 
Kupanda kwa bei ya mafuta kulikotangazwa na serikali ili kuendana na na mafuta mengine kwa kisingizio cha kuwabana wachakachuaji,inaelekea kumuumiza zaidi mwananchi hasa wa kipato cha chini,ambaye lita moja huitumiakwa siku maka mbili tu na kwa bei ya sasa Tshs 2000+,itambidi angalau kwa mwezi awe na 15,000/ kwa ajili ya nishati hiyo.Je wanasiasa na watunga sera tutafika kweli?Maisha yanazidi kuwa magumu jamani.
 
Kwa kweli hata mimi nimewashangaa sana serikali ya CCM. Mafuta ya taa ndo nishati ambayo inatumiwa na 80% ya watanzania walioko vijijini kwa ajili ya mwanga! Huu ni utesaji wa hali juu wa wananchi!
Sielewi CCM wana mkakati gani, maana ni mateso kila mahali! Mjini tunaotegemea umeme, umeme haupo! Kijijini wanategemea mafuta ya taa, wamepandisha bei! Kweli Watanzania hawana mtetezi...:(!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nilishaandika humu kuwa serikali inataka kuhakikisha kwamba mgao wa giza unafika nchi nzima!
 
Ukisikia serikali legelege inayowaabudu wafanyabiashara na wenye mali ndio hii tulionayo sasa. Serikali haiwezi kushindwa kudhibiti uchakachuaji kwa sheria kali na usimamizi wa nguvu badala yake ikaingiza kodi nyingi kwenye mafuta ya taa. Wachakachuaji wanafahamika, shughuli hizi za uchakachuaji zinafanyika wazi, zinahusisha watu wengi tu. Sasa tuna EWURA, TBS, FCC, POLISI, UwT,.....
 
Kupanda kwa bei ya mafuta kulikotangazwa na serikali ili kuendana na na mafuta mengine kwa kisingizio cha kuwabana wachakachuaji,inaelekea kumuumiza zaidi mwananchi hasa wa kipato cha chini,ambaye lita moja huitumiakwa siku maka mbili tu na kwa bei ya sasa Tshs 2000+,itambidi angalau kwa mwezi awe na 15,000/ kwa ajili ya nishati hiyo.Je wanasiasa na watunga sera tutafika kweli?Maisha yanazidi kuwa magumu jamani.
Imenikumbusha siku moja, nilimwona baba mmoja akiwa amebeba mtoto kumsaidia mkwewe wakiwa wametoka hosiptali wanakatiza mitaa ya Upanga kwa miguu. Ghafla akatokea mbwa anawabwekea akimfuata yule baba. Baba wa watu akahamaki kuwa mbwa atamdhuru. Baba akamtupia mbwa Kitoto huku akisema 'wachaaa'.Hawa watu tuliowaweka huko mbele watuongoze wame'behave' kama huyu baba. Wananusuru mashangingi yao kwa kuwatosa walala hoi. Maskini Watanzani!
 
Nyerere alisema vizuri kwamba mkikubali nchi inunuliwe na watu fulani msijutie tena yatakayotokea, sasa nchi imenunuliwa muda mrefu sisi hatuhitaji kujuta wala kushangaa. Cha msingi hapa kama tumeshapata hasira za kutosha tuamue moja maana uwezo tunao. lakini tunapokaa na kushangaa sana wala haisaidii na hakuna la ajabu analoweza kufanya JK maana kwanza yeye mwenyewe hapo alipo sio mali yake, mlishamwona JK akiwa na nguvu katika lipi tangu amechaguliwa nchi hii? Hamuoni hata Mkapa amechukia? Hata kama ni uzembe umeshapita kile kiwango ambacho wananchi wanaweza kuona ni kupitiwa. Sasa hapa kama hasira hazijatosha wala msilalamike ila kusanyeni data kwanza za kutosha kisha tukiona tuko sawa tufanye mambo. Na mimi nitachoweza kusema hapa ni kwamba hatuna haja ya kusubiri uchaguzi, inatakiwa tufanye mpango JK atoke tu taratibu wala si kwa kumwaga damu, najua madaraka matamu kwahiyo huo ni ushauri...ikishindikana taratibu mengine yatayofuata mimi sitaki kuyasema kwa sasa.
 
Back
Top Bottom