Ni utaratibu gani hutumika kusajili kikundi?

tizo1

JF-Expert Member
Mar 9, 2011
856
145
Msaada Jamani.MIMI na Vijana wenzangu 24 wakiume na wakike tumeunda kikundi cha kusaidiana kijamii, kiuchumi n.k.lengo kubwa ni kupeana nguvu katika maswala ya elimu,Harusi ,maradh na Misiba.JE NI Utaratibu gani hutumika kusajili Kikundi?je ni vitu gani vya Kuandaa kama Viambatanisho?JE NI OFISI GANI HUSHUGHULIKA NA HAYA MAMBO YA Usajili??MSAADA TAFADHARI
 
Wakuu nawategemea kwa msaada zaidi wa jambo hili.tafadhali msinitupe
 
Vizuri kama ungejieleza zaidi kuwa kikundi hiki kipo wapi, mji gani, kusaidiana vipi?..maana kusaidiana pekee haitoshi inatakiwa utueleze kama ni wafanya biashara au mna shughuli gani ktk kusaidiana huko. Kama mnasaidiana wenyewe tokana na mapato ya kila mtu mkicheza Upatu, ushirika huu sidhani kama kuna usajili isipokuwa mnaweza kumtafuta wakili ambaye atasimamia haki za makubaliano yenu...Funguka mkuu au unaweza niandikia PM kunipa picha nzima..
 
Kusaidiana huku ni kwa kutoa pesa toka mifukoni mwetu.Kikundi kipo mkoani Tabora.Hakuna chanzo cha mapato zaid ya mifuko yetu binafsi.Kwa mfano tulikubaliana ada ya uanachama ni sh 3000 kila mwezi.mtu akiumwa kila mtu atatoa 1000 kumchangia na Mfuko utatoa 20000 na jumla zinakuwa 44000 kwa mgonjwa.mtu akioa au kuolewa tumepatana kima cha chini cha mchango kiwe elfu kumi kwa kila mwanachama.MAKUBALIANO HAYA TULIKUBALIANA PAMOJA NA YANAKWENDA SAMBAMBA NA HALI ZETU ZA UCHUMI.NDO TUNAANZA MKUU
 
Back
Top Bottom