luckyperc
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 495
- 46
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hawana faida yoyote zaidi ya kupeleka faida yote ya hela wanayopata kwao India thru bank zao.Zaidi ya hapo wamehonga hela mafisadi ya NHC kote nchini na kukaa ndani ya nyumba za NHC huku wazalendo watanzania halisi wakikosa nyumba!
mkuu mchango wao ni kama hivi
View attachment 30930
Sijui umetembea wapi na wapi ndugu, lakini nchi zingine wahindi hao hao tunaowalaumu sisi wanafanya kazi kwa bidii na wanachangia maendeleo ya nchi walizofikia kama raia wengine wa asili wa mahali hapo.Ni madaktari, IT pros, wanasheria, actuaries, na kama nyumbani pia nchi zingine walipo wengi ni wafanyabiashara wa rejareja. Wanalipa kodi, wapo serikalini n.k. Tutazunguka zunguka wee.... tutarudi palepale, serikali yetu ni mzaha mwingi. Sheria hazifanyi kazi. Kwa nini watu haoahao wawe productive members of society na kwetu wawe villains.Mchango wao upo kwenye bishara kama za EPA,Richmond,na ujanja ujanja mwingine wa deal feki
Ninachoshangaa mimi ni kwamba "wahindi" siyo polisi. polisi ni sisi. wahindi ni watoa rushwa, wezi, walanguzi, wakwepa kodi... na wakati huohuo hamna wahindi serikalini kote. sasa cha kujiuliza kwa nini sisi polisi,PCCB na vyombo vingine vya usalama haviwafikishi kwenye vyombo vya sheria? "wahindi" wanapotoa rushwa, wanampa nani?
Kwa nini mnawalamu wahindi badala ya serikali yenu? Mnaelekeza lawama mahali pasipo. Hao "wahindi" wa madukani wakiondoka wote, mtahamia kwa Wanyakyusa wa Bima, baadaye Wachaga wa TRA, Wakurya jeshini....dhambi ya ubaguzi haiishi.
Ziara ya indian officials hapa Tanzania ni wasaa muafaka wa kutafakari umuhimu na uwajibikaji wa jamii ya kihindi hapa Tanzania.
Je kuna tija yoyote?
Wanajenga hospitali ya Open heart surgery mlimani city