Mwana dada Shyrose Bhanji amemtolea uvivu Mzee Johni Chiligati alipo post kwenye ukurasa wake wa faacebook kauli mbiu yao ya
"TUMETHUBUTU,TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE!"
Mwana Dada Shyrose akamwandikia mzee Chiligati maneno haya
Hayo ni maneno makali sana kutoka kwa mwanadada Shyrose, ana muona wa mbali sana tofauti na wana CCM wengine ambao hawataki kukubaliana na ukweli kwamba CCM inaelekea kufa.
"TUMETHUBUTU,TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE!"
Mwana Dada Shyrose akamwandikia mzee Chiligati maneno haya
@Mhe. John Chiligati. kauli mbiu kama hizi ndizo zinazoturudisha nyuma. Tazizo moja kwenye Serikali ya CCM tunaongoza kwa kauli mbiu lakini utekelezaji ndiyo kasheshe...huu siyo tena wakati wa mbwembwe za kauli mbiu, ila kikubwa kinachotakiwa ni utekelezaji. Mimi naomba nikwambie ukweli kuhusu mtazamo wa watanzania leo juu ya chama chetu CCM...
Wananchi wengi sana wameanza kukosa imani na CCM kutokana na fitna, majungu, unafiki wa kumsifia Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete hata pale anapoharibu. Ni ukweli usiopingika kwamba leo hii CCM iko katika hali mbaya kimtazamo mbele ya macho ya jamii. Je unalifahamu hili Mhe Chilligati? Je unafahamu kwamba wananchi wameanza kuichoka CCM? Je unafahamu kwamba Rais JK ndiyo kiongozi anayechangia kwa kiasi kikubwa sana kukigawa hichi chama chetu
hivi mnamwambia ukweli wa mambo au mnampotosha kwa kutomwambia ukweli? Nitashukuru sana ukimfikishia ujumbe wangu JK kwamba style yake ya uongozi ndani ya chama chetu na akiwa kama mkuu wa nchi inalalamikiwa sana huku mitaani, hata na mwananchi wa kawaida...kila mtu anauliza JK yuko wapi? mbona yuko kimya sana? Mwambie wananchi wanataka kuskia kauli yake nchi inapoelekea kwani kila kikicha kuna matatizo lukuki...kwa leo ni hayo tu Mhe. Chilligati...naomba kuwasilisha!
Hayo ni maneno makali sana kutoka kwa mwanadada Shyrose, ana muona wa mbali sana tofauti na wana CCM wengine ambao hawataki kukubaliana na ukweli kwamba CCM inaelekea kufa.