Ni ugonjwa au ni imani?

PSI Factor

Member
Apr 21, 2011
32
143
Wakuu,

Nina tatizo moja ambalo sijui kama binadamu wenzangu mnalo. Tatizo hili ni tangu nikiwa mtoto (miaka ya 70) na nimeendelea kuwa nalo.

TATIZO:

Nikikiangalia (au kusikiliza) kitu kwa muda mrefu huwa napata sura zaidi ya 4 ya kitu hicho. Sipendi hii hali na inaninyima raha sana.

Mifano:

Nikiiangalia picha moja naweza kukuonyesha hata vingine ambavyo wewe kama mwangaliaji hukuviona kwa haraka. Nikimwangalia mwadamu mwenzangu usoni wakati anaongea naweza kusahau kusikiliza nikaendelea kumwangalia kwa kama dakika 10 nikaweza kujua kama ni mwongo, mkweli, anafanya ushirikina n.k.

Nimeoa, nikimwangalia sana mke wangu huwa najiuliza sana nini kilinisababishia nikaoana na mtu huyu, lakini nikiondoka kwenye concentration ya kuangalia basi namwona wa kawaida na anapendeza kweli.

Hata kusikiliza hali ipo vilevile, nikisikiliza sauti ya mtu au mnyama napata hisia mbaya kiasi nafikia kusikia kama wanyama wanaongea, hii hunisaidia hasa nikikutana na mbwa au paka, nikikaa na mbwa hata kama ana kichaa huwa hanisumbui, wananikimbilia.

Nakumbuka wakati JK anaanguka Jangwani nilikuwa namwangalia kwenye TV, aliposema "I see" nikamwambia jamaa yangu pembeni 'anaanguka' hata haikuchukua dakika akaanguka. Niliona kama ameanza kulegea, sikuwa namsikiliza nilikuwa namwangalia usoni.

UTOTONI: Niliwahi kuiangalia picha nikaona kama inatoa machozi, picha hii ilikuwa ya Bikra Maria (mimi mkristo), lakini nilipomwambia marehemu mamangu yeye alisema ni hisia tu, akasema labda nilihadithiwa kuwa Maria analia. Tatizo ni kuwa niliiangalia sana picha ile kwakuwa ilikuwa mara yangu ya kwanza kuona sanamu kubwa kiasi kile. Sikuwa nimehadithiwa kama mama alivyofikiri.

UKUBWANI: Niliwahi kuhudhuria semina moja ya kusoma body languages, hii haimaanishi kuwa ndiyo imeniletea tatizo hili, hata mwalimu aliyekuwa anatoa semina hii nilikuwa nikimwangalia sana niliona alikuwa hajiamini. Nilipomwambia kwa nje kuwa kuna vitu alitwambia lakini alionekana kutokuwa na uhakika navyo alikiri ni kweli.

OMBI:
Niliambiwa na rafiki yangu ninayefanya naye kazi ofisi moja kuwa nikiwauliza waungwana hapa kutakuwa na wataalam wanaoweza kunisaidia. Naomba msinichukulie kiutani mwenzenu, ni tatizo linaloninyima raha. Ningependa kujua ni tatizo? Chanzo ni nini? Nifanye nini? Kuna dawa ya kuzuia hali hii?
 
kwa fikra zangu na mawazo yangu wewe katika Macho yako na akili yako Mwenyeezi Mungu kakupa kipaji na nguvu fulani ya asili ndio maana waweza kuhisi kitu na kikatokea watu wa namna hii ni wachache sana duniani. mimi pia nina tabia hiyo inafanana kama ya kwako lakini mimi

huwa nikizungumza na mtu huwa namuangalia sana Usoni na nikaweza kumjuwa huyo mtu ni muongo au mkweli, mimi kwenye familia yangu nimezaliwa Mapacha yaani Tweens mwenzangu alikuwa ni Mwanamke mimi ni Mwanamme kwa lugha ya kizaramo tunasema hivi Kulwa na doto

mimi ndio wa kwanza kutoka katika tumbo la mama yangu nikaitwa kulwa kwa jina la utani mwenzangu alichelewa dakika kutoka tumboni akaitwa doto. Na huyo mwenzangu alifariki Mwaka 1991 na kuhusu kifo chake niliwahi kumueleza mama huo mwaka kama kutatokea Kifo katika

nyumba yetu mama yangu alishangaa sana na kuniogopa hicho ni kipaji toka kwa Mwenyeezi Mungu tu. Kwa hiyo inategemea wewe mwenzangu umezaliwa lini? na wewe ni wangapi katika familia yenu. wewe kwa mawazo yangu kama ungesomea kazi ya Uhakimu, Polisi, Utabiri,au kazi ya (psychology) saikolojia hizo kazi mojawapo ingelikufaa kwa hicho kipaji chako. huo sio Ugonjwa bali Nguvu fulani aliyekupa

Mwenyeezi Mungu. Inapokutokea hivyo jaribu kujishughulisha na kazi yoyote ile ili mradi uwe busy kwa kitu fulani na usipende kila mtu kumueleza hayo sio maradhi jaribu kwenda kwa mchungaji akuombee kwa Mungu yatapunguwa au nenda kanisani kaombe Dua zako kwa Mungu matatizo yatakwisha huo ndio ushauri wangu.
 
Unataka kusema unataka kuwa kama sherh yy haya bwana hii bongo inia kichwa kichwa watu wakutoakafara
ukiwa na shida hizo hisia zako zitatoka
conquest-god knows than uuuuu
 
Ungekua mzungu, ungekua mbali sana.

Wakina Newton, Galileo,nk walikua na maono kama yako, afu wakayafanyia kazi.
 
labda wewe ni psychic.una uwezo wa kuona vitu ambavyo mtu wa kawaida hawezi kuona.kwa uonaji wako,ukimwangalia mtu au ukiona picha ya mtu au ukiangalia sehemu kwa makini unaona vitu ambavyo mtu wa kawaida hawezi kuona.ila sina uhakika/wengine huwaona mpaka watu waliokwisha kufa
 
mkuu we ni moja ya watu wengi sana ambao wan super power..hii huwa wanazaliwa nayo...tatizo hapa tanzania ukimweleza mtu kuhusu wewe anabaki kukushangaa...ndo maana wengi hujificha na anyoona au kusikia inakua siri yake..mm nina jamaa tulisoma nae chuo alikua kama ww ila yeye alikua anaona visivyoonekana including wachawi...
 
mkuu we ni moja ya watu wengi sana ambao wan super power..hii huwa wanazaliwa nayo...tatizo hapa tanzania ukimweleza mtu kuhusu wewe anabaki kukushangaa...ndo maana wengi hujificha na anyoona au kusikia inakua siri yake..mm nina jamaa tulisoma nae chuo alikua kama ww ila yeye alikua anaona visivyoonekana including wachawi...

natural super power :A S 114:.. hakuna kitu kama hicho...!!! wewe haha, kuona visivyoonekana either you are psychic :der: or wewe ni mchawi pia .. ! mkuu usinambia unawaamini wale wanaocheza mazingaobwe, au unadhani mtu kama super he really do exist!
 
Wakuu,Nina tatizo moja ambalo sijui kama binadamu wenzangu mnalo. Tatizo hili ni tangu nikiwa mtoto (miaka ya 70) na nimeendelea kuwa nalo.TATIZO:Nikikiangalia (au kusikiliza) kitu kwa muda mrefu huwa napata sura zaidi ya 4 ya kitu hicho. Sipendi hii hali na inaninyima raha sana.Mifano:Nikiiangalia picha moja naweza kukuonyesha hata vingine ambavyo wewe kama mwangaliaji hukuviona kwa haraka. Nikimwangalia mwadamu mwenzangu usoni wakati anaongea naweza kusahau kusikiliza nikaendelea kumwangalia kwa kama dakika 10 nikaweza kujua kama ni mwongo, mkweli, anafanya ushirikina n.k.Nimeoa, nikimwangalia sana mke wangu huwa najiuliza sana nini kilinisababishia nikaoana na mtu huyu, lakini nikiondoka kwenye concentration ya kuangalia basi namwona wa kawaida na anapendeza kweli.Hata kusikiliza hali ipo vilevile, nikisikiliza sauti ya mtu au mnyama napata hisia mbaya kiasi nafikia kusikia kama wanyama wanaongea, hii hunisaidia hasa nikikutana na mbwa au paka, nikikaa na mbwa hata kama ana kichaa huwa hanisumbui, wananikimbilia.Nakumbuka wakati JK anaanguka Jangwani nilikuwa namwangalia kwenye TV, aliposema "I see" nikamwambia jamaa yangu pembeni 'anaanguka' hata haikuchukua dakika akaanguka. Niliona kama ameanza kulegea, sikuwa namsikiliza nilikuwa namwangalia usoni.UTOTONI: Niliwahi kuiangalia picha nikaona kama inatoa machozi, picha hii ilikuwa ya Bikra Maria (mimi mkristo), lakini nilipomwambia marehemu mamangu yeye alisema ni hisia tu, akasema labda nilihadithiwa kuwa Maria analia. Tatizo ni kuwa niliiangalia sana picha ile kwakuwa ilikuwa mara yangu ya kwanza kuona sanamu kubwa kiasi kile. Sikuwa nimehadithiwa kama mama alivyofikiri.UKUBWANI: Niliwahi kuhudhuria semina moja ya kusoma body languages, hii haimaanishi kuwa ndiyo imeniletea tatizo hili, hata mwalimu aliyekuwa anatoa semina hii nilikuwa nikimwangalia sana niliona alikuwa hajiamini. Nilipomwambia kwa nje kuwa kuna vitu alitwambia lakini alionekana kutokuwa na uhakika navyo alikiri ni kweli.OMBI:Niliambiwa na rafiki yangu ninayefanya naye kazi ofisi moja kuwa nikiwauliza waungwana hapa kutakuwa na wataalam wanaoweza kunisaidia. Naomba msinichukulie kiutani mwenzenu, ni tatizo linaloninyima raha. Ningependa kujua ni tatizo? Chanzo ni nini? Nifanye nini? Kuna dawa ya kuzuia hali hii?
Mkuu huo si ugonjwa.Nakumbuka miaka 17 iliyopita niliwahi kuelezwa na classmate juu ya HALI HIYO,NA NILIPOJARIBU KUTAZAMA SEHEMU 1 NILIONA MAMBO MENGI.Kifupi ni suala hili limegawanyika makundi 2,la kwanza yaweza kuwa ni IMANI. Kuna IMANI inayoitwa MEDITATION & CONSTRATION FAITH. Ambao ibada yao huwa ni kutazama au kufikiria kitu kimoja hadi pale unaposikia/kuona vitu zaidi ya vile halisi unavyo sikia/kuona. IEPUKE ITAKUTESA!Na Upande wa pili huwa ni hali ya ama kuzaliwa nayo au inayohusiana na mambo ya NGUVU ZA GIZA. nitarudi kwa UFAFANUZI.ILA EPUKA KUTAZAMA/KUFIKIRI NA KUSIKILIZA KITU KIMOJA KWA MUDA MREFU
 
mkuu we ni moja ya watu wengi sana ambao wan super power..hii huwa wanazaliwa nayo...tatizo hapa tanzania ukimweleza mtu kuhusu wewe anabaki kukushangaa...ndo maana wengi hujificha na anyoona au kusikia inakua siri yake..mm nina jamaa tulisoma nae chuo alikua kama ww ila yeye alikua anaona visivyoonekana including wachawi...

hivi vitu vipo ni nguvu za asili watu wengi wanavyo ila hawajitambui na wala watu wa karibu yao hawawezi kuwaamini sidhani kama ni tatizo la kidaktari, niliwahi kukaa na mtu kwenye daladala anaongea na simu anajibushana lakini hiyo simu haionekani wala haijaonekana ikiita alivyomaliza akarudisha kitu mfukoni.vp ulishaenda kwa madaktari na wakasemaje,
 
Inawezekana ikawa ni nguvu kutoka kwa Mungu au kutoka kwa shetani. Kama ni nguvu ya Mungu unaweza kuwa kama T.Joshua wa Emmanuel TV na kama ni ya shetani unaweza kuwa Mganga wa kienyeji au mnajimu ni vizuri ukaeleze shida yako kwa wachungaji wanaofanya huduma za maombezi ili iweze kujulikana ni nguvu ipi kati ya hizo mbili inatenda kazi ndani yako. Kwangu mimi naona ni suala la kiimani ila wanasayansi au watu wa saikolojia wanaweza kukuambia kuwa ni ugonjwa.
 
Wakuu,

Nina tatizo moja ambalo sijui kama binadamu wenzangu mnalo. Tatizo hili ni tangu nikiwa mtoto (miaka ya 70) na nimeendelea kuwa nalo.

TATIZO:

Nikikiangalia (au kusikiliza) kitu kwa muda mrefu huwa napata sura zaidi ya 4 ya kitu hicho. Sipendi hii hali na inaninyima raha sana.

Mifano:

Nikiiangalia picha moja naweza kukuonyesha hata vingine ambavyo wewe kama mwangaliaji hukuviona kwa haraka. Nikimwangalia mwadamu mwenzangu usoni wakati anaongea naweza kusahau kusikiliza nikaendelea kumwangalia kwa kama dakika 10 nikaweza kujua kama ni mwongo, mkweli, anafanya ushirikina n.k.

Nimeoa, nikimwangalia sana mke wangu huwa najiuliza sana nini kilinisababishia nikaoana na mtu huyu, lakini nikiondoka kwenye concentration ya kuangalia basi namwona wa kawaida na anapendeza kweli.

Hata kusikiliza hali ipo vilevile, nikisikiliza sauti ya mtu au mnyama napata hisia mbaya kiasi nafikia kusikia kama wanyama wanaongea, hii hunisaidia hasa nikikutana na mbwa au paka, nikikaa na mbwa hata kama ana kichaa huwa hanisumbui, wananikimbilia.

Nakumbuka wakati JK anaanguka Jangwani nilikuwa namwangalia kwenye TV, aliposema "I see" nikamwambia jamaa yangu pembeni 'anaanguka' hata haikuchukua dakika akaanguka. Niliona kama ameanza kulegea, sikuwa namsikiliza nilikuwa namwangalia usoni.

UTOTONI: Niliwahi kuiangalia picha nikaona kama inatoa machozi, picha hii ilikuwa ya Bikra Maria (mimi mkristo), lakini nilipomwambia marehemu mamangu yeye alisema ni hisia tu, akasema labda nilihadithiwa kuwa Maria analia. Tatizo ni kuwa niliiangalia sana picha ile kwakuwa ilikuwa mara yangu ya kwanza kuona sanamu kubwa kiasi kile. Sikuwa nimehadithiwa kama mama alivyofikiri.

UKUBWANI: Niliwahi kuhudhuria semina moja ya kusoma body languages, hii haimaanishi kuwa ndiyo imeniletea tatizo hili, hata mwalimu aliyekuwa anatoa semina hii nilikuwa nikimwangalia sana niliona alikuwa hajiamini. Nilipomwambia kwa nje kuwa kuna vitu alitwambia lakini alionekana kutokuwa na uhakika navyo alikiri ni kweli.

OMBI:
Niliambiwa na rafiki yangu ninayefanya naye kazi ofisi moja kuwa nikiwauliza waungwana hapa kutakuwa na wataalam wanaoweza kunisaidia. Naomba msinichukulie kiutani mwenzenu, ni tatizo linaloninyima raha. Ningependa kujua ni tatizo? Chanzo ni nini? Nifanye nini? Kuna dawa ya kuzuia hali hii?
Piga goti, muombe Mungu akufungue ili ujue ni yeye au siye aliyekupa hizo Nguvu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom