Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,988
Tunaambiwa kuwa tuwe tayari kutoa maoni yetu kwenye hii tuma inayopendekezwa. Kwamba, watu wajitokeze kwa wingi kutoa maoni yao na maoni hayo yatakusanywa na kuratibiwa na baadaye kufanyiwa kazi. Wapo ambao wameshakubali prima facie kuwa kutoa maoni ndicho kitu tunachokitaka na kwamba kwa vile nafasi imepatikana basi watu watoe maoni yao halafu wasubiri kuona kitakachofuata.
Nimebakia kufikiria na kutafuta mfano wa Tume ya Rais yoyote huko nyuma ambayo ilisikilizwa na Serikali kwa asilimia mia moja. Najiuliza ni tume ipi iliyoundwa na Rais ambayo ilikusanya maoni ya wananchi halafu maoni yale yakazingatiwa kabisa na kukubaliwa na serikali. HIvi, tume hii ikikusanya maoni ambayo serikali haitaki wananchi watafanya nini?
Tume ya Nyalali (Chini ya Urais wa Mzee Mwinyi)- Tume hii iliundwa na Mzee Mwinyi kukusanya maoni ya Watanzania kuhusu mambo mbalimbali yanayohusiana na demokrasia na sheria. Miaka ishirini baadaye, maoni ya Watanzania yaliyotolewa kwa tume hii hayakutekelezwa yote na mengine yalikataliwa na serikali.
Tume ya Kisanga (chini ya Urais wa Ben Mkapa)- hii ilikuwa ni katika kufuatilia White Paper ya serikali na kama wengi wanakumbuka ripoti yake ilikataliwa na serikali kwa sehemu kubwa na kuwa ilienda zaidi ya kazi iliyotumwa kufanya. Baadhi ya mapendekezo yalifanyiwa kazi lakini mengine yalikataliwa kwa sababu serikali haikupenda maoni hayo. Prof. Peter Maina anaandika hivi kwenye mojawapo ya kazi zake kuhusu hili "The government kept its work, in an unprecedented fashion, after reading the report for a month and without releasing it to the public, the President decided to blast the Kisanga Committee for going beyond its mandate by making recommendations which were not in conformity with the views of the people [read here views of the government]. On his side, the Chairman of the Committee informed the press that he would not enter into a debate with the President and that the President was entitled to his own views and could pick whatever he found useful in the report. With this the whole momentum built through the work of the Committee was lost. That meant that another opportunity to meaningfully better the Constitution of the country was lost"
Tume ya Bomani - kwa wanaokumbuka hii ni mojawapo ya tume ambayo iliundwa na RAis Kikwete (2007) ili kupitia sekta ya madini na kutoa mapendekezo yake. Tume hii - wengine tulipinga mapema - ilitarajiwa kuja na mapendekezo ambayo yangeweza kabisa kubadilisha mwelekeo wa sekta ya madini nchini na hivyo kutengeneza kile ambacho Rais Kikwete alikiita "win win win situation". Tume ilitoa ripoti nzuri na ya kufurahisha. Miaka minne baadaye mapendekezo yake kadhaa yamefanyiwa kazi na mengine ndiyo 'hivyo tena'.
Kumbe tuna ushahidi wa kutosha wa kihistoria usiopingika kuwa Tume ya Rais ya kukusanya maoni haina maana kuwa maoni ya yatakayokusanywa yatakubaliwa kwani mwisho wa siku ni wao serikali (na siyo wananchi) ambao wataamua ni maoni yapi ya kuyakubali hata kama ni ya wananchi wengi. Kwa mfano, wengi tunafahamu kuwa uamuzi wa kuingia kwenye vyama vingi ulichukuliwa kinyume na matakwa ya wananchi wengi (asilimia 80 walitaka tuendelee chini ya chama kimoja). Je yawezekana Watanzania wengi walikuwa sahihi kuwa tungeendelea kwenye chama kimoja ila mabadiliko fulani muhimu yangetakiwa? Kama Serikali kweli 'inasikiliza' wananchi wake tungekuwa bado kwenye chama kimoja! Kwa ufupi ni kuwa serikali iliamua kukataa maoni ya wananchi na kuchukua maoni ya kikundi cha watu wachache. Yawezekana ndio chanzo cha mgongano uliopo sasa?
Lakini baada ya kusema hayo swali langu linabakia. Je ni tume gani ya Rais ya kukusanya maoni huko nyuma ambayo ilifanya kazi yake na maoni yake yakasikilizwa na serikali bila kukataliwa au kupuuzwa? Kwa nini ni vigumu wakati mwingine kwa serikali kukubali maoni ambayo imeyataka kutoka kwa wananchi? Je, ni kwanini wapo wanaoamini kuwa katika "tume" hii ambayo inapendekezwa kwenye mchakato wa Katiba maoni yake yatasikilizwa na serikali wakati Sheria iliyopitishwa hailazimishi serikali kukubali maoni hayo ya wananchi?
Nimebakia kufikiria na kutafuta mfano wa Tume ya Rais yoyote huko nyuma ambayo ilisikilizwa na Serikali kwa asilimia mia moja. Najiuliza ni tume ipi iliyoundwa na Rais ambayo ilikusanya maoni ya wananchi halafu maoni yale yakazingatiwa kabisa na kukubaliwa na serikali. HIvi, tume hii ikikusanya maoni ambayo serikali haitaki wananchi watafanya nini?
Tume ya Nyalali (Chini ya Urais wa Mzee Mwinyi)- Tume hii iliundwa na Mzee Mwinyi kukusanya maoni ya Watanzania kuhusu mambo mbalimbali yanayohusiana na demokrasia na sheria. Miaka ishirini baadaye, maoni ya Watanzania yaliyotolewa kwa tume hii hayakutekelezwa yote na mengine yalikataliwa na serikali.
Tume ya Kisanga (chini ya Urais wa Ben Mkapa)- hii ilikuwa ni katika kufuatilia White Paper ya serikali na kama wengi wanakumbuka ripoti yake ilikataliwa na serikali kwa sehemu kubwa na kuwa ilienda zaidi ya kazi iliyotumwa kufanya. Baadhi ya mapendekezo yalifanyiwa kazi lakini mengine yalikataliwa kwa sababu serikali haikupenda maoni hayo. Prof. Peter Maina anaandika hivi kwenye mojawapo ya kazi zake kuhusu hili "The government kept its work, in an unprecedented fashion, after reading the report for a month and without releasing it to the public, the President decided to blast the Kisanga Committee for going beyond its mandate by making recommendations which were not in conformity with the views of the people [read here views of the government]. On his side, the Chairman of the Committee informed the press that he would not enter into a debate with the President and that the President was entitled to his own views and could pick whatever he found useful in the report. With this the whole momentum built through the work of the Committee was lost. That meant that another opportunity to meaningfully better the Constitution of the country was lost"
Tume ya Bomani - kwa wanaokumbuka hii ni mojawapo ya tume ambayo iliundwa na RAis Kikwete (2007) ili kupitia sekta ya madini na kutoa mapendekezo yake. Tume hii - wengine tulipinga mapema - ilitarajiwa kuja na mapendekezo ambayo yangeweza kabisa kubadilisha mwelekeo wa sekta ya madini nchini na hivyo kutengeneza kile ambacho Rais Kikwete alikiita "win win win situation". Tume ilitoa ripoti nzuri na ya kufurahisha. Miaka minne baadaye mapendekezo yake kadhaa yamefanyiwa kazi na mengine ndiyo 'hivyo tena'.
Kumbe tuna ushahidi wa kutosha wa kihistoria usiopingika kuwa Tume ya Rais ya kukusanya maoni haina maana kuwa maoni ya yatakayokusanywa yatakubaliwa kwani mwisho wa siku ni wao serikali (na siyo wananchi) ambao wataamua ni maoni yapi ya kuyakubali hata kama ni ya wananchi wengi. Kwa mfano, wengi tunafahamu kuwa uamuzi wa kuingia kwenye vyama vingi ulichukuliwa kinyume na matakwa ya wananchi wengi (asilimia 80 walitaka tuendelee chini ya chama kimoja). Je yawezekana Watanzania wengi walikuwa sahihi kuwa tungeendelea kwenye chama kimoja ila mabadiliko fulani muhimu yangetakiwa? Kama Serikali kweli 'inasikiliza' wananchi wake tungekuwa bado kwenye chama kimoja! Kwa ufupi ni kuwa serikali iliamua kukataa maoni ya wananchi na kuchukua maoni ya kikundi cha watu wachache. Yawezekana ndio chanzo cha mgongano uliopo sasa?
Lakini baada ya kusema hayo swali langu linabakia. Je ni tume gani ya Rais ya kukusanya maoni huko nyuma ambayo ilifanya kazi yake na maoni yake yakasikilizwa na serikali bila kukataliwa au kupuuzwa? Kwa nini ni vigumu wakati mwingine kwa serikali kukubali maoni ambayo imeyataka kutoka kwa wananchi? Je, ni kwanini wapo wanaoamini kuwa katika "tume" hii ambayo inapendekezwa kwenye mchakato wa Katiba maoni yake yatasikilizwa na serikali wakati Sheria iliyopitishwa hailazimishi serikali kukubali maoni hayo ya wananchi?