Ni sawa Marekani kuwasaka Boko haramu Leader's?

mshikachuma

JF-Expert Member
Dec 2, 2010
2,853
626
Jamani siku mbili zilizopita Serikali ya Marekani imetangaza kuwa imewaweka viongozi 3 wa kikundi cha Boko haramu
cha Nigeria kwenye list ya most wanted people in the world...watawasaka kwa udi na uvumba mpaka wawashike no
matter wakiwa hai au wamekufa lakini wanawahitaji tu. - Sasa maswali yangu ni

1.Kwanini ni Boko haramu tu? mbona hawakutangaza hivi kwa Al-shabaab ya somalia while wote ni magaidi?
2.Je ikatokea wamefanikisha kuwakamata na kuwauwa au kuwafunga maisha, Je Nigeria itakalika salama? au
ndiyo itakuwa mwanzo wa vifo vingine kutoka kwa Boko haramu?.
3.Je ni kweli Boko haramu ni watetezi wa dini ya kiislamu huko Nigeria au ni kikundi cha wahuni tu?

Kwa wale wataalamu wa mambo ya kidiplomasia naombeni mnijuze Saga hili kwa faida yangu na wanaJF wengine.

Shukrani....na nawasilisha
 
Marekani wamechelewa sana kuchukua hatua hii wasakwe haraka sana hata ikibidi wakiuawa sawa tu! watu wanaua watu wasio na hatia wakkristo wakiwa makanisani! Al-shabab nao wanashugulikiwa, A-qaeda wanafuatiliwa! kwamba nigeria haitakalika? kwani kuwaacha ndio inakalika?? Vunja uti wa mgongo wa Boko Haramu!
 
Unauliza kama ni Boko Haram peke yake? Mbona muda mrefu Marekani imekuwa inawasaka Al Shabab kule Somalia kwa kutumia drones? Unakumbuka yule Mkomoro aliyekuwa Al Qaida aliyetafutwa kwa muda mrefu? Mbona alitunguliwa na kamzinga ka drone huko Somalia? Hawa magaidi kila wanakochipuka ni kuwatungua tu kwa sababu wakiachiwa washamiri wanatoa fursa kwa Al Qaida kujiimarisha.
 
Watunguliwe tu ni wauaji hawa. Wafutiliwe mbali. Al- shababu, Al- Qaida, Al- Boko haramu ( Na kwa nini majini yao yanaanzia na Al Al tu?) Wanachafua dini ya kiislamu hawa. Wafatwe kote hata kama wamejificha misikitini. Nina imani Obama ataweza kazi hii. Mzigo mzito mpe mjaruo.
 
Marekani wamechelewa sana kuchukua hatua hii wasakwe haraka sana hata ikibidi wakiuawa sawa tu! watu wanaua watu wasio na hatia wakkristo wakiwa makanisani! Al-shabab nao wanashugulikiwa, A-qaeda wanafuatiliwa! kwamba nigeria haitakalika? kwani kuwaacha ndio inakalika?? Vunja uti wa mgongo wa Boko Haramu!
Nimekusoma mkuu!...Je kwa mtizamo wako unaona Boko haramu ni watetezi wa Uislam au ni kikundi cha wauni tu?
 
Watunguliwe tu ni wauaji hawa. Wafutiliwe mbali. Al- shababu, Al- Qaida, Al- Boko haramu ( Na kwa nini majini yao yanaanzia na Al Al tu?) Wanachafua dini ya kiislamu hawa. Wafatwe kote hata kama wamejificha misikitini. Nina imani Obama ataweza kazi hii. Mzigo mzito mpe mjaruo.
Hapo kwenye bold....sijawahi sikia hawa watu wanajificha misikitini ila mara nyingi nasikia hawa watu wanaishi porini na
milimani
 
Nimekusoma mkuu!...Je kwa mtizamo wako unaona Boko haramu ni watetezi wa Uislam au ni kikundi cha wauni tu?
Ni Kikundi cha wahuni wanaotumia mwavuli wa dini najua uislamu siku zote unahubiri amani upendo na kuvumiliana sina utalaam sana na maandiko ya kiislamu ila nina uhakika hakuna uislamu unposema uchome makanisa, uue wakkristo na kuhamasisha vitendo vya kihalifu hao ni wahuni na magaidi ila wamevaa ngozi ya dini!!
 
Jamani siku mbili zilizopita Serikali ya Marekani imetangaza kuwa imewaweka viongozi 3 wa kikundi cha Boko haramu
cha Nigeria kwenye list ya most wanted people in the world...watawasaka kwa udi na uvumba mpaka wawashike no
matter wakiwa hai au wamekufa lakini wanawahitaji tu. - Sasa maswali yangu ni

1.Kwanini ni Boko haramu tu? mbona hawakutangaza hivi kwa Al-shabaab ya somalia while wote ni magaidi?
2.Je ikatokea wamefanikisha kuwakamata na kuwauwa au kuwafunga maisha, Je Nigeria itakalika salama? au
ndiyo itakuwa mwanzo wa vifo vingine kutoka kwa Boko haramu?.
3.Je ni kweli Boko haramu ni watetezi wa dini ya kiislamu huko Nigeria au ni kikundi cha wahuni tu?

Kwa wale wataalamu wa mambo ya kidiplomasia naombeni mnijuze Saga hili kwa faida yangu na wanaJF wengine.

Shukrani....na nawasilisha

who is boko haram ????? jibu Boko Haram Is PDP & PDP Is Boko Haram- Gen Azazi - Politics - Nairaland

ona hii video http://www.youtube.com/watch?feature=endscreen&v=z7yMRbYFUZE&NR=1

ona hii interview Louis Farrakhan interview with Mike Wallace(1996).3gp - YouTube

 
Nimekusoma mkuu!...Je kwa mtizamo wako unaona Boko haramu ni watetezi wa Uislam au ni kikundi cha wauni tu?

Jibu la hilo swali linategemea uko upande gani. Kwa asiye muislam, ni wazi kabisa kwa akili ya kawaida kuwa kufanya ugaidi kwa kisingizio cha kuisafisha dini yao na ukafiri ni upuuzi na hakiupi uislam heshima mbele ya ulimwengu.

Lakini ukiwa muislam ni stori nyingine. Kuna baadhi wanaona Boko Haram, au al qaeda, au taleban, ni wakombozi, mashujaa, watu wenye ujasiri wa kusimama dhidi ya ukafiri wa kikristo na kimagharibi. Ukipita pita kwenye mitaa ya hata hapa kwetu yenye waislam wengi, mfano Zanzibar, ni kawaida kuona vijana wakiwa wamevaa t-shirt zenye picha ya Osama bin Laden kama ishara ya kumuenzi. Gaidi anaenziwa.

Kwa hiyo usiwasemee waislam au dini ya kiislam. Waislam walio wengi ni watu wa kawaida, kama sisi, kama wewe, wanawaza mkate wao wa siku kama watu wengine, wanawaza kusomesha watoto wao kama watu wengine. Lakini baadhi yao si watu wa kawaida, hawa wanawaza siku uislam utakapokuwa majority ulimwenguni, siku sharia itakapotawala, na hawa wapo tayari kufanya lolote ikiwemo kulipua vijana wao ili kutekeleza maluweluwe yao vichwani.
 
Unauliza kama ni Boko Haram peke yake? Mbona muda mrefu Marekani imekuwa inawasaka Al Shabab kule Somalia kwa kutumia drones? Unakumbuka yule Mkomoro aliyekuwa Al Qaida aliyetafutwa kwa muda mrefu? Mbona alitunguliwa na kamzinga ka drone huko Somalia? Hawa magaidi kila wanakochipuka ni kuwatungua tu kwa sababu wakiachiwa washamiri wanatoa fursa kwa Al Qaida kujiimarisha.


Minister Farrakhan Knows Who Killed JFK - YouTube
 
Boko haram sio watetezi wa waislam,bali ni majambazi na magaidi kama walivyo uamsho na sasa ni bora watafutwe na wapigwe risasi na washukuru marekani kwani wao hawasubiri mabomu yawalipukie watu bali mabomu yao huwalipukia magaidi.

Kwakweli vitendo vinavyo fanya na haya makundi ni kutaka kuitawala dunia kwa kisingizio cha uislam.

Siku si nyingi kikundi cha kigaidi cha uamsho kitatangazwa kuwa kikundi hatari na maghala ya silaha yatafunguliwa kukiangamiza.

Nashangaa hii serikali yetu ina subiri nini kukiangamiza hichi kikundi kabla hakijasambaa.
 
Jibu la hilo swali linategemea uko upande gani. Kwa asiye muislam, ni wazi kabisa kwa akili ya kawaida kuwa kufanya ugaidi kwa kisingizio cha kuisafisha dini yao na ukafiri ni upuuzi na hakiupi uislam heshima mbele ya ulimwengu.

Lakini ukiwa muislam ni stori nyingine. Kuna baadhi wanaona Boko Haram, au al qaeda, au taleban, ni wakombozi, mashujaa, watu wenye ujasiri wa kusimama dhidi ya ukafiri wa kikristo na kimagharibi. Ukipita pita kwenye mitaa ya hata hapa kwetu yenye waislam wengi, mfano Zanzibar, ni kawaida kuona vijana wakiwa wamevaa t-shirt zenye picha ya Osama bin Laden kama ishara ya kumuenzi. Gaidi anaenziwa.

Kwa hiyo usiwasemee waislam au dini ya kiislam. Waislam walio wengi ni watu wa kawaida, kama sisi, kama wewe, wanawaza mkate wao wa siku kama watu wengine, wanawaza kusomesha watoto wao kama watu wengine. Lakini baadhi yao si watu wa kawaida, hawa wanawaza siku uislam utakapokuwa majority ulimwenguni, siku sharia itakapotawala, na hawa wapo tayari kufanya lolote ikiwemo kulipua vijana wao ili kutekeleza maluweluwe yao vichwani.

Cha muhimu zaidi kuliko yote ni kuwa muuaji yeyote yule ni lazima asakwe na aangamizwe, iwe anafanya mauaji hayo huku ameshika biblia, msahafu, tasbihi au rozari, huyu ni mhalifu na hana nafasi katika ulimwengu wa kistaarabu. Hawa wasakwe na wamalizwe hata kama watatumia majina ya namna gani. Kama ni Al Shabab, Uamsho, Boko Haram, Talebani, Al Qaeda, Lords Resistance Army au Tamir Taigars, hiyo haijalishi, cha muhimu ni je, wanafanya nini? Kama wanafanya maovu malipo yao ni dhahiri, ni lazima waadhibiwe bila huruma. Tena katika hilo hakuna kuwa na haja ya kuwa na woga wa kuwa watalipiza kisasi. jamii ya Ulimwengu wa Kistaarabu haiwezi kupoteza muda wa kutofanya tendo la kuwadhibi kwa hofu ya kushambuliwa na watu hawa. Wanaweza kuvizia na kuwaua wachache wetu lakini mwisho wa yote ulimwengu wa Ustaarabu utashinda.
 
Back
Top Bottom