Ni Sahihi Kuapa kwa Kutumia Vitabu vya Dini Kwamba Utalinda Katiba ya Jamhuri?

kibavu

Senior Member
Oct 15, 2008
136
82
Umekua ni utaratibu kwa viongozi mbalimbali wa kuteuliwa na kuchaguliwa kuapishwa kwa kushika vitabu vya dini/madhebu yao na kuapa kwamba watailinda katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Lakini watu hao hao wakifanya makosa na kukiuka kiapo chao hushitakiwa kwa mujibu wa sheria zilizotungwa kulingana na katiba ya Jamhuri. Hoja yangu ni kwamba kuna haja gani ya kuapa kwa kutumia vitabu vya dini, na watu wanapokosa wanashitakiwa kwa kutumia sheria za jamhuri? Na je ni kwa nini wasiape kwa kutumia katiba ambayo wanaahidi kuilinda? Najua kuna watu wanaapa kwa kutumia katiba, Kwa nini isingekua hivyo kwa wote kwakua wote wanatumikia katiba ya Jamhuri na si madhehebu/dini zao?

Nawasilisha.
 
Mara zote watu huapa kwa kitu kilicho juu yao ili waonekane kuwa wanamaanisha wanachosema.
Watu wote wanajua ndani ya mioyo yao kuwa Mungu ni mkuu kuliko wao, na sio katiba. Katiba zinatungwa na zinaondolewa. Katiba sio kitu kilicho juu ya mwanadamu, ni Mungu pekee.

Wanaposema tofauti na ukweli wanajivunia dhambi na mshahara wa hizo dhambi ni mauti, wasipotubu.
 
Umekua ni utaratibu kwa viongozi mbalimbali wa kuteuliwa na kuchaguliwa kuapishwa kwa kushika vitabu vya dini/madhebu yao na kuapa kwamba watailinda katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Lakini watu hao hao wakifanya makosa na kukiuka kiapo chao hushitakiwa kwa mujibu wa sheria zilizotungwa kulingana na katiba ya Jamhuri. Hoja yangu ni kwamba kuna haja gani ya kuapa kwa kutumia vitabu vya dini, na watu wanapokosa wanashitakiwa kwa kutumia sheria za jamhuri? Na je ni kwa nini wasiape kwa kutumia katiba ambayo wanaahidi kuilinda? Najua kuna watu wanaapa kwa kutumia katiba, Kwa nini isingekua hivyo kwa wote kwakua wote wanatumikia katiba ya Jamhuri na si madhehebu/dini zao?

Nawasilisha.

Mkuu hii hoja ni nzito. Serikali haijui dini lakini viongozi wake wanatumia vitabu vya dini wakati wanaapa kuitumikia serikali!! Hoja inahitaji tafakuri jadidi.
 
Back
Top Bottom