Ni sahihi bunge la Tanzania kupewa msaada?

Injinia

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
849
26
Ndugu zangu,

Nimeona kule kwa Michuzi kwamba eti Bunge la Tanzania limepewa msaada wa kompyuta, tena zenye thamani ya TShs Milioni 20 tu, toka kwa ubalozi wa Korea ya kusini!!

==============
Korea Kusini yalipatia msaada wa Komputa Bunge

IMG_8427.JPG


Juu na chini: Katibu wa Bunge Dk. Thomas Kashililah akipokea msaada wa Komputa 18 zenye thamani ya zaidi ya million 20 toka kwa Balozi wa Korea Kusini nchini Mhe. Young – Hoon Kim. Komputa hizo zimetolewa na Ubolozi huo nchini kusaidia matumizi mbalimbali kwa waheshimiwa na watumishi wa Ofisi ya Bunge. Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge
IMG_8407.JPG

IMG_8422.JPG


Balozi wa Korea Kusini nchini Mhe. Young – Hoon Kim akimweleza katibu wa Bunge Dk. Thomas Kashililah namna nchi hiyo inavyokusudia kusaidia Bunge la Tanzania katika maswala ya Teknolojia ya mawasiliano mara baada ya kukabidhi msaada wa Komputa 18 zenye thamani ya zaidi ya million 20 katika Ofisi ndogo ya Bunge Dar es salaam jana. Waliosimama toka kulia ni Mkurugenzi wa Mipango na ICT wa Bunge ndg. Siegfied Kuwite na Msaidi wa Katibu wa Bunge Emanuel Mpanda. Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge


========================

Hili jambo limenichekesha pamoja na kunishtua.
1. Hivi kama hadi BUNGE la nchi linapokea msaada, hii nchi inaelekea wapi?
2. Je, ni kweli Bunge kama mhimili mkuu wa serikali, halina uwezo wa kununua kompyuta zake lenyewe?
3. Hizo kompyuta zimepitiwa na wataalamu kuangalia uwezekano wa kuwepo kwa virusi na vifaa/programu za kiuchunguzi (yaani, spying)?

Yaani nimekosa raha kabisa kwa hili jambo. Tunaingiliwa hadi jikoni, tena tunafungua mlango wenyewe!
 
Wabunge na bunge lao wanafikiria kujiongezea mishahara tu lakini vitendea kazi hawafikirii kununua. Hili tatizo la kutojali vitendea kazi/miundo mbinu ni kila ofisi ya umma, wakubwa wanafikiria tumbo kwanza.
 
Hivi kati ya taasisi/ watu wanaohitaji misada Tanzania bunge letu lipo? Kuna shule ngapi zinahitaji hizi computer ? Huu ni msaada au kuna virusi kwenye comuter humo kama alivyosema mkuu hapo juu?

Kwa sababu za kiusalama mi naona bunge izitoe hizi computer wilayani kwenye mashule. Huwezi kutumia computer ya msaada kwa shughuli za bunge. Hata kama haiko networked.
 
Sisi si always tunafurahia kusaidiwa!!!
Kila siku tunaimba imba tu tu masikini!!!
 
Wakuu zangu hivi hili tatizo hatukuliona hadi misaada umetolewa?..
Haiwezekani kwamba sisi wenyewe ndio wavivu wa kufikiria hadi litokee janga ndipo tunatafuta nchawi?..iweje Bunge letu miaka yoote hii limekuwa halina vitendea kazi kama Komputa na tushindwe kuelewa mapungufu haya...Kuna kitu hapa sikielewi!
 
Wakuu zangu hivi hili tatizo hatukuliona hadi misaada umetolewa?..
Haiwezekani kwamba sisi wenyewe ndio wavivu wa kufikiria hadi litokee janga ndipo tunatafuta nchawi?..iweje Bunge letu miaka yoote hii limekuwa halina vitendea kazi kama Komputa na tushindwe kuelewa mapungufu haya...Kuna kitu hapa sikielewi!

Hivi tunajuaje kama misaada hii iliombwa? Inawezekana kabisa Wakorea wamependa wenyewe kutoa msaada, na hawakujua pa kuanzia kutoa wapi, wakaongea na bunge bunge likasema zilete hapa.

Ninachoona hakifai hapa (ukiachilia mbali swala la kwamba tulitakiwa tusisaidiwe in the first place), ni kwamba hata ukiondolea mbali sababu za kiusalama zilizotajwa hapo juu, ni ukweli kwamba bunge letu halihitaji msaada huu, na mtu kukubali msaada usiohitaji ni kashfa, hususan kama kuna watu wanaohitaji msaada huo kikweli. Bunge linataka kufanya ukarafati wa mamilioni ya dola. Marupurupu ya nyumba ya spika kwa mwezi mmoja tu yanafika karibu nusu ya thamani ya msaada wote, hapo sijaongelea mamia ya wabunge, kwa hiyo si haki bunge kuchukua msaada huu, hususan kwa sababu kuna shule kibao zinasota bila hata vitabu sembuse computer.

Sasa hapa tunakuja kuibua maswala mengine, ya ulafi, umimi, kutokuwa na kiasi, kutojali wengine, kutoangalia matumizi mazuri ya resources/ misaada etc.

Mimi ningekuwa afisa wa bunge ninayehusika na kuukubali msaada huu ningewaunganisha wakorea na shule inayohitaji msaada huu.Bunge letu lina uwezo wa kununua computers za $ 20,000.

Ulafi huu ni aibu.
 
Hii kitu imenishangaza sana. Hivi tutaondokana vipi na wazo la kuomba na kupokea misaada? Hii ni sawa na mtu kukujia nyumbani kwako kukupatia msaada wa chakula cha familia yako, sijui kama baba/mama utajisikiaje, wakati hapo kwako hakuna njaa. Kama lengo la Korea kweli ni kutoa misaada ilikuwa ni lazima wao watoe kwa Bunge? Bunge linaendeshwa kwa bajeti ya kila mwaka, hawakuwahi kuwa na bajeti ya kununua kompyuta. Huku ni kujizalilisha kwa hali ya juu.
 
Kiranga,
Mkuu nakukubali sana tu ila yanishangaza sana kuona Upinzani wasifikirie vitu kama hivi mapema wakati wa bajeti kiasi kwamba najiuliza kuna utaratibu gani wa bunge kutunza hansard pamoja na uwezekano wa wabunge wenyewe kuzipitia mara kwa mara. Hili la kusaidiwa linaonyesha uvivu wa Taifa zima na wala sii aibu tu kwa Bunge isipokuwa nchi nzima..
Inaudhi sana kuona mambo kama haya yakitokea kiholela tena yakipewa sifa na kupambwa magazetini utafikiri sisi ni maskini wa hivyo. Aaaaah nchi yetu hii jamani ama kweli umaskini hauna elimu.
 
Kiranga,
Mkuu nakukubali sana tu ila yanishangaza sana kuona Upinzani wasifikirie vitu kama hivi mapema wakati wa bajeti kiasi kwamba najiuliza kuna utaratibu gani wa bunge kutunza hansard pamoja na uwezekano wa wabunge wenyewe kuzipitia mara kwa mara. Hili la kusaidiwa linaonyesha uvivu wa Taifa zima na wala sii aibu tu kwa Bunge isipokuwa nchi nzima..
Inaudhi sana kuona mambo kama haya yakitokea kiholela tena yakipewa sifa na kupambwa magazetini utafikiri sisi ni maskini wa hivyo. Aaaaah nchi yetu hii jamani ama kweli umaskini hauna elimu.

Bob,

Unlike you ambaye unafikiri kwamba bungeni kuna upungufu wa computer, mimi siamini hilo (first off hata watumiaji hamna).Ndiyo maana napigia kelele kwa nini bunge linakubali msaada lisilohitaji?

Hata kama kuna uhitaji kweli wa computer za $ 20,000 bunge letu halishindwi kupitisha ki exception cha kupata hizo fedha. They are getting ready to do a multimillion dollar extension, watashindwa $ 20,000 wakati wanatoa karibu nusu ya hizo kila mwaka kwa posho ya nyumba ya Spika? Kwa hiyo mimi sikubali kwamba bunge lina hitaji hili.

Na ingawa naamini kwamba Tanzania tunatakiwa tusiwe ombaomba, lakini naamini pia kwamba hili ni swala linalotaka mkakati wa long term, na in the short term tutakubali msaada mpaka tutakapoweza kusimama wenyewe.Tatizo kwa nini msaada uende kwenye sehemu isiyohitaji msaada wakati tuna shule kibao na sehemu nyingine ambazo hazina budgets za ku afford computers hizi?
 
Kiranga,
Mkuu nakupata lakini hata kama huko Bungeni zipo na wana uwezo wa kununua,maadam imesemakana zimetolewa na Ubolozi huo nchini kusaidia matumizi mbalimbali kwa waheshimiwa na watumishi wa Ofisi ya Bunge. Hapa ndipo penye herufi kubwa!..

Haya mazoea ya kuomba na kupokea misaada ni hulka yetu. Umaskini hauna elimu hata kidogo na mara nyingi pride pia inaua. hivyo kama ulivyosema tunahitaji misaada lakini iwe muhimu ktk mapambano yetu.

Hakika mimi sikubaliani kabisa na misaada yoyote nje ya miundombinu. Ndicho alichofanya mwalimu wakati wake hakupokea misaada ya kipuuzi pamoja na kwamba hawa wasomi wa siku hizi wanambeza..

Pia nakumbuka rais wa Malaysia aliwahi kusema inafika wakati mtu alovunjika mguu kuacha kutembea na magongo (msaada) pindi anapopata nafuu ili kujipa imani ya kutembea tena...lakini sisi Tanzania tumekuwa ktk magongo toka niijue nchi hii..Sawa na ombaomba mmoja nilimkuta pale mtaa ya Jamhuri namkumbuka toka mwaka 1984, kisha kuwa ombaomba mzoefu.

Ifikie wakati Upinzani waulize sheria za kupokea misaada kama hii inaidhinishwa na nani? maanake iswetu ili mradi nchi fulani imejisikia kutoa msaada basi unapokelewa pasipo utaratibu maalum kwani hawa watu wanakuja na mengi sana. Misaada mingine inakuja kama hongo la kupata tender au yawezekana kuwa hatari kwa Usalama wa nchi yetu...
 
Mimi na *HATE* hii kitu inayoitwa misaada wazazi wangu
waliimba sana huu msemo wakati nipo mdogo "cha mtu
mavi ukikiona kiteme mate"
. Huwa nachukia sana tabia ya
kuomba omba nipo radhi nikae na njaa kuliko kuomba
(I know I'm very hardcore). Tupak once said "I'd rather be
dead than be a punk nigga"

Sijui misaada sijui nini... yaani kweli tunashindwa kuzalisha
wenyewe? kweli? Nchi (bunge) inapokea msaada wa $20,000
kweli hii inaigia akilini. Halafu hawa jamaa wanaendesha
sijui SUV sijui nini? kwa nini walicho kifanya?

Katika miaka michache niliyoishi hapa duniani sijawahi kuona
kitu free hata wazazi wetu hawakutulea bure. Wali house
genes zao kwetu ndio maana walihakikisha wanatulea until
we're mature enough. It was all for self interest... but I'm not
gonna get too philosophical here. Sasa ndo hawa the so
called wahisani.

Mimi huwa nipo makina sana na mtu ambaye ananipa favor.
Huwa naangalia effect ya hiyo favor katika kila angle hata
kama ni rafiki yangu wa karibu. Wazazi wangu walinifundisha
"binadamu humbwa na uso wa haya" ukipokea sana favor,
siku moja utaona haya na ukiombwa utashindwa kukataa.

Mwanzoni mwa mwaka huu kuna demu alini-offer watoto
wake (bila ya kumuomba) ili niwa file kwenye tax (kwa wale
wa US wanaelewa gemu). kwa kweli ninge vuta zaidi $7000
lakini nikaona hiyo favor siyo bure. Nilijua yakuwa demu ata
ni n'gan'gania sana baadae kwahiyo nikajisemea to hell with
those grands. Sikumjibu! that kind of thinking ndiyo inayo
kosekana Tanzania. Yaani tunakuwa na impulsive decision
kwenye mambo ya national security, inasikitisha sana.

Serikali yetu inatakiwa kukataa hivi vimisaada kwasababu
inakuwa rahisi kwa wahisani kutuingia kirahisi kwasababu
wanakuwa wame tengeneza ka bond fake fulani na sisi.
 
Mimi na *HATE* hii kitu inayoitwa misaada wazazi wangu
waliimba sana huu msemo wakati nipo mdogo "cha mtu
mavi ukikiona kiteme mate"
. Huwa nachukia sana tabia ya
kuomba omba nipo radhi nikae na njaa kuliko kuomba
(I know I'm very hardcore). Tupak once said "I'd rather be
dead than be a punk nigga"

Sijui misaada sijui nini... yaani kweli tunashindwa kuzalisha
wenyewe? kweli? Nchi (bunge) inapokea msaada wa $20,000
kweli hii inaigia akilini. Halafu hawa jamaa wanaendesha
sijui SUV sijui nini? kwa nini walicho kifanya?

Katika miaka michache niliyoishi hapa duniani sijawahi kuona
kitu free hata wazazi wetu hawakutulea bure. Wali house
genes zao kwetu ndio maana walihakikisha wanatulea until
we're mature enough. It was all for self interest... but I'm not
gonna get too philosophical here. Sasa ndo hawa the so
called wahisani.

Mimi huwa nipo makina sana na mtu ambaye ananipa favor.
Huwa naangalia effect ya hiyo favor katika kila angle hata
kama ni rafiki yangu wa karibu. Wazazi wangu walinifundisha
"binadamu humbwa na uso wa haya" ukipokea sana favor,
siku moja utaona haya na ukiombwa utashindwa kukataa.

Mwanzoni mwa mwaka huu kuna demu alini-offer watoto
wake (bila ya kumuomba) ili niwa file kwenye tax (kwa wale
wa US wanaelewa gemu). kwa kweli ninge vuta zaidi $7000
lakini nikaona hiyo favor siyo bure. Nilijua yakuwa demu ata
ni n'gan'gania sana baadae kwahiyo nikajisemea to hell with
those grands. Sikumjibu! that kind of thinking ndiyo inayo
kosekana Tanzania. Yaani tunakuwa na impulsive decision
kwenye mambo ya national security, inasikitisha sana.

Serikali yetu inatakiwa kukataa hivi vimisaada kwasababu
inakuwa rahisi kwa wahisani kutuingia kirahisi kwasababu
wanakuwa wame tengeneza ka bond fake fulani na sisi.

Nilisikia mtu ameripoti hapa kuwa Makamba anawamabi watu kwao huko Bumbuli wamchague mwanae ama sivyo eti hawatapata misaada! Gonjwa hatari sana hilo linaloitwa misaada
 
hakuna msaada wa bura naweza shawishika kuwa huenda jamaa wamezitumia hizo computa kwa muda wakaona waje kuzitupa kama kipindi fulani tulipopigia makofi msaada mmoja wa computa kwenda chuo fulani lkn baada ya mwaka mmoja computa zote zimekufa misaada nachukia hili neno na sipendi kulisikia
 
Balozi wa Korea Kusini nchini Mhe. Young – Hoon Kim akimweleza katibu wa Bunge Dk. Thomas Kashililah namna nchi hiyo inavyokusudia kusaidia Bunge la Tanzania katika maswala ya Teknolojia ya mawasiliano mara baada ya kukabidhi msaada wa Komputa 18 zenye thamani ya zaidi ya million 20 katika Ofisi ndogo ya Bunge Dar es salaam jana. Waliosimama toka kulia ni Mkurugenzi wa Mipango na ICT wa Bunge ndg. Siegfied Kuwite na Msaidi wa Katibu wa Bunge Emanuel Mpanda. Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge[/FONT]


Hebu connect the dots....hapo kwenye red amesema ...Korea wanakusudia kulisaidia Bunge katika..... nadhani Korea wapo kibiashara zaidi (which is correct) wanajua Bunge linataka kufanya upgrade soon na biashara ipo hapo, thats it!
 
Back
Top Bottom