Ni rekodi gani iliyompandisha chati Kikwete kiasi kile mwaka 2005?

Wewe unavyoona kuna mwelekeo wa maisha bora chini ya JK? Kama sivyo ni vema tukajiuliza ni nini kilichotuloga kumpa "kula" za kishindo mwaka 2005 ili tusije kufanya kosa kama hilo wakati mwingine! Mimi nionavyo JK alivinunua vyombo vya habari na kuweka mtandao mzito wa kumnadi! Tunaona hadi kufikia uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 vyombo vya habari vilimgeuka na mtandao ulisambaratika na kubakia yeye (JK) na familia yake tu, yaani BMW - Baba, Mama na Watoto!

Simple ni mapenzi na imani juu yake ndio iliyomfanya apate ushindi wa kishindo! wakati ule watu walikuwa na imani na JK kama walivyokuwa na imani na Dr Slaa leo hii. Kufeli kwa slogan ya maisha bora na sera kama za elimu na kilimo kwanza ni changamoto as yeye sio mtendaji wala mtunga sera wanaomwangusha ni watu wake kwahiyo labda tuone amewajibikaje kuhusu watu wake kufanya sera zishindwe kufanya kazi. Lakini pia haiwi basi kwa kumkejeli na kumdhihaki yeye ana ndugu ana watoto wanajisikia vibaya mnavyomdhalilisha hivi wewe mjomba wako au baba yako akidhalilishwa utafurahia? pia JK kama alivyo Lipumba, Mbowe, Dr Slaa, Cheyo na kina Mnyika na JK pia ana watu wanaompenda ikiwa leo wanaCDM wanaona uchungu kukejeliwa kwa viongozi wao basi mjue kuna watu wenye mapenzi na JK wanaumia kama nyie mlivyo na mapenzi na kina Lipumba na Dr Slaa na mnaumia mkitukaniwa viongozi wenu.

Napenda kumalizia kwa kusema jambo usliopenda wewe au mtu wako afanyie basi ni busara usimfanyie mwenzio. Lugha zinazotumika kuuliza haya maswali sizo. Tunayo nafasi ya kujirekebisha.

Kuambiana kupo kusikilizana hakupo!!!!
 
Naungana na wewe. Historia inatufundisha nini tulikosea ili uchaguzi mwingine ukifika tusifanye makosa tena. Hatuwezi kupanga mikakati kama hatujatambua wapi tulikosea. Kwa mfano, watanzania wengi sasa wamebaini kwamba vyombo vya habari vingi vilinunuliwa ili kumpamba mtu ambaye hakuwa na hata chembe ya sifa ya kuwa rais wa nchi. In fact, inasemekana hata Mzee Madiba (Nelson Mandela) alishangaa aliposikia kwamba Dr. Salim A. Salim amedondoshwa na chama chake kwenye kinyang'anyiro cha urais. Inasemekana alishangaa na kuishia kusema kwamba kama Dr. Salim ameshindwa, basi Tanzania ina hazina kubwa ya viongozi!!!

Kwenye blue naomba unipe sifa za mtu anaeweza kugombea urais na hatimae kuwa Rais. Na kwenye hiyo RED inaonyesha ni jinsi gani Mzee Mandela ana busara hakutumia maneno ya kejeli kama wengi wetu tunavyofanya hapa.
 
Well, kwa jinsi ninavyofahamu nadhani mwaka 2005 Kikwete alikuwa na sifa zote zinazotakiwa kwa Rais. Binafsi ilinichukua muda kumkubali Kikwete hasa baada ya Generali Tumainieli Kiwelu kutamka hadharani kuwa hafai. Mimi nina mwamini sana Generali Kiwelu na maneno yake yaliniingia vizuri kwani nilikuwa kama yeye. Baadae nilikubali kuwa anazo sifa.

Kikwete wa 2005 siyo kikwete wa leo. Amechakachuliwa sana. Amekuwa dhaifu sana. Kanali wa Jeshi apaswi kwa namna yeyote ile kuwa laini kiasi hiki. Mfumo wa kiutendaji ndio uliomfanya Kikwete awe alivyo lakini si jinsi wala taratibu yake kwa mwaka 2005. Tafadhali rejea aliyofanya wizara yz fedha n.k ..... alianzisha mifumo mizuri sana huko.
 
Jambo moja watanzania hatujataka kulikubali ni Rais JK ana kipaji cha ku-network.
Hiki ni kitu hatuwezi kumwondolea, anapendwa hata na watoto wasiojua siasa. Kawafanyia nini wampende, hakuna awezaye kujibu.

Kama kiongozi ana mapungufu ambayo wengi mmesha yajadili. Kama angeweza kutumia kipawa hicho kuwafanya wasaidizi wake watende yaloyo sahihi leo hii Tanzania tungekuwa mbele ya nchi zote za mashariki mwa afrika katika kila kitu.

Kwa kifupi majibu yoyote utakayopata hapa kwa kuonyeshwa rekodi, I guarantee you, hayatakuwa na uhusiano wa kwa nini tulimchagua 2005.
 
katika maisha hakuna makosa najutia kama haya. nilimpigania sana mrema nikadhani ni mkombozi kumbe da, nikampigania JK nikadhani ataleta mapinduzi ya kweli nikaliwa. Mwaka 2010 nilipoteza kadi sikuchukua nyingine maana sikuona wa kuchagua. alikuja kujitokeza dr slaa too late. wapo wengi kama mimi ambao hawakujitayarisha kupiga kura kwa kupoteza matumaini. ndio maana nawaasa chadema muongeze umakini watu wakikata tamaa na nyie pia nchi hii itakuwa chini ya ccm kwa miaka 50 ijayo. nyie ndio tegemeo pekee. ji
http://www.google.com
 
Kipindi cha Mrema umri haukuniruhusu kupiga kura. Jk sijawahi kumpa kura. Chadema wakaze buti, matumaini ya waTZ wengi yapo kwao.
 
Ili utawala CCM uwe historia, tunahitaji katiba mpya ambayo itafafanua kizungumkuti cha tume ya uchaguzi. Tunahitaji Tume Huru ya uchaguzi ili CDM tusiendelee kuporwa haki zetu.
 
katika maisha hakuna makosa najutia kama haya. nilimpigania sana mrema nikadhani ni mkombozi kumbe da, nikampigania JK nikadhani ataleta mapinduzi ya kweli nikaliwa. Mwaka 2010 nilipoteza kadi sikuchukua nyingine maana sikuona wa kuchagua. alikuja kujitokeza dr slaa too late. wapo wengi kama mimi ambao hawakujitayarisha kupiga kura kwa kupoteza matumaini. ndio maana nawaasa chadema muongeze umakini watu wakikata tamaa na nyie pia nchi hii itakuwa chini ya ccm kwa miaka 50 ijayo. nyie ndio tegemeo pekee. ji
Google

Umakini wa CHADEMA hautakuwa na msaada iwapo watu wa aina yako wamejaa Tanzania: wenye historia ya kufanya kufanya makosa katika chaguzi mbali mbali kama ulivyoeleza makosa uliyofanya mwaka 1995 na kuyarudia mwaka 2005; makosa ya kutotunza kadi ya kupigia kura na kuipoteza; makosa ya kuwatupia lawama CHADEMA wawe makini zaidi ili hali wapiga kura wa aina yako hamko makini hata kutunza kadi tu!
 
Binafsi sikumpigia kura Kikwete mwaka 2005, hata hivyo tafadhalini naomba mwenye kumbu kumbu anijuze ni sifa zipi alizokuwa nazo Kikwete hadi kuchaguliwa kuwa Raisi wa Tanzania. Sambamba na hilo pia ningependa kufahamu ni sifa zipi zilizopelekea kuongezewa kipindi kingine cha miaka mitano mwaka 2010.

Kwa mbali nakumbuka 2005 kuna watu walikufuru kwa kudai kuwa Kikwete alikuwa chaguo la Mungu na wapo waliodai kuwa ni tumaini lililorejea. Sasa leo naomba hawa kama wapo wanijuze tu misingi ya hayo madai yao na walivyoyafikia mpaka kuamini kuwa Tanzania imempata mkombozi wa kweli, Jakaya Mrisho Kikwete.

Cha ajabu ni kwamba katika kipindi kisichozidi mwaka moja baada ya kuchaguliwa, wananchi walianza kushuhudia dalili za utawala lege lege usio makini na madudu kibao. Hata hivyo lawama hazikuweza kuelekezwa moja kwa moja kwa Kikwete, kiongozi wa serikali na Mwenyekiti wa chama tawala, bali kwa wasaidizi wake.

Hali iliendelea hivyo mpaka Uchaguzi wa mwaka 2010 ambapo, pamoja na mapungufu ya wazi ya kiuongozi, ilidaiwa wananchi walimrejesha tena Kikwete madarakani. Hivi leo pamoja na kashfa lukuki na hali ya wananchi ikizidi kudorora, bado lawama hazielekezwi moja kwa moja kwa Kikwete bali wachawi wa kufikirika !

Matokeo yake ni kuwa waliodai Kikwete ni chaguo la Mungu na waliodai ni tumaini lililorejea hivi sasa wamezuka na dai jipya kuwa wanaomkosoa Kikwete hawaitakii mema Tanzania. Badala yake wengi wao wanawanyooshea vidole wapinzani, hasa Chadema, wakidai nia yao si kutetea maslahi ya taifa bali kuchochea vurugu.

Wanadai Chadema kwa kuwaelimisha wananchi, wanabaka demokrasia kwani uchaguzi ulipita na kiongozi kupatikana kwa njia ya kura. Watawala kwa upande wao wanakiri mapungufu kiasi cha kulazimika kuvua magamba huku wakisahau kwamba hata inapobidi nyoka kuvua magamba anabakia nyoka tu.

Kwa wanaomtetea Kikwete kama Raisi, nawapa pole kwani ni kama kumtetea dereva aliyelewa, hana habari na anakotoka wala anakoelekea huku abiria wanashangilia. Si vigumu kutabiri safari itaishaje kama hatua hazikuchukuliwa za haraka za kumwondoa usukani na kumkabidhi gari dereva makini.

Kwa wanaoitetea CCM kama chama tawala na nyie nawapa pole kwani ni kama kitanda kilichojaa kunguni, chawa na mende - mnaishi kwa kunyonya damu ya Watanzania. Dawa yenu ni maji ya moto na tayari yako jikoni yanachemka yakizidi kuchochewa na Chadema na muda si mrefu mtaonja mchungu yake.
Kuwatambua ni rahisi kwani miili yenu imejaa upele !
 
kwani JK mwaka 2010 alishinda?

binafsi nina uhakika (kwa ushahidi wa kimazingira) hakushinda!
 
Mwaka 2005:
Sifa kubwa aliyokuwa nayo Kikwete ni kuhonga fedha. Walitumia fedha nyingi sana kuhonga vyombo vya habari, Viongozi wa dini, Wakuu wa vyombo vya usalama, Wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM na watu wote wenye ushawishi ili wawadanganye wananchi.
Mwaka 2010:
Kipindi hiki mbinu zake chafu zizilishagundulika hivyo ikabidi atumie nguvu ....kuchakachua matokeo.
 
Mwaka 2005:
Sifa kubwa aliyokuwa nayo Kikwete ni kuhonga fedha. Walitumia fedha nyingi sana kuhonga vyombo vya habari, Viongozi wa dini, Wakuu wa vyombo vya usalama, Wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM na watu wote wenye ushawishi ili wawadanganye wananchi.
Mwaka 2010:
Kipindi hiki mbinu zake chafu zizilishagundulika hivyo ikabidi atumie nguvu ....kuchakachua matokeo.

Asante macho_mdiliko, mpaka sasa sifa zilizomwingiza madarakani ulizozitaja ni hizi;

  1. Wizi
  2. Hongo
  3. Udanganyifu
Tunaendelea .............................
 
Kumwandalia Mtoto wa Mwinyi njia ili na yeye awe RAIS.

Siyo siri kuwa Mwinyi ndiye ALIMBEBA Kikwete na kumuweka hapo maana huko kwenye makamati ya juu ya CCM, jamaa kwa sasa ana nguvu sana na baada ya kufa Kawawa, ni kama kabaki peke yake.

Dawa ni kuhakikisha Mtoto wa Mwinyi anapigwa chini kwa kila hali ili kumkomoa huyu Mzee.

Halafu Wazenji wanakuja na kusema SISI tunawatawala wakati ukweli anayetawala kwa sasa Tanzania ni Mwinyi ambaye ni Mzenji.
 
Hakuwa na sifa hata moja! Kilichotokea ni ku'take' advantage ya uelewa mdogo wa wananchi na kibaya kuliko vyote ni kura za huruma alizopewa kutoka kwa wananchi/akina mama kutokana na sura yake na imani kwamba ni yeye alistahili zaidi ya Mkapa baada ya kupata kura nyingi kwenye raundi ya kwanza huko NEC-CCM! Ndio maana hadi leo yupo bize kutafuta huruma za wananchi kwa kauli mbiu kibao ikiwemo ile ya "rais hana tatizo, wasaidizi wake ndio wanamshauri/ wanamwangusha vibaya!
 
Hakuwa na sifa hata moja! Kilichotokea ni ku'take' advantage ya uelewa mdogo wa wananchi na kibaya kuliko vyote ni kura za huruma alizopewa kutoka kwa wananchi/akina mama kutokana na sura yake na imani kwamba ni yeye alistahili zaidi ya Mkapa baada ya kupata kura nyingi kwenye raundi ya kwanza huko NEC-CCM! Ndio maana hadi leo yupo bize kutafuta huruma za wananchi kwa kauli mbiu kibao ikiwemo ile ya "rais hana tatizo, wasaidizi wake ndio wanamshauri/ wanamwangusha vibaya!
Asante Filipo, sifa zimefika saba;

  1. Wizi
  2. Hongo
  3. Udanganyifu
  4. Uzuri wa sura
  5. Huruma
  6. Mwinyi
  7. Uelewa mdogo wa wananchi
Tunaendelea.............
 
Mmesahau? Walisema jamaa alikua handsome jaman, Ubongo wake ni madudu tupu!
 
Mathalani tuseme JK halifanyi kitu chochote Taifa miaka ya nyuma lakini yeye sasa hivi sio Mwenyekiti wa chama tu bali ni Rais wa Tanzania kujua kwako uzalendo na aliyoyafanyia Tanzania kabla ya kuwa Rais hakuathiri kitu chochote kwenye madaraka aliyopewa na Katiba. Pili Hoja yako imekaa kihuni na ukosefu wa adabu kwa kiongozi wa nchi, nasema kiongozi wa nchi kwa kuwa Katiba ndio inamtambua na sote tumeambiwa tuwa heshimu viongozi (mamlaka) kwenye vitabu vya dini. Sikuelewi unapomwita Rais "huyu jamaa" kama kweli unamtendea haki au baadhi yetu humu kumdhihaki na kumwita "kilaza" sisi ni watu wazima inatupasa kuwa na hoja zenye heshima na adabu ili hata wao wakipata fursa ya kusoma basi waone yale tunayoyajadili na kuyafanyia kazi. Hivi ingekuwa wewe ndio JK halafu unaingia JF unakuta unakejeliwa na kudhihakiwa na kupostiwa picha za mwanamke mwenye sura yako will you spend your time kusoma maoni ya members wanaokushambulia kwa kejeli? hebu jiweke kwenye nafasi yake then uone kuwa utaona hawa ni wapuuzi na wenye wivu na wengi wao ni wahuni na ndio maana wanajiita "kingcobra" kwanini hawakujiita majina yao? atapata jibu kwasababu hawataki kutambulika na wengine ni watumishi wa umma!

Kwahiyo mheshimiwa siasa sio kama wewe unavyoifikiria unaweza ukawa hujafanya lolote la maana kabla lakini ukashitukia wewe ni mtu muhimu sana kwa taifa. Naomba nikuulize swali ukilijibu vizuri then mimi na wewe leo kutwa nzima tutajuzana ya maana yaliyofanywa na JK kabla. Je Marehem Dr. Omar Ali Juma alifanya jambo gani la maana la kizalendo kabla ya kuwa Makamu wa Rais? je Dr Mohamed Shein aliemrithi Marehemu Dr Omar alikufanyia nini wewe pamoja na taifa jambo la maana kabla ya kuchukua nafasi ya Dr Omar? Unamkumbuka waziri mkuu mstaafu Mhe Fedrick Tulway Sumaye? aliifanyia nini Tanzania jambo la maana la kukumbukwa kabla hajateuliwa na Mkapa kuwa waziri mkuu? ulikuwa unamjua vipi Sumaye kabla hajawa waziri mkuu?

Ukiwalinganisha hao niliowataja amabao hatukujua hata siku moja na si kuwa sie tu hatukujua kama watashika nyadhifa hizo hata wao hawakuota kama watakuwa na nafasi hizo kwenye siasa. Ni kwamba waliaminiwa kuwa wanaweza wakapewa nafasi kutekeleza azma za kulipeleka taifa mbele na hapo ndipo wakaanza kulitumikia Taifa na kuonekana walichokuwa nacho.

Naomba niishie hapa.

Kaka mbona maneno mengi,ukishakuwa kiongozi wa watu lazima watu wakuseme kwa sab ulipoomba ridhaa yao uliwaahidi,na kugusa hisia zao,wakati ukishindwa kutimiza yale uliyoahidi lazima wakusute,muda wa kubembelezana ulikwisha zamani,zipo njia mbili tu unafaa au haufai,basi
 
Naombeni tukumbushane sababu moja iliyofanya Kikwete kuaminiwa na kupewa ualali wa kuongoza Watanyania 2005.
 
Back
Top Bottom