zumbemkuu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2010
- 10,831
- 8,621
wadau wenzangu hapa JF! nimekuwa najiuliza hi swali sana, kuwa ni nini kitatokea baada ya Zanzibar kuwa huru? nimejiuliza sana hilo swali kwakuwa znz inaunganiswa na visiwa vikubwa vya Unguja na Pemba vyenye histori zinazotofautiana sana kisiasa, ukijumlisha na umbali unaotenganisha visiwa hivyo ndo utagundua kuwa NI HERI MUUNGANO HUU UNAOVUNJIKA KWA KUWA ULIANZA NA TOBO NA HATIMAYE VIRAKA NA MWISHO KUVUNJIKA KABISA KULIKO MPASUKO UTAKAOJITOKEZA WA NCHI HURU MBILI ZA UNGUJA NA PEMBA, HAPO NDO UTABIRI WA NYERERE UTAKAPOONEKANA WA MZANZIBARI NA MZANZIBARA.. hayo ni mawazo yangu tu wajameni, msinitoe roho nkashindwa kwenda taifa leo kushuhudia mnyama akirarua mtu.