Superman
JF-Expert Member
- Mar 31, 2007
- 5,695
- 1,696
Ni nini hasa Mwanamke anahitaji kutoka kwa Mwanamume na katika Maisha yake?
Assume:
1. Ni binti Mrembo wa asili wazazi wako ni watu makini, waelewa, wasomi na wanaoheshimika sana katika jamii na wamekulea vema, ukapata mume makini anayejiheshimu na mwenye upendo wa kweli akakuoa - Hutaki kutulia macho juu juu, memeo akagundua nyendo zako na kukukanya, ukaomba msamaha akakusamehe maisha yakaendelea.
2. Ulikuwa huna kazi, mumeo akakukabidhi kampuni uiendeshe, ukaifanya kampuni kijiwe cha mashoga zako na mawasiliano na wanaume zako na kisha kutafuna mapato ya kampuni, mumeo akakuondoa kukunusuru wewe na kampuni. Ukakusamehe makosa yako maisha yakaendelea.
3. Mumeo kwa upendo ili usiwe bored akakutafutia kazi nzuri na makini ya kuheshimika, ukaanza kufanya kazi lakini kiwango chako cha utendaji kikawa chini na pia bado unajihusisha na wanaume nje ya ndoa. Mumeo akagundua, kakukanya tena ukaomba msamaha. Mwajiri akaamua kukuondoa kazini kwa kuwa kazi huwezi.
4. Mumeo akaamua kukutafutia mtaji mkubwa ufanye biashara zako, ukatumia bado nafasi hiyo kuendeleza mambo yako na wanaume.
5. Bado mumeo kakununulia gari na unaweza kutumia magari mengine yaliyopo nyumbani, lakini bado huonekani kuridhika.
6. Mumeo huyo, anakuonyesha mapenzi makubwa usiku na mchana, anakutunza, anakupa kila kitu utakacho, anakupa pesa zozote unazohitaji na kukupeleka popote utakapo nakuridhisha kwa mahitaji yako yote ya kimapenzi, kimwili, kihali na kimali lakini bado hutulii wewe na wanaume tu.
7. Elimu yako ilikuwa ya chini akakuendeleza kufikia level ya Chuo Kikuu (Degree), lakini bado wewe na wanaume tu kila kukicha.
8. Mumeo kwa upendo hakutaka mambo yako yajulikane nje hata hivyo mara kadhaa katumia rafiki yake wa familia wa karibu sana kukuonya ili ujirekebishe, kila wakati unaomba msamaha utaacha na kujirekebisha lakini huachi. Anajitahidi kukuchukua mara kwa mara mkapime HIV ili kujinusuru na kukufanya uwe makini lakini somo halieleweki.
9. Mumeo anakuchukua nje ya nchi mahali kwa likizo muwe wawili tu mpate kudumisha mapenzi na kurelax, lakini muda mwingi wewe unautumia kupiga simu kuongea na wanaaume wako na SMS kibao.
10. Hatimaye mume wako anaamua kukufuatilia ajue ni nini shida yako hasa, anagundua miaka yote mliyopo katika ndoa umekuwa na mahusiano na wanaume wengine na kibaya zaidi ni kuwa si moja tu bali ni zaidi ya watatu. Ili kusikia kauli yako kama ni kweli unafanya hayo mambo safari hii anamuhusisha mama yako mzazi ambaye ndoyo tegemeo la mwisho la kwako, unakubali mbele ya mama na mumeo kuwa ni kweli hayo mambo umekuwa ukiyafanya na kutahayari kuonyesha kuchanganyikiwa na sasa mume umeamua "Kujiweka Pembeni, kuepusha msongamano".
Lakini bado hili jambo linaaacha maswali mengi moja wapo ni hili: NI NINI HASA MWANAMKE ANAHITAJI KUTOKA KWA MWANAUME NA KATIKA MAISHA YAKE?