Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Nijuavyo mimi neno "elekezi", maana yake ni inayoonyesha njia. Kwa mantiki hiyo, semina elekezi maana yake nikuwajumuisha watu pamoja kwaajili ya kuwaonyesha njia inayopashwa ifuatwe ili kufanikisha malengo yaliyokusudiwa. Kama tafsiri yangu hiyo ni sahihi, basi hizo semina elekezi ni moja ya majenga ya taifa hili; Nasema hivyo kwasababu katika dunia ya sasa watu wazima kama wabunge, wenye elimu yao, na uzoefu wa miaka mingi katika shughuli mbali mbali, hukutana ili kubadilishana mawazo na uzoefu, na wala siyo kupigwa msasa. Kwani huyo anayewapinga msasa yeye huo ujuzi ambao hauwezi kuhojiwa aliupata wapi!