Texas Tom.
JF-Expert Member
- Jun 8, 2013
- 510
- 273
Hakuna fundi/kipaji/taaluma/chuo cha kutongoza kwa mwanaume, hakuna kujiandaa/kujipanga kwenda kutongoza! kuna blogs nyingi zinafundisha watu maneno ya kwenda kumwambia msichana ili umpate...NI UONGO! labda mtu akuambie maneno ya kuepuka kumwambia msichana. Usione kidume kimesimama muda mrefu na mdada ukafikiri kuna la maana anachosema, mengine ni ujinga tuu!!! utasikia ''NATAKA KUNUNUA GX 100" "NATAKA KUHAMIA KWENYE NYUMBA YANGU" ni kujipamba kiujinga utakuta hata kumi huna. Halafu hakuna mwanaume anaeweza kukuambia ni maneno gani alimwambia binti yule hadi akakubali sana sana atakuambia tu nilipiga saundi nikapiga saundi hadi akaingia line...muulize hiyo saundi ni ipi??? Angalia hata zile bongo muvi ikifika wakati wa kumtokea binti wanashindwa kuongea....ila wakina dada huwa wanatuenjoy wakati tunawatoke!! sasa umkute anaepiga maswali ya papo kwa hapo utakimbia.. mi lishawahi kutema cheche kwa dada mmoja akawa anacheka hana mbavu, nilimwambia (nakusimulia kwasababu hunijui) ''kwenye majani mabichi wanakuja wanyama mbalimbali sasa mi nakuja kama kondoo..." kabla hata sijamaliza akawa hana mbavu.. nikakimbia akawa ananiita ndo nikatokomea kabisa. nilikua form 1 hadi leo ananiita MZEE WA MAJANI MABICHI (kweli nilikua ---- ee)... hebu jiulize na wewe ni maneno gani ulisema ukikumbuka unacheka...au dada ulowahi kuambiwa nawe ukikumbuka unacheka..