majorbuyoya
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 1,828
- 564
Natanguliza heshima kwenu wana JF!. Leo niliamua kuperuzi peruzi gazeti la Raia Mwema kwenye safu ya Maoni/Makala nikakutana na makala yenye kichwa cha habari kisemacho ''Nyerere angemkemea Dr. Slaa au CCM?'' ambayo imeandikwa na Arcado Ntagazwa.................. Ndani ya habari hii napenda nijikite zaidi kwenye paragraph moja ambayo mwandishi anasema:- ''Lakini, kwa mfano, mheshimiwa fulani anajua kuwa kuendelea kutumia majina ya kudandia kwa kughushi badala ya majina yake halisi ya Lameck Madelu Mkumbo, siku si nyingi yatamfikisha kwenye makosa ya kijinai. Wanasema ukitaka kuheshimiwa uanze kujiheshimu''..........mwisho wa kunukuu, nilikuwa napenda kufahamu huyu mheshimiwa aliyetajwa hapa kutumia jina lisilo lako wakati jina lake halisi ni Lameck ni yupi? je kwa nini atumie jina ambalo si lake kuna kitu gani anakificha na sheria ya nchi inasemaje katika suala kama hili?