Ni Nani Huyu- ENJI BIN UNUUTI?? TUSAIDIENI !!!

Grand Master Dulla

JF-Expert Member
Jul 20, 2012
411
146
Kwa wale wakazi wa kilwa na maeneo ya karibu yake nadhani mtakuwa mnalijua au mmeshakulisikia jina hili la Enji Bin Nuuti inasemekana kwamba jamaa alikuwa ni mtu wa kale sana aliyetokea kaskazini na sifa yake kubwa ni kwamba alikuwa ni mrefu sana,inasemekana kwamba jamaa aliletwa ili apime kina cha bahari ya mwambao wote wa pwani yetu mbaka arabuni basi hata maji yawe na kina kiasi gani yalikuwa yanamfikia magotini tu.!!

Inasemekana kuwa huyu jamaa alikuwa anakwenda baharini anakamata samaki anayemtaka halafu ananyoosha mkono juu hafu samaki anakauka kwa jua mara moja ndio anamla.Wapemndwa tusishangae sana mana kizazi hiki itakuwa kilikuwepo tu duniani si mnakumbuka kwa wale wasomaji wa biblia kuwa kulikuwa na kizazi cha majitu kilichotokana kati ya bin adam na malaika? Au kwa waliosoma kitabu cha Enoki anawaelezea hawa watu ni wa namna gani vizuri zaidi !!!

Iinavyoonekana huyu bwana alikuwa wa mwisho wa kizazi chake cha majitu.Kisa kingine ni kwamba jamaa aliletwa kupima kina cha bahari na hawa wageni labda waarabu au waajemi na alipofika pwani ya kilwa inasemekana kuna sehemu alikuta kina kirefu sana maji yalimfikia kiunoni akaweka alama hadi leo nasikia alama alizoweka zipo.

Hadithi hii mimi nilihadithiwa na babu yangu aliyekuwa na umri wa miaka yapata 107 sasa ni marehem (rip) na alinihakikishia kuwa stori hii ni kweli na akaniambia kuwa hapo kilwa hadi leo kaburi lake lipo!!! ila alisema lipo pembezoni karibu na bahari.
Na yeye history hii alihadithiwa na mzee wake.hivyo basi wana JF tunawaomba kama kuna mtu alishawahi kusikia habari yeyote kuhusu sahaba huyu naomba atujuze maana hili ni jambo la kihistoria kwetu na nchi yetu kwa ujumla na ni utalii tosha.
 
mmmmmmmmmmmh........

Bibi yangu aliwahi kusimulia kuna mdudu anaitwa nyangurapembe, alowahi kumuona anielezee alivyo.....

Kaka kizazi cha majitu kilishaangamizwa toka kale...... Maandiko hayakuandika kama kuna masalia yalibaki.....

Pia urefu wa huyo mtu inategemea ufupi wa waliomzunguka....

Sitaki kuamini hilo lakini acha wengine waje, inawezekana kuna maajabu hatuyajui....

Hapa sibanduki walaaahi nimeipenda hii historia.......(nzuri maana haiongelei muungano wa pemba, zimbabwe na tanganyika)
 
Wiki ijayo naenda zangu KILWA KIPATIMO, nitafanya udadisi, nitaweka habari kamili humu...................

Lakini nadhani hii post imepotea njia, ilitakiwa ipelekwe kule kwenye jukwa la HISTORIA..


MODS TAFADHALI...

Mtambuzi katafiti uje na newz......

By the way jukwaa la historia lipo wapi? Nielekeze njia plz
 
Last edited by a moderator:
"Huwezi kumtambua mchawi unless wewe ni mchawi pia" by Benjamin W. Mkapa
 
Tupe vituko vyke basi kama mlivyosikia nyie.

Ukifika Bwagamoyo, tembelea Kaole Crocodile Ranch. Ukifika hapo, muulize Mzee mmoja anaitwa Abdoo, usistuke kwa mvi zake, ni mcheshi sana, ukitaka kufurahi ukienda nenda na pakiti za sigara kali umwambie nimekuletea zawadi nataka kisa cha Unju bin Unuku. Basi naam, utastarehe na roho yako. Nakutakia utafiti mwema.
 
Hadithi kama hizi zilikuwa na maana kuu moja, mara nyingi walikuwa wakihadithiwa watoto wadogo na kuwafanya kuwa na hofu ya Mungu. Watoto walikuwa wakiendelea kukua wanajiuliza kama kulikuwa na majitu ya kutisha hivi na Mungu ni mkuu kuliko haya majitu basi Mungu ni wa kuugopewa zaidi.

Siku hizi hadithi hizi hatukuwasimulia watoto wetu na ndio maana watoto wetu wamekosa maadili, wanaapizana hovyo hovyo, wanafanya mambo ambayo hata sisi wazazi wao tunawashangaa. Mwisho wa siku wa kulaumiwa ni sisi tulioshindwa kuwapasia hadithi hizi watoto wetu na dhambi zao tutazibeba sisi wazazi.
 
Hadithi kama hizi zilikuwa na maana kuu moja, mara nyingi walikuwa wakihadithiwa watoto wadogo na kuwafanya kuwa na hofu ya Mungu. Watoto walikuwa wakiendelea kukua wanajiuliza kama kulikuwa na majitu ya kutisha hivi na Mungu ni mkuu kuliko haya majitu basi Mungu ni wa kuugopewa zaidi.

Siku hizi hadithi hizi hatukuwasimulia watoto wetu na ndio maana watoto wetu wamekosa maadili, wanaapizana hovyo hovyo, wanafanya mambo ambayo hata sisi wazazi wao tunawashangaa. Mwisho wa siku wa kulaumiwa ni sisi tulioshindwa kuwapasia hadithi hizi watoto wetu na dhambi zao tutazibeba sisi wazazi.

Sidhani kwamba ni kweli jua kabisa siku zote lisemwalo lipo!! unakumbuka kisa cha wayaudi weusi wabantu wa zimbabwe wale jamaa walikuwa wanaadithiwa hivi hivi na babu zao kuwa sisi asili yetu hasa ni wayaudi,watu wakawa wanawadharau na kuwacheka juzi mzungu kaenda kasikiliza stori akaona ngoja ajiridhishe akawapima DNA, shangaa!!
jamaa kumbe ni wayaudi kabisa tena damu yao ni ya kiyaudi kushinda hata wale wayaudi wazungu wa israel na marekani!!! hivi vitu vinaukweli hawawezi watu pwani yote wakatunga stori inayofanana.
 
Da nami nimemsikia kwa jina la Unzi Bin Ununuk, na hiyo stori nilishaipata sema nilisikia alizama baharini pande za Kilwa.
 
Hadithi kama hizi zilikuwa na maana kuu moja, mara nyingi walikuwa wakihadithiwa watoto wadogo na kuwafanya kuwa na hofu ya Mungu. Watoto walikuwa wakiendelea kukua wanajiuliza kama kulikuwa na majitu ya kutisha hivi na Mungu ni mkuu kuliko haya majitu basi Mungu ni wa kuugopewa zaidi.

Siku hizi hadithi hizi hatukuwasimulia watoto wetu na ndio maana watoto wetu wamekosa maadili, wanaapizana hovyo hovyo, wanafanya mambo ambayo hata sisi wazazi wao tunawashangaa. Mwisho wa siku wa kulaumiwa ni sisi tulioshindwa kuwapasia hadithi hizi watoto wetu na dhambi zao tutazibeba sisi wazazi.

Ndo maana wengine wanaleteana mizaha kuhusu Mungu na matokeo yake misahafu inakojolewa.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom