Jambazi alipora nini??? Je Uli anaweza kuwa shahidi kwenye hii kesi. Mbona mjambazi ya EPA uchunguzi unaendelea imekuwaje huyu siku moja tu mahakamani.
Ni lugha ya karaha, lakini jazba ilinituma nitumie huu msemo.Duh,hyo ya kutawaza kabla ya kunya nimeipenda.kwa mujibu wa kova huyo jamaa ni mzoefu katika matukio hayo.haingii akilini ajutie hicho kitendo.kova kweli govi
Kesi iliyokuwepo ni sensitive na imeligusa Taifa zima na zaidi pale wengine wanaposema ni serikali na wengine wanaposema ni Chadema ,wananchi wanataka kujua ni nani alienyuma ya jambazi hili au tuseme kesi hii .Na kama unavyojua Chadema ni watu wa makanisa kanisa na jamaa ameenda huko ili wamsaidie ila wakanisa wamevunja amri ya mtu anaeungama.
Kama ni toba, mbona kakana mashitaka. Hivi ni viini macho. Pia wanataka kutumia delay tactics--eti august ndio itasomwa tena!Kuna maswali mengi nyuma ya kiinimacho kilichotangazwa na kamanda Kova juu ya utekaji wa dr Ulimboka. kati ya mengi, Maswali yafuatayo yana wafanya Tanzania wasiamini taarifa ya jeshi la polisi juu ya utekaji na utesaji aliofanyiwa dr Ulimboka.
- Kwamba mtekaji alienda kufanya toba kanisani haiingii akilini hata kidogo.Si rahisi kiasi hicho kwanza kanisa lipo kila mahali. Toba hiyo ingeweza kufanyika Kenya, Uganda na nchi nyingine bila hatari ya mtuhumiwa kukamatwa.
- Kwamba mtekaji alitumwa na mtu asiyemfahamu tena anafanya kazi serikalini,serikali ipi ya Kenya au hii ya JK? Kwa hiyo Watanzania walikuwa sahihi kuituhumu serikali? Mbona waziri mkuu na Rais walikanusha kwa sauti kali tena ya kuapa? Haya mwajiri wa mtekaji anafanya idara ipi? Kama mwajiri na mwajiriwa hawafahamiani mshahara baada ya kazi ulilipwa vipi? Nani alishawahi kuajiriwa bila kufahamiana kwanza na mwajiri? Kujaza mkataba wa kazi?
- Mbona katika hili taarifa ya polisi haikuonyesha picha ya mtuhumiwa? Mbona watuhumiwa wengine huonyeshwa picha zao pindi wanapokamatwa?
- Kwa madhehebu mengi ya Kikristo, toba haifanywi kwa kwenda kuisema dhambi kwa mchungaji isipokuwa kanisa Katoliki,Je kanisa aliloenda mtekaji lina utaratibu huo wa toba?
- Kwamba polisi imemnasa mtuhumiwa,kwa taarifa hiyo ndo mwisho wa uchunguzi wa chaini ya kiharifu iliyo nyuma ya tukio hili?
Embu waonyeshe picha zake kwenye vyombo vya habari, si ajabu si Mkenya, wawezakuta ni Mmbongo wa hapahapa, watu wanamjua na ndugu zake!