Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,349
- 6,476
Akiwahutubia akinamama huko Kigoma, Mama Kikwete kwa nyakati mbili tofauti amezungumzia juu ya wafanyao kampeni za uchaguzi kwa kutumia udini na ukabila kuwa ni hatari kwa amani ya nchi.
Bila kukitaja chama, NGO au watu binafsi alionekana kuguswa sana na hilo swala na alijua kuwa akina mama ndio karata yake ya mwisho katika kulipuuzia hilo na kudumisha amani.
Swali kubwa la kujiuliza hapa, HIVI MAMA KIKWETA ALIDHAMIRIA KUWANYOOSHEA KIDOLE AKINA NANI? CUF, CHADEMA, NCCR, CCM au TLP?
Hiki ni kitendawili ninachowaomba wenzengu hapa JF tutatue bila upendeleo. Natanguliza shukrani zangu za dhati.
Je, Urais ni suala la kifamilia aliwaambia?