Nimependa sana maelezo yako. Kama asipokuelewa basi tena. Kwa nyongeza amuheshimu na kumuogopa MUNGUAcha kuzunguka sana, ameshakuambia yeye ni mke wa mtu, halafu mume wake ni mtu wa safari, then anakupigia na kutaka kudumisha mawasiliano, anakuuliza wkend plans, kwani wewe ni mgeni katika gemu mpaka usijue kuwa anakutaka? Mbaya zaidi unamsifu kuwa ni mzuri, yaani unatuambia mpaka ongea yake jinsi inavyokuvutia. Moyoni mwako umeshaanza kuwaza ufuska, na hata tukikushauri tayari unajua nini chakufanya. Kabla hujafanya huo ufuska, jiweke katika nafasi ya yule mume wake halafu imagine how would you feel? Imagine mchumba wako akijua itakuwa hasara kwa nani? Mume wake akijua na labda ndoa ikavunjika,mtoto wao ataishi katika mazingira gani? Mbaya zaidi unaweza kuondoka dunia hii siku si zako.Kama hiyo ni tabia ya huyo mwanamke unaweza kuwa msaada kwake, muoneshe kuwa wapo wanaume wanaojali wake za wenzao. Mwekee mazingira ya kuelewa kuwa sisi wanaume hatupendi kuwa mbali na familia zetu, tunafanya hivyo kwa sababu wakati mwingine hatuna jinsi, na tunajua wazi kuwa sisi sote ni dhaifu, lakini tunawaamini kuwaacha nyumbani tukaenda kutafuta riziki, na kwamba tunawapenda sana. Kwa wivu tulionao tungeamua kukaa tu nyumbani kuwalinda, lakini upendo tulionao umezaa imani kwao kuwa watalinda na kuheshimu ndoa zetu kama tunavyo linda na kuheshimu tunapokuwa mbali nao.