Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,269
Leo ni Jumamosi tarehe 13 Mfunguo Tisa Jamadi Thani mwaka 1433 Hijria, inayosadifiana na terehe 5 Mei mwaka 2012 Miladia.
Siku kama hii ya leo miaka 1003 iliyopita alifariki dunia mjini Cairo Misri mwanafizikia, mtaalamu wa hesabu na msomi mkubwa wa Kiislamu Ibn Haytham.
Alizaliwa mwaka 354 Hijiria katika mji wa Basra ulioko kusini mwa Iraq ya leo. Baada ya juhudi nyingi za kusoma na kufanya utafiti Ibn Haytham alitokea kuwa mtaalamu mkubwa wa hesabu. Mbali na fani hiyo ya hesabu Ibn Haytham alikuwa pia mtaalamu na mwalimu wa elimu za fizikia, tiba, falsafa na nyota ambapo aliweza kufanya utafiti yakinifu kuhusiana na mwanga. Miongoni mwa mambo mengine aliyoyafanya Ibn Haytham ni kuanzisha mbinu na njia mpya katika elimu ya hesabu. Ibn Haythamameandika vitabu vingi katika fani za elimu ya hesabu na tiba. Miongoni mwa athari zake muhimu ni kitabu kiitwacho "Al Manadhir" ambacho kimetarujumiwa kwa lugha ya Kingereza.
Siku kama hii ya leo miaka 31 iliyopita alifariki dunia Bobby Sands, mwanamapambano maarufu wa Ireland baada ya kukaa katika jela ya Uingereza, kupambana na kugoma kula chakula kwa siku 66 akipigania uhuru wa nchi hiyo. Kufuatia kifo cha Bobby Sands na wanaharakati wenzake wa Ireland waliosusia chakula wakiwa jela, serikali ya kikoloni ya Uingereza ilikabiliwa na wimbi la malalamiko kutoka ndani na nje ya nchi hiyo. Aidha kifo cha mwanamapambano huyo kilizusha hali ya ukosefu wa amani huko Ireland Kaskazini. Kwa ajili hiyo Bobby Sands akatambulika kuwa bingwa wa mapambano ya wananchi dhidi ya wavamizi Waingereza huko Ireland.
Na siku kama ya leo miaka 37 iliyopita aliuawa shahidi Majid Sharif Waqifi ndani ya ofisi ya taasisi ya Mujahidina Khalqi wa Iran maarufu kwa jina la MKO na wapinzani wa serikali ya Iran wenye kufuata siasa za Umaksi. Taasisi hiyo iliundwa mnamo mwaka 1344 Hijiria Shamsia na vijana kadhaa kwa lengo la kupambana kwa silaha na vikosi vya utawala wa Shah wakati huo. Hata hivyo baadhi ya wajumbe dhaifu wa taasisi hiyo waliathiriwa taratibu na fikra za umaksi na kuzusha mivutano ya ndani sambamba na kuwaua wanachama walioonekana kuwa na imani thabiti ya Kiislamu, kwa ajili ya kuwania madaraka katika taasisi hiyo. Baada ya Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran mwaka 1979, na kutokana na siasa za viongozi wa MKO za kufuata mirengo isiyo sahihi na tamaa yao ya kuwania madaraka, kundi hilo liligeuka na kuwa mpinzani mkubwa wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran. Tokea mwaka 1981 taasisi hiyo iliendeleza vitendo vya kigaidi vya kuwalenga viongozi na watu kawaida mitaani. Hatimaye viongozi wa taasisi walishindwa kudumisha siasa zao za kigaidi nchini na kulazimika kukimbilia nchi za kigeni. Wananchi wa Iran wanalitambua kundi hilo kama kundi la "Munafiqina" yaani wanafiki, kutokana hiana pamoja na jinai zao dhidi ya taifa la Iran na vilevile ushirikiano wao mkubwa na dikteta wa zamani wa Iraq, Saddam Hussein dhidi ya taifa hili.
Siku kama hii ya leo miaka 1003 iliyopita alifariki dunia mjini Cairo Misri mwanafizikia, mtaalamu wa hesabu na msomi mkubwa wa Kiislamu Ibn Haytham.
Alizaliwa mwaka 354 Hijiria katika mji wa Basra ulioko kusini mwa Iraq ya leo. Baada ya juhudi nyingi za kusoma na kufanya utafiti Ibn Haytham alitokea kuwa mtaalamu mkubwa wa hesabu. Mbali na fani hiyo ya hesabu Ibn Haytham alikuwa pia mtaalamu na mwalimu wa elimu za fizikia, tiba, falsafa na nyota ambapo aliweza kufanya utafiti yakinifu kuhusiana na mwanga. Miongoni mwa mambo mengine aliyoyafanya Ibn Haytham ni kuanzisha mbinu na njia mpya katika elimu ya hesabu. Ibn Haythamameandika vitabu vingi katika fani za elimu ya hesabu na tiba. Miongoni mwa athari zake muhimu ni kitabu kiitwacho "Al Manadhir" ambacho kimetarujumiwa kwa lugha ya Kingereza.
Siku kama hii ya leo miaka 31 iliyopita alifariki dunia Bobby Sands, mwanamapambano maarufu wa Ireland baada ya kukaa katika jela ya Uingereza, kupambana na kugoma kula chakula kwa siku 66 akipigania uhuru wa nchi hiyo. Kufuatia kifo cha Bobby Sands na wanaharakati wenzake wa Ireland waliosusia chakula wakiwa jela, serikali ya kikoloni ya Uingereza ilikabiliwa na wimbi la malalamiko kutoka ndani na nje ya nchi hiyo. Aidha kifo cha mwanamapambano huyo kilizusha hali ya ukosefu wa amani huko Ireland Kaskazini. Kwa ajili hiyo Bobby Sands akatambulika kuwa bingwa wa mapambano ya wananchi dhidi ya wavamizi Waingereza huko Ireland.
Na siku kama ya leo miaka 37 iliyopita aliuawa shahidi Majid Sharif Waqifi ndani ya ofisi ya taasisi ya Mujahidina Khalqi wa Iran maarufu kwa jina la MKO na wapinzani wa serikali ya Iran wenye kufuata siasa za Umaksi. Taasisi hiyo iliundwa mnamo mwaka 1344 Hijiria Shamsia na vijana kadhaa kwa lengo la kupambana kwa silaha na vikosi vya utawala wa Shah wakati huo. Hata hivyo baadhi ya wajumbe dhaifu wa taasisi hiyo waliathiriwa taratibu na fikra za umaksi na kuzusha mivutano ya ndani sambamba na kuwaua wanachama walioonekana kuwa na imani thabiti ya Kiislamu, kwa ajili ya kuwania madaraka katika taasisi hiyo. Baada ya Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran mwaka 1979, na kutokana na siasa za viongozi wa MKO za kufuata mirengo isiyo sahihi na tamaa yao ya kuwania madaraka, kundi hilo liligeuka na kuwa mpinzani mkubwa wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran. Tokea mwaka 1981 taasisi hiyo iliendeleza vitendo vya kigaidi vya kuwalenga viongozi na watu kawaida mitaani. Hatimaye viongozi wa taasisi walishindwa kudumisha siasa zao za kigaidi nchini na kulazimika kukimbilia nchi za kigeni. Wananchi wa Iran wanalitambua kundi hilo kama kundi la "Munafiqina" yaani wanafiki, kutokana hiana pamoja na jinai zao dhidi ya taifa la Iran na vilevile ushirikiano wao mkubwa na dikteta wa zamani wa Iraq, Saddam Hussein dhidi ya taifa hili.