Wadau
Katika kipindi cha week moja tumekuwa katika msukosuko wa kuwasema au kuwataja mawaziri ambao wanashtumiwa kutumia madaraka yao vibaya kwa kukwapua mali za nchi yetu. Haya yamekuwa yakitokea kwa viongozi kadhaa ndani ya serikali na chama tawala (CCM).
Vikao vya ndani ya CCM tunasikia vinafanyika mara kwa mara na hivi karibuni kulikuwa na vikao wa wabunge kutoka CCM. Wengi hatujui haswa yanayojadiliwa katika hivyo vikao zaidi ya habari za hapa na pale ambazo hama tunazipata humu kwenye jamvi (JF) au vyombo vingine vya habari.
Swali linalonijia mara kwa mara ni Je katika hivyo vikao CCM wanajadili jinsi ya kuendelea kutawala au jinsi ya kumkomboa Mtanzania wa kawaida katika hali ngumu ya maisha inayomkabili? Viongozi wanaoshtumiwa kuwaletea watanzania hali ngumu ya maisha bado wanaendelea na vyeo vyao na hata wabunge wanaojaribu kuwakemea wanatishiwa maisha yao. Je CCM inafanya hivyo kwa manufaa ya Mtanzania au mwana CCM (aliye na cheo).
Enyi wana CCM, tuambieni mbiu yenu kuu ni Kuendelea kutawala au Kumkomboa Mtanzania katika hali ngumu ya maisha?
Katika kipindi cha week moja tumekuwa katika msukosuko wa kuwasema au kuwataja mawaziri ambao wanashtumiwa kutumia madaraka yao vibaya kwa kukwapua mali za nchi yetu. Haya yamekuwa yakitokea kwa viongozi kadhaa ndani ya serikali na chama tawala (CCM).
Vikao vya ndani ya CCM tunasikia vinafanyika mara kwa mara na hivi karibuni kulikuwa na vikao wa wabunge kutoka CCM. Wengi hatujui haswa yanayojadiliwa katika hivyo vikao zaidi ya habari za hapa na pale ambazo hama tunazipata humu kwenye jamvi (JF) au vyombo vingine vya habari.
Swali linalonijia mara kwa mara ni Je katika hivyo vikao CCM wanajadili jinsi ya kuendelea kutawala au jinsi ya kumkomboa Mtanzania wa kawaida katika hali ngumu ya maisha inayomkabili? Viongozi wanaoshtumiwa kuwaletea watanzania hali ngumu ya maisha bado wanaendelea na vyeo vyao na hata wabunge wanaojaribu kuwakemea wanatishiwa maisha yao. Je CCM inafanya hivyo kwa manufaa ya Mtanzania au mwana CCM (aliye na cheo).
Enyi wana CCM, tuambieni mbiu yenu kuu ni Kuendelea kutawala au Kumkomboa Mtanzania katika hali ngumu ya maisha?