Ni lini CCM ilibadilika na kuanza kuwa rafiki wa Waislamu Tanzania?

Status
Not open for further replies.
the truth is that the CCM government has acted arbitrarily and is not alive to the grave situation into which it has plunged the country. By being biased and allowing itself to be duped by the Catholic clergy that Muslim preaching was insulting to Christianity, the CCM government has embarked on a course of action which violates the constitutional rights of Muslims to propagate religion, is arbitrary and without any regard to the due process of law - [URL="http://www.igs.net/%7Ekassim/mwembechai/index.html"](Barua ya Abu Aziz kwa Mwanasheria Mkuu; Mwembechai Killings and the Political Future of Tanzania)
[/URL]
Nipo katika kuandika makala fupi yenye kuhusiana na kichwa hicho cha habari. Swali hili limekuja baada ya kusoma hoja alizotoa Mufti Shehe Shaaban Bin Simba akiitetea serikali ya CCM na uongozi wake.

Nilichukua muda kidogo na kurudi kusoma vitabu viwili ambavyo ni maarufu miongoni mwa Waislamu wa Tanzania ambavyo vinaelezea kwa kirefu jinsi CCM na serikali yake ilivyowakandamiza Waislamu. Kitabu cha Prof. Hamza. M. Njozi - ambaye kwa wanaokumbuka nilifanya naye mahojiano ya kina mwaka 2006 - cha "Mwembechai Killings and the Political Future of Tanzania" na kupitia maandishi ya Bw. Mohammed Said kuhusu historia ya Waislamu katika harakati za uhuru - ikiwemo kile kitabu kinachomhusu Abdulwahid Sykes.


Vitabu hivyo viwili na maelezo mengi ya ziada kabla ya 2010 yalijaribu kutuaminisha kuwa CCM ndio ilikuwa kikwazo cha maendeleo ya maslahi ya Waislamu:

a. Kuanzia kufutwa kwa EAMWS hadi mauaji ya Mwembechai na mambo mengine yote kati yake.

b. Kwamba pamoja na jitihada mbalimbali CCM iligeuka na kuwa sehemu ya Kanisa au kutumiwa na Kanisa - Dr. Njozi na barua ya Abu Aziz vinathibitisha mashtaka hayo makubwa.

Sasa, bila ya kwenda mbali sana kuna kitu kimebadilika hivi karibuni ambacho kinawafanya Waislamu kuiunga mkono CCM na uongozi wake. Utetezi mkubwa uliofanywa na vyombo mbalimbali vya habari vya Kiislamu na watu mbalimbali wakati wa kampeni kuitetea CCM kwa wapiga kura vinanifanya niamini kabisa kuwa kuna kitu cha msingi sana ambacho kimebadilika kiasi cha kuifanya CCM - chama ambacho kilikuwa kinaonekana na kiini cha tatizo ya Waislamu kuanza kupendwa, kukumbatiwa na hata kufikia serikali yake kutetewa kwa kiasi ambacho hatujawahi kuona.

Ndio swali liko mbele yetu; CCM imebadilika kitu gani hadi kuwa rafiki wa Waislamu leo hii? Ni sera na mfumo gani wa CCM ambao unawafanya baadhi ya Waislamu kuona kuwa maisha na maslahi yao yatalindwa vizuri na CCM kuanzia sasa? Je, endapo uongozi ujao wa CCM utakuwa ni wa tofauti na huu uliopo bado CCM itapata support hii kubwa? Je, makosa yote ya CCM na serikali yake ya huko nyuma yamesamehewa na sasa "tugange yajayo" au yamewekwa kiporo tu ili ukija uongozi tofauti na huu wa sasa yakumbushiwe tena?

Je, Waislamu wote wanatakiwa kuanzia sasa kuiunga mkono CCM, kutoikosoa, kutoilalamikia, kutoonesha makosa yake wala kutokubaliana hata kidogo na wale wenye kuikosoa? Kwa maneno mengine, Muislamu anaweza kuwa Muumini mzuri huku bado anaendelea kuipinga CCM kinyume na maelekezo ya viongozi wake wa kidini? Au bado wapo baadhi ya Waislamu ambao msimamo wao haujatetereka dhidi ya CCM na serikali yake?

Ni maswali ya uchokozi wa kifikra tu. Natumaini mawazo yenu juu ya somo husika yatanisaidia kuandika makala ambayo itajaribu kushughulikia suala hili kwa kiasi cha kutosha.

Mimi nina maoni haya:

1. Kama CCM ya zamani, ambayo kwa mtazamo wangu ilikuwa better, inashutumiwa kuwakandamiza Waislamu, CCM ya sasa, ambayo inakumbatia ufisadi na viongozi wasiowajibika, haiwezi kuwa imebadilika kuwanufaisha Waislamu unless kama na wao wanashabikia huo uozo. Ni kitu gani ambacho serikali ya CCM imekifanya kuboresha maisha ya Watanzania wakiwemo Waislamu has huduma muhimu za jamii kama vile elimu na afya wakati matokeo ya shule zetu yanaendelea kuwa mabaya na huduma ya afya ndiyo hiyo tena?

2. Mimi naona provided CCM itakuwa na viongozi wa kuu wa nchi Waislamu kama ilivyo sasa itaendelea kupendwa na Waislamu na ikitokea wakawepo wa dini nyingine mapenzi yataisha.

3. CCM haijabailika kiasi cha kutoka 'bad kwenda good' ila ilipoona inalaunmiwa kutotekeleza ahadi yake ya kutafuta ufumbuzi kwa suala la Mahakama ya Kadhi, ikaahidi kuanzisha Mahakama ya Kadhi na Tanzania kujiunga na OIC. Tangu hapo Waislamu wakaona CCM ni chama kinachosikiliza kilio chao. Wakati wa kampeni walikuwa wanampiga vita Dr Slaa na magazeti yao yalichangia sana na sasa wameanza kukipiga vita waziwazi Chadema na sababu yake si kitu kingine ni udni kwa vile wanaamini chama hicho kina waumini walio wengi Wakristo.
 
Mzee MMM,
Heshima na salaam mbele,
Hii mijadala ya amani ya kidini ni sensitive na muhimu sana,
Inaondoa sintofahamu, inajenga kuelewana, kuaminiana na kukubaliana kutofautiana nk.

Kimsingi historia ya TANU, CCM na uislam ni ndefu kidogo,

Kuna baadhi ya malalamiko ya waislam, mapya na yazamani dhidi ya serikali ya CCM yana ukweli na yanahitaji ufafanuzi na ufumbuzi.

Na hii ni muhimu kwa chama chochote kitakachokuwa madarakani.

Hii pia inapply kwa ALL religious institutions.

La msingi ni; kuwa na katiba ya watanzania kwa ajili ya watanzania.

Yoote haya yatapata ufumbuzi.

Haya mambo yawekwe wazi kwenye katiba mpya,
Tusimumunye na kulea maradhi.

Hakika nchi ya neema itakuwa sii ndoto wala miujiza
 
Nimefurahia sana michango ya watu ambayo imeonesha restraint kubwa sana (ukiondoa wachache ambao huwa hawawezi kujizuia kuchukua cheap shots). Lakini yawezekana CCM ndio inachezea akili za Watanzania namna hii?
 
hapa ccm inashindwa kutimiza wajibu wake kama chama tawala, hawasemi ukweli, wanatumia cheap resolutions kama kutoa ahadi za uongo ilimradi kuwaridhisha waislamu! pia waislamu nao jamani mnatakiwa mjifunze kwa kufanya maendleo, waliopo serious mbona wapo fresh tuu? mnaojibweteka kutaka msaada ndo manaachwa hivyoo!
 
Heshima yako mzee mwanakijiji, kwanza kabla ya yote naomba kuuliza ni maslahi gani waislam wa tanzania wanayakosa na ambayo wakristu wanayo. Nauliza hivi kwa sababu kabla haujamsaidia mtu lazima ujue matatizo aliyonayo. Pili tatizo la waislamu kulalamika liko dunia nzima sehemu zote wanalalamika wanaonewa. Na kama ni tatizo la dunia nzima basi Tanzania pekee haiwezi kulimaliza. Naomba ndugu zangu waislam watwambie maslahi wanayoyataka ili tuyajue
 
Kwani hao viongozi wa upinzani,walikuwa chama gani wakati huo mnaodai waislam walikuwa wanakandamizwa?....honestly,this is one of the cheapest shots i've ever seen!!
 
Heshima yako mzee mwanakijiji, kwanza kabla ya yote naomba kuuliza ni maslahi gani waislam wa tanzania wanayakosa na ambayo wakristu wanayo. Nauliza hivi kwa sababu kabla haujamsaidia mtu lazima ujue matatizo aliyonayo. Pili tatizo la waislamu kulalamika liko dunia nzima sehemu zote wanalalamika wanaonewa. Na kama ni tatizo la dunia nzima basi Tanzania pekee haiwezi kulimaliza. Naomba ndugu zangu waislam watwambie maslahi wanayoyataka ili tuyajue

Umekuwa kama Mkapa aliyewaita Waislamu kabla ya uchaguzi wa mwaka 2000 na kuwataka kuwapa kero na malalamiko yao kisayansi na bila kuchelewa akapewa na baada ya hapo kilichotokea ni BUSINESS AS USUAL!!

Sasa ikiwa kila mtu atakuja na kuomba aonyeshwe kereo za Waislamu itakuwa ni kama mchezo yaani tumekuwa kama Wabunge wetu wanaokwenda Majimboni na kuomba waoredheshewe kero zote zinazowakabili!!
Kwani Mbunge anaishi mbinguni? haishi na wapiga kura wake? inamaana hajui kero zao?

Waislamu walipigania Uhuru wa nchi hii ili Raia wote wafaidi matunda ya nchi hii kwa usawa na haki lakini hayakuwa hivyo! sasa Wataendelea kupigania haki yao hiyo ama wakiwa ndani chama Tawala, Upinzani au hata ikibidi Kuanzisha Chama Cha Kiislamu!! lakini haiko tayari kuburuzwa kibubusa na vyama uchwara vya kisiasa vinavyotaka kuingia madarakani kwa kutumia mgongo wa Waislamu!
 
Umekuwa kama Mkapa aliyewaita Waislamu kabla ya uchaguzi wa mwaka 2000 na kuwataka kuwapa kero na malalamiko yao kisayansi na bila kuchelewa akapewa na baada ya hapo kilichotokea ni BUSINESS AS USUAL!!

Sasa ikiwa kila mtu atakuja na kuomba aonyeshwe kereo za Waislamu itakuwa ni kama mchezo yaani tumekuwa kama Wabunge wetu wanaokwenda Majimboni na kuomba waoredheshewe kero zote zinazowakabili!!
Kwani Mbunge anaishi mbinguni? haishi na wapiga kura wake? inamaana hajui kero zao?

Waislamu walipigania Uhuru wa nchi hii ili Raia wote wafaidi matunda ya nchi hii kwa usawa na haki lakini hayakuwa hivyo! sasa Wataendelea kupigania haki yao hiyo ama wakiwa ndani chama Tawala, Upinzani au hata ikibidi Kuanzisha Chama Cha Kiislamu!! lakini haiko tayari kuburuzwa kibubusa na vyama uchwara vya kisiasa vinavyotaka kuingia madarakani kwa kutumia mgongo wa Waislamu!
Mkuu umeulizwa kero za Waislaam kwa maana kwamba ni kero za kundi moja kati ya wananchi wote..hatuwezi soote kusali msikitini mmoja wewe wakilisha..

Mbunge huwakilisha watu wa jimbo lake bungeni..hakuna mtu alosema serikali au sisi wananchi hatufahamu kero za wananchi wote kwa ujumla wake ila hatujui kero za kila jimbo na priority zao na ndio sababu ya kuwa na wawakilishi wa majimbo.

Sasa wewe waona taabu gani kuwakilisha kero za waislaam ikiwa wewe ni Muislaam na unazijua au kifikra unafikiri Dr Slaa na Chadema hawawezi kuzitatua kwa sababu sio waislaam?..

Mkuu wangu kwa mwendo huu hatuwezi kufika mahala kwa sababu sisi kama Wakerewe kero zetu zinawakilishwa na mbunge wetu,vivyo hivyo majimbo yote huwakilishwa bungeni,sasa mimi sioni tatizo hata kidogo kama Waislaam wanaweza orodhesha kero zao ktk kutafuta haki yao kitaifa.. Si tunasema Tanzania ni yetu wote? Then kuna taabu gani kusema unachotaka?

Nini, Mahakama ya kadhi?
Hili sio jambo rahisi kuwa la kikatiba pasipo referandum ya waislaam wenyewe kupiga kura for or against, kwa sababu hatuwezi kuwalazimisha watu ambao hawafuati dini kwenda mahakamani kwa sababu tu wamezaliwa Waislaam na sii waislaam kiimani..Watu ambao zinaa sii haramu kwao na wamezaa nje mitoto kibao kisha twende kuwanyang'anya mirathi kwa makosa ya baba zao ambao tumeshindwa kufuata maadili ya dini na kukumbatia zinaa kama hatuna dini.. Acheni zinaa au tuwahukumuni nyie kwanza kuzuia matatizo ya mirathi,t na ndoa haramu..

Haya swala la OIC?
M adhani Chadema ilikuwa na sambamba na CUF miaka sita iliyopita wakati swala hili lipo ubaoni..
Binafsi sioni utata hata kidogo, kwani kama Tanzania ni mwanachama wa Commonwealth ya Malkia,hakuna sababu ya kuwazuia Zanzibar ambao hawamtambui Malkia kama sisi bara..

Haya jingine lipi? Maana mimi siyajui yote isipokuwa nayoyasoma ktk magazeti kinyume cha pale naijua chuki ya western world agaist Islam inatokana na manufaa ya interest zao na sii chuki ya kiimani..
Fremaison tactic of rule and concur ni ku create hate within the society na wanapoona interest zao zipo matatani hu create pia brain storm divension kupindua attention ya watu kama vile Loliondo ilivyoondoa mada zote kubwa na kero za wananchi...wao wanasema unaleta tumaini jipya..
 
Fremaison tactic of rule and concur ni ku create hate with the society na wanapoona interest zao zipo matatani hu create pia brain storm ku divension attention kama vile Loliondo ilivyoondoa mada zote kubwa na kero za wananchi...wao wanasema unaleta tumaini jipya..

Mkandara, mojawapo ya vitu ambavyo nadhani watawala wanatuchezea akili ni kutufanya tuamini kuwa maslahi yetu yamegawanyika. Kwa mfano, kuna wanaotaka barabara nzuri na wengine hawataki, hospitali bora na madawa nafuu na ya kutosha na wengine hawataki n.k Ukijiuliza sana utaona kuwa baadhi ya mabo ya kidini yanayodaiwa ni mambo ambayo tayari yanaweza kufanywa pasipo matatizo yoyote. Kwa mfano, binafsi kweli kabisa ningependa Mahakama ya Kadhi iaanzishwe na tujiunge OIC halafu labda tutaanza kudai mambo mengine kwa pamoja.

Na inawezekana kabisa CCM inayaweka mambo hayo kiporo na kuyafanyia kama nyama ya kuwavutia watu tu kuja; kwamba "tutafanya tutafanya". Kwa sababu ukifikiria sana siku mambo hayo makubwa yakifikia tamati sijui CCM itatumia mbinu gani tena.
 
Nimefurahia sana michango ya watu ambayo imeonesha restraint kubwa sana (ukiondoa wachache ambao huwa hawawezi kujizuia kuchukua cheap shots). Lakini yawezekana CCM ndio inachezea akili za Watanzania namna hii?

Nadhani CCM kama chama cha watu kinakereka sana na mambo kama haya na wapo watu makini wanaochukia kuiona hali hii. Tatizo ni kuwa CCM sio chama kile cha wananchi, ni chama cha mapapa 3 au 4 ambao kwa makusudi na kutumia pesa wamo ndani ya CC na NEC, wamenunua na kuwadhibiti baadhi ya viongozi na sasa chama hakina kauli.

Kukudhihirishia haya,uchaguzi mkuu licha ya RA kuchomeka udini kwa rushwa kwa viongozi wa dini na vyombo vya habari ili kulinda maslahi yake, bado wananchi wakiwemo wana CCM wameonyesha hasira zao wazi wazi.
Nilitegemea CCM na serikali yake kukemea hali ya hatari ya mtu kutumia pesa na vyombo vya habari kueneza chuki, lakini nani aseme ikiwa wote wamefika hapo kwa pesa za Igunga?Angalia rushwa inavyoigawa UVCCM kwa maslahi ya hawa watu wachache na angalia majaribio ya kutaka kuua viongozi kwa kisingizio eti wanapiga vita dini fulani. Yaani mtu akisema rushwa! basi ni vita dhidi ya dini.

Kama mbunge mmoja anaweza kutoa 50,000 kwa vijana 107, itashindikana vipi kununua kiongozi wa dini ili kueneza chuki dhidi ya watanzania au chama fulani cha kisiasa. Leo FM station zinaimba kuhusu Chadema kama chama cha kidini, fikiria kwanini wimbo huu umeshika kasi baada ya magazeti ya RA kuandika? inaonekana kama CDM ndio mwanzo wa matatizo, na wananchi wameshau kuwa adui wao ni umasikini ujinga na maradhi. Adui yao ni rushwa inayotafuna mifuko yao, huku wakiimba nyimbo wasizo zijua.

Rushwa ni ugonjwa mbaya sana, unatafuna kila kona ya society. Rushwa imenunua viongozi wa serikali na dini kwa bei ndogo sana lakini kwa gharama kubwa sana ya taifa.
Sisi kama Watanzania tusimame kwa pamoja na kukataa ujinga wa rushwa inayoozesha jamii hasa viongozi wa serikali na dini. Hakuna tatizo kati ya watu wa imani tofauti ,tatizo ni walaghai kutumia rushwa kuwarubuni waganga njaa ili kulivuruga taifa. Na kwa bahati mbaya sana rushwa ukiichanganya na uongozi dhaifu ni sawa kambale ndani ya ziwa.
Leo RA na EL wanafaijika kwasababu mada ya Richmond na Dowans hazijadiliwi tena,leo hatuongeli kufeli kwa watoto, hali duni ya afya na umasikini uliotamalaki bali udini na Chadema. Inasikitisha sana.
 
Naona una muono finyu na mawazo mgando Mufti kuzungumza maneno yale amefikiri kwa kina na anajua nini kinachoendelea sio wewe unaosubilia habari zilizopikwa na kuwa muumini wa hizo. kwa kifupi na ndio ukweli uliopo baadhi ya serikali zilizopita ziliukandamiza sana uislam na waislam kwa ujumla hadi ikafikia mtu kufungwa kwa kusema yesu sio mungu,pia kumvunja viungo mzee wetu aliye mtetea, kuuwa waislam eti sababu mchungaji amepeleka malalamiko.hii sio haki na ni haramu kwa waislam kuruhusu haki isitendeke. mufti amesema hayo kwa kulinganisha uongozi uliopita uliufanyia nini uislam na uliopo unaufanyia nini, akaona afadhali japo sio sana awamu ya nne.
siku zote waislam hawataki wapendelewe elewa wewe MWANAKIJIJI WANACHOTAKA NI VIONGOZI WAADILIFU tofauti na makafiri ni watu wa kutaka kubebwa kila siku hata kama hawana sifa eti kisa MWALIMUaliwawekea msingi mzuri basi mjue ule msingi umezeeka mnabidi mjenge wenu mwingine siku zote batili huwa ni yenye kuondoka na haki uchukua nafasi yake.
waislam ni watu wa kukutaza mabaya siku zote ukisikia waislam wanakataza kitu fulani basi ujue kina madhala kuliko faida. na pia nakupongeza kusoma vitabu hivyo usisahau vile vya sivalon
 
Asante Mzee Mwanakijiji. Hapa kinachoonekana ni kuwa waislam wanatumika tena na hiyo CCM kujimaliza wenyewe, kwani hakuna sera, muundo au itikadi yeyote ya ccm iliyo badilika, hapa Kikwete ndiye anaonekana kuushupalia udini na wao (waislam) bila kujua wana shusha lawama kwa CDM. kweli "wajinga ndio waliwao" Kwani madai ya waislam (ambayo yako jumla jumla) miaka yote kuwa wanaonewa yamekuwa yakipelekwa serikalini (CCM) Leo sijui nini kimewasibu ndugu zetu hawa na kuifagilia CCM
 
Mkuu umeulizwa kero za Waislaam kwa maana kwamba ni kero za kundi moja kati ya wananchi wote..hatuwezi soote kusali msikitini mmoja wewe wakilisha..

Mbunge huwakilisha watu wa jimbo lake bungeni..hakuna mtu alosema serikali au sisi wananchi hatufahamu kero za wananchi wote kwa ujumla wake ila hatujui kero za kila jimbo na priority zao na ndio sababu ya kuwa na wawakilishi wa majimbo.

Sasa wewe waona taabu gani kuwakilisha kero za waislaam ikiwa wewe ni Muislaam na unazijua au kifikra unafikiri Dr Slaa na Chadema hawawezi kuzitatua kwa sababu sio waislaam?..

Mkuu wangu kwa mwendo huu hatuwezi kufika mahala kwa sababu sisi kama Wakerewe kero zetu zinawakilishwa na mbunge wetu,vivyo hivyo majimbo yote huwakilishwa bungeni,sasa mimi sioni tatizo hata kidogo kama Waislaam wanaweza orodhesha kero zao ktk kutafuta haki yao kitaifa.. Si tunasema Tanzania ni yetu wote? Then kuna taabu gani kusema unachotaka?

Nini, Mahakama ya kadhi?
Hili sio jambo rahisi kuwa la kikatiba pasipo referandum ya waislaam wenyewe kupiga kura for or against, kwa sababu hatuwezi kuwalazimisha watu ambao hawafuati dini kwenda mahakamani kwa sababu tu wamezaliwa Waislaam na sii waislaam kiimani..Watu ambao zinaa sii haramu kwao na wamezaa nje mitoto kibao kisha twende kuwanyang'anya mirathi kwa makosa ya baba zao ambao tumeshindwa kufuata maadili ya dini na kukumbatia zinaa kama hatuna dini.. Acheni zinaa au tuwahukumuni nyie kwanza kuzuia matatizo ya mirathi,t na ndoa haramu..

Haya swala la OIC?
M adhani Chadema ilikuwa na sambamba na CUF miaka sita iliyopita wakati swala hili lipo ubaoni..
Binafsi sioni utata hata kidogo, kwani kama Tanzania ni mwanachama wa Commonwealth ya Malkia,hakuna sababu ya kuwazuia Zanzibar ambao hawamtambui Malkia kama sisi bara..

Haya jingine lipi? Maana mimi siyajui yote isipokuwa nayoyasoma ktk magazeti kinyume cha pale naijua chuki ya western world agaist Islam inatokana na manufaa ya interest zao na sii chuki ya kiimani..
Fremaison tactic of rule and concur ni ku create hate within the society na wanapoona interest zao zipo matatani hu create pia brain storm divension kupindua attention ya watu kama vile Loliondo ilivyoondoa mada zote kubwa na kero za wananchi...wao wanasema unaleta tumaini jipya..

Mkandara I concur!

Sometimes we fail to realise ourselves nakujikuta tunadanganywa kama watoto na pipi. I of recent attended a class hapo ndani that prof akawaanaeleza prediction ya matuzi ya energy kuanzia 2010 mpaka 2050. Akaanza kueleza kuhusu what the international community has decided on how to reduce global co2 emission by 50%...Kilicho draw attention yangu ni kuwa aliweka note: kwamba anaposema international community anamaanisha G8 na siyo lile kundi kubwa ambalo wanakuja kutalii na kufanya shopping alafu wakirudi kwao hawafanyi kitu na kuishia kutengeneza poetic policies. Nikiwa mweusi pekee kwenye hilo darasa nilijisikia vibaya lakini nilipofikiria kwa undani nikajikuta nakubaliana naye kwani yuko sahihi. Tulivyoeendelea mbeleni ikaonekana hayo malengo yatafikiwa kama tu China na India (Nchi ambazo zitakuwa zimeendelea sana wakati huo) watakubali kutokutumia big reserve ya coal kwenye economy which according to him ni kikwazo na ukweli hadhani kama watakubali. Ukiwa unameza tu kila kitu utajikuta unajiona kuwa unaonewa lakini pamoja na kuwa pia ukiamua kusema hata sisi tunaweza basi jiulize ni kama China na India wanavuruga formular je na Africa ikiamua kujiendeleza assume wasomi wetu watakubali responsibility na kusaidia economy hao hao wanaotuona hatunazo wataturuhusu tufanye hivyo? So you can see double standrds katika politics iwe ya global au local na ndivyo wanasiasa wanavyoamua kutumia kundi ambalo pengine kwa sababu moja au nyingine watavutika kirahisi kufanikisha agenda za wanasiasa.

I sometimes hate politics lakini kama nita hate bila kufanya kitu then hao politician wasipokuwa moderated wanamchezo wakuwafanya wenzao hamnazo! Dawa ni kupambana nao kisiasa na ki science mpaka wakae kwenye mstari.
 
Mkandara I concur!

Sometimes we fail to realise ourselves nakujikuta tunadanganywa kama watoto na pipi. I of recent attended a class hapo ndani that prof akawaanaeleza prediction ya matuzi ya energy kuanzia 2010 mpaka 2050. Akaanza kueleza kuhusu what the international community has decided on how to reduce global co2 emission by 50%...Kilicho draw attention yangu ni kuwa aliweka note: kwamba anaposema international community anamaanisha G8 na siyo lile kundi kubwa ambalo wanakuja kutalii na kufanya shopping alafu wakirudi kwao hawafanyi kitu na kuishia kutengeneza poetic policies. Nikiwa mweusi pekee kwenye hilo darasa nilijisikia vibaya lakini nilipofikiria kwa undani nikajikuta nakubaliana naye kwani yuko sahihi. Tulivyoeendelea mbeleni ikaonekana hayo malengo yatafikiwa kama tu China na India (Nchi ambazo zitakuwa zimeendelea sana wakati huo) watakubali kutokutumia big reserve ya coal kwenye economy which according to him ni kikwazo na ukweli hadhani kama watakubali. Ukiwa unameza tu kila kitu utajikuta unajiona kuwa unaonewa lakini pamoja na kuwa pia ukiamua kusema hata sisi tunaweza basi jiulize ni kama China na India wanavuruga formular je na Africa ikiamua kujiendeleza assume wasomi wetu watakubali responsibility na kusaidia economy hao hao wanaotuona hatunazo wataturuhusu tufanye hivyo? So you can see double standrds katika politics iwe ya global au local na ndivyo wanasiasa wanavyoamua kutumia kundi ambalo pengine kwa sababu moja au nyingine watavutika kirahisi kufanikisha agenda za wanasiasa.

I sometimes hate politics lakini kama nita hate bila kufanya kitu then hao politician wasipokuwa moderated wanamchezo wakuwafanya wenzao hamnazo! Dawa ni kupambana nao kisiasa na ki science mpaka wakae kwenye mstari.
Hii nimeikubali mwana dah, pamoja daima.
 
Mkuu umeulizwa kero za Waislaam kwa maana kwamba ni kero za kundi moja kati ya wananchi wote..hatuwezi soote kusali msikitini mmoja wewe wakilisha..

Mbunge huwakilisha watu wa jimbo lake bungeni..hakuna mtu alosema serikali au sisi wananchi hatufahamu kero za wananchi wote kwa ujumla wake ila hatujui kero za kila jimbo na priority zao na ndio sababu ya kuwa na wawakilishi wa majimbo.

Sasa wewe waona taabu gani kuwakilisha kero za waislaam ikiwa wewe ni Muislaam na unazijua au kifikra unafikiri Dr Slaa na Chadema hawawezi kuzitatua kwa sababu sio waislaam?..

Mkuu wangu kwa mwendo huu hatuwezi kufika mahala kwa sababu sisi kama Wakerewe kero zetu zinawakilishwa na mbunge wetu,vivyo hivyo majimbo yote huwakilishwa bungeni,sasa mimi sioni tatizo hata kidogo kama Waislaam wanaweza orodhesha kero zao ktk kutafuta haki yao kitaifa.. Si tunasema Tanzania ni yetu wote? Then kuna taabu gani kusema unachotaka?

Nini, Mahakama ya kadhi?
Hili sio jambo rahisi kuwa la kikatiba pasipo referandum ya waislaam wenyewe kupiga kura for or against, kwa sababu hatuwezi kuwalazimisha watu ambao hawafuati dini kwenda mahakamani kwa sababu tu wamezaliwa Waislaam na sii waislaam kiimani..Watu ambao zinaa sii haramu kwao na wamezaa nje mitoto kibao kisha twende kuwanyang'anya mirathi kwa makosa ya baba zao ambao tumeshindwa kufuata maadili ya dini na kukumbatia zinaa kama hatuna dini.. Acheni zinaa au tuwahukumuni nyie kwanza kuzuia matatizo ya mirathi,t na ndoa haramu..

Haya swala la OIC?
M adhani Chadema ilikuwa na sambamba na CUF miaka sita iliyopita wakati swala hili lipo ubaoni..
Binafsi sioni utata hata kidogo, kwani kama Tanzania ni mwanachama wa Commonwealth ya Malkia,hakuna sababu ya kuwazuia Zanzibar ambao hawamtambui Malkia kama sisi bara..

Haya jingine lipi? Maana mimi siyajui yote isipokuwa nayoyasoma ktk magazeti kinyume cha pale naijua chuki ya western world agaist Islam inatokana na manufaa ya interest zao na sii chuki ya kiimani..
Fremaison tactic of rule and concur ni ku create hate within the society na wanapoona interest zao zipo matatani hu create pia brain storm divension kupindua attention ya watu kama vile Loliondo ilivyoondoa mada zote kubwa na kero za wananchi...wao wanasema unaleta tumaini jipya..

Mkandara wewe mara nyingi unapo post baadhi ya maoni yako huwa unajinasibisha na Uislamu na huenda unataka tuhalalishe na kuona kweli unachosema kinaweza kuwa kweli kwa sababu Mkandara mwenye ni Muislamu!
Kwani huwezi kufikisha ujumbe wako bila ya kujiita Muislamu?

Sasa la kushangaza ni kuwa pamoja na Uislamu wako ati hujui kero za Waislamu? unaleta issue za OIC, na Mahakama ya Kandhi! yaani wewe umeona kuwa kero za Uislamu ni OIC na ISlamic court? unaonekana wewe umeishi nje ya nchi muda mrefu sana na kwa kuwa hujaishi TZ huwezi kujua na madhambi waliyofanyiwa Waislamu ndio maana Waislamu hawatasita kudai haki yao:

Kama kweli hujawahi kusikia kero za Waislamu wa nchi hii nakuomba tumia muda wako usome nyaraka na vitabu vifuatavyo:
1) Barua ya Halmashauri kuu ya Waislamu kwa Rais Mkapa
2) Mwembechai Killings
2) Waraka wa Aziz
3) Barua kwa Wabunge

Kwa ufupi mkuu, Waislamu kama WaTZ wengine wanaathirika na hali ngumu ya uchumi inayoikabili TZ leo na madhambi yote ya Kifisadi, rushwa nk. sio kwama Waislamu haiwaathiri kama baadhi ya watu hapa JF wanataka kutuaminisha! bali kila shida inayompata MTZ wa leo na Muislamu hawezi kuiepuka!

Ila mbali na matatizo ya kiuchumi na kijamii Waislamu wameathirika sana na Maamuzi ya Serikali za Awamu zote hasa hasa ni Uvunjaji wa makusudi wa Katiba yetu juu ya haki ya Waislamu ya kuabudu!!!
Kipengele hiki cha katiba kinachoainisha waziwazi haki ya kila mwananchi kuabudu bila kuvunja sheria, na imedhihirika kuwa kifungu hicho cha sheria kinawahusu Dini zingine lakini sio Waislamu! ukitaka kujua ni vipi soma vitabu hapo juu!

Muislamu safi yuko tayari kufa njaa kuliko kukosa haki yake ya kuabudu!!
 
Kwa ufupi mkuu, Waislamu kama WaTZ wengine wanaathirika na hali ngumu ya uchumi inayoikabili TZ leo na madhambi yote ya Kifisadi, rushwa nk. sio kwama Waislamu haiwaathiri kama baadhi ya watu hapa JF wanataka kutuaminisha! bali kila shida inayompata MTZ wa leo na Muislamu hawezi kuiepuka!

Huyu Muislamu si Mtanzania? Kama shida inampata Mtanzania ina maana inampata Muislamu vile vile sivyo? Labda itabidi nirejee mfano wa seti Kama kwenye seti kubwa ya "Watanzania" Wamo "Waislamu, Wakristu, Wahindu, Wapagan, Wasioamini) basi Seti ya "Muislamu" inahusissha Mtanzania vile vile na seti ya Mkristu inahusisha Mtanzania vile vile. Hivyo, ukizungumzia matatizo ya seti ya Tanzania unazungumzia matatizo ya wote waliomo kwenye seti hiyo.

Sasa kwenye seti ndogo ya Wakristu, Waislamu utaona kuwa namo kuna seti ndogondogo; kwa mfano kwa Waislamu kuna "Shia, Sunni, Suffi, Ahmadiya, n.k) Hivyo kwa kadiri unavyozidi kuzigawa seti utaona ni jinsi gani zinavyozidi kuwa specific.

Ila mbali na matatizo ya kiuchumi na kijamii Waislamu wameathirika sana na Maamuzi ya Serikali za Awamu zote hasa hasa ni Uvunjaji wa makusudi wa Katiba yetu juu ya haki ya Waislamu ya kuabudu!!!

Serikali za "awamu zote" zilikuwa ni serikali za chama kile kile, chenye sera na itikadi ileile. Yaani, Chama cha Mapinduzi.

Kipengele hiki cha katiba kinachoainisha waziwazi haki ya kila mwananchi kuabudu bila kuvunja sheria, na imedhihirika kuwa kifungu hicho cha sheria kinawahusu Dini zingine lakini sio Waislamu! ukitaka kujua ni vipi soma vitabu hapo juu!

Muislamu safi yuko tayari kufa njaa kuliko kukosa haki yake ya kuabudu!!

Sasa, hapa ndio nadhani kuna tatizo (na nilijadiliana sana Mohammed Said kwenye hili) Muislamu "safi" Tanzania ni yupi? Maana Muislamu asiyekubaliana na tafsiri fulani au msimamo fulani wa kidini anaonekana kama siyo "safi" na hivyo hata wale ambao wana mawazo tofauti kwa mfano kwenye suala la Kadhi au OIC wanaonekana kama siyo wazuri. Unaweza kufikiria kuwa Waislamu wote duniani (kama walivyo Wakristu) hukubaliana kwa kila kitu the theolojia au imani.

Ndio maana yawezekana wapo Waislamu wanaounga mkono CCM kwa sababu labda hawaamini kuwa kuna madai makubwa hivyo ya kuwafanya wasikiunge mkono. Na wapo wengine ambao kwa hakika huwezi kuwaambbia chochote kuhusu CCM hata kama inaongozwa na Muislamu. Wao wanaamini kuwa kuna tatizo kubwa la kimfumo ambalo limetengenezwa na CCM na hivyo CCM yenyewe haiwezi kulisahihisha na hivyo bora kutafuta njia mbadala ya kutatua tatizo hilo.

Ndio maana msingi mkubwa wa swali letu hapa ni kuwa yawezekana kweli CCM (kama chama kilichotengeneza mfumo wetu wa utawala) kimebadilika kiasi cha kuwa rafiki wa kila Muislamu hasa kama tumeaminishwa huko nyuma kuwa ndicho kilikuwa chanzo cha matatizo na dhulma dhidi ya makundi kadhaa ya Waislamu?

Jawabu ambalo ningelitarajia kwako (labda na wengine vilevile) ni kuwa Wapo Waislamu ambao hawaungi mkono CCM si kwa sababu haijashughulikia matatizo ya Waislamu tu bali kwa sababu ni chanzo na sababu ya matatizo mengi ambayo tunayo kama taifa. Matatizo ambayo hayawezi kuondolewa isipokuwa kwa kubadilisha kabisa chama kilichoko madarakani.
 
Mtu ni mazingira yaliyomzunguka ikiwa na pamoja na chakula na malezi, haya yote tunayokutana nayo ni mwanzo wa ukombozi wa kweli kama ikiwa tutavuta kamba mara dufu au anguko la milele kama ikiwa tutaregea kama mlenda, wenzetu wanaamini binadamu wote ni sawa wakati wakuzaliwa lakini wanaanza kuweka gap katika hali ya maisha, akili na mwili kadri mazingira yanavyo wa-mould.

Samahani sana kama kuna mtu nitamkwaza, ila naomba kuchangia zaidi kutoka na tafiti za kiingereza nilizo waikuzisoma na kushangaa kama ifutavyo: -

  • Kwanini CUF walipo kimbia Zanzibar baada ya kufanya vurugu walikimbilia Uingereza badala ya Mashariki ya kati/mbali kama ambavyo mtu mwenye akili timamu angetegemea iwe! na wengi wapo hadi leo wanaishi raha mstarehe bila shaka, lakini tukiwa nyumbani tuna nadi ubaguzi wa rangi na dini kila kukicha? Huu ni ushahidi wa tafiti zilizofanywa na uingereza katika karne ya 13, 14 na 15. Pia ina uhusiano na swala la Muungano pia.

  • Waingereza na Marekani urafiki wao mkubwa ni katika Elimu na kujenga uchumi kwa kushirikia bila ubaguzi, kwa kweli naweza kusema pamoja na kutawala sehemu kubwa ya dunia kikoloni Waingereza wanaamini katika umoja na uhuru wa kuishi katika nchni yoyote unayotaka ili mradi unafuata sheria, nadhani kama ingekuwa ni rai yao Dunia yote ingekuwa mahali pa kuishi kwa kila binadamu bila ubaguzi wa rangi yake na dini yake, kwa kuamini katika hili wao waliwekeza katika tafiti nyingi za tabia za binadamu na uwezo wao kutokana na mazingira na maeneo wanayoishi huku ndugu zao USA wakiwa wamekita katika tafiti za technologia na maendeleo . Wamerikani hawakuathiriwa sana na vita vya dunia hivyo rafikie na ndugu uingereza ilimpa siri ya mafanmikio, ya wapi walipo binadamu wenye ubongo na utashi mkubwa wakuweza kuweka katika ubongo wa binadamu. Hivyo Marekani ikawa kinara wa tafiti hizo tokea zamani ingawa wao hiyo bado ni siri kwao mpaka leo. vitu vingi vinavyooneka kama kwamba vinavumbuliwa leo inasemekana wezetu tayari wanayo majibu siku nyingi wanatumia kulingana na mahitaji ya wakati husika. Japani pekee ndio iliyoonja ladha ya tafiti za US baada ya vita ya dunia na US kuamua kuisaidia Japani ilikuziba pengo lililo tokana na vita vivyo japani ikapaa juu sana watu wengi mapaka leo hawajui kuwa hile ilikuwa ni kazi ya kalatasi waliyopewa tayari kuiweka katika vitendo kutoka katika nadharia. Ukweli ni kuwa huwezi kuendelea bila tafiti sahihi za maendeleo, ingawa sisi tunaamini unawe kuendea kwa kumsikiliza Mgonjwa mmoja kutoka CCM ambaye anashida mara mia zaidi yetu eti ajenge nchni yetu!

  • Katika Tanzania na Dunia nzima Tafiti zinaonyesha Waislaam ni Volatile material, handle with care; huu ndio ukweli na kama nilivyo nilivyoainasha hapo juu mazingira na malezi yetu yanatufanya tuwe volatile. Samani sana ndugu zangu kusema hili; Sisi ni volatile. wepesi kuwaka wepesi kuchukuliwa na upepo, mtu yeyote anayetunza petrol lazima hajue masharti na safety means za kupambamba na moto muda wowote.

  • Kikwete ndiye aliye leta haya yote kwasababu alijua petrol ilipo ni kutia moto itawaka bila shaka, ila ninavyojua mimi lazima ameshaulizwa ndio maana anaangaika kila siku na hofu tele maana wenye tafiti zao wanajua kuwa volatile material lazima idhibitiwe ili kuleta amani Dunia kote, tayari Qadhafi lazima ataondoka tu ni volatile material anaweza kuwaka moto kama petrol ikaleta janga.

  • Compromise tunayotaka sisi waislaam haipo na haitatokea millele dunia. tunapenda kunyiwa mambo ambayo sisi binafsi hatuwezi na hatutaki kuwafanyia wenzetu. Kikwete ashukuru sana Slaa hana tabia kama ya Maalimu maana angelikuwa na tabia hiyo na akaamua kwenda kuelezea mambo yaliopo humu nchni dunia nzima kuwa huyu Jamaa anaeneza udini na mambo ya Al-shababi nawaambie kikwete hasinge fika hata miezi miwili, angeondoka mara moja. Ila Time will tell tutaona mwisho wake na huu ubaguzi anaotaka kuwaachni watanzania labda kama ameshajua kuwa soon anaondoka kwenda Jehaam, lakini kama atabaki humu nchni yote haya yatamtesa sana kabla hajaingia kaburini maana anafanya kwa makusudi.
 
Mkandara wewe mara nyingi unapo post baadhi ya maoni yako huwa unajinasibisha na Uislamu na huenda unataka tuhalalishe na kuona kweli unachosema kinaweza kuwa kweli kwa sababu Mkandara mwenye ni Muislamu!Kwani huwezi kufikisha ujumbe wako bila ya kujiita Muislamu?:

Kadogoo, usiwe unasoma maandishi kwa kuangalia nani ni mtu wa aina gani,zama katika maudhui(contents).'Prejudice' inapunguza uwezo wa kutafakari.
Mkandara anatoa maoni kwa muono wake si lazima yaegemee imani yake, ukomavu wa kufikiri ni pamoja na kukubali kukosoa au kukosolewa. Maoni yake hayabadilishi au kupunguza imani yake bali yanamjenga kuwa mtu huru mwenye fikra huru asiyesubiri mtu mwingine afikirie au aandike kwa niaba yake.

Kadogoo;Kama kweli hujawahi kusikia kero za Waislamu wa nchi hii nakuomba tumia muda wako usome nyaraka na vitabu vifuatavyo: 1) [URL="http://www.igs.net/~kassim/nyaraka/barua_halmashauri.htm" said:
Barua ya Halmashauri kuu ya Waislamu kwa Rais Mkapa[/URL]
2) Mwembechai Killings
2) Waraka wa Aziz
3) Barua kwa Wabunge

Waislamu wameathirika sana na Maamuzi ya Serikali za Awamu zote hasa hasa ni Uvunjaji wa makusudi wa Katiba yetu juu ya haki ya Waislamu ya kuabudu!!! kujua ni vipi soma vitabu hapo juu!

Muislamu safi yuko tayari kufa njaa kuliko kukosa haki yake ya kuabudu!!

Kwa sentensi yako ya mwisho, sioni kwanini wakati wa kudai haki mtu afe na njaa! hata vitani watu wanakula sembuse linaloweza kujadiliwa. Sijui muislam safi ni yupi! Kwa ufahamu wangu kidogo sana, mwenye siri ya uislam wa mja ni Mwenyezi Mungu (S.W.T). Je anayetofautiana na wenzake kimtazamo anakuwa si safi! na hawa wanakuwa kundi gani wanaoamini au wasioamini?

Kuhusu vitabu na maandiko uliyoweka hapo juu, kwasababu umeyasoma ukiwa na 'mwelekeo tayari' umekosa faida ya uchambuzi,hayo ni maoni wewe unapaswa kuyaelewa na kutafakari.
Katika mjadala na M.Said, ilisemwa kusoma ni jambo moja, kuelewa na kutafakari ni mambo tofauti.
Maandiko ya hapo juu yanaonyesha kuwa hakuna 'mfumo' mmoja wa kushughulikia matatizo ya waislam ndio maana suala moja limerudiwa mara 3 na watu au taasisi tofauti. Jiulize baraza la halmashauri ni lipi! la Bakwata? na kama siyo ilipewa mamlaka hayo na nani?

La muhimu zaidi ni kuwa maandiko unayotaka tuyasome, ndiyo hasa kiini cha swali la MMKJ. Je kadhia zote hizo zimepata ufumbuzi? kama hapana, hiyo CCM iliyoleta kadhia zote hizo imegeukaje kuwa rafiki wa wale wale waliodhulumiwa leo?

Kwa vile umesoma ukiamini tu bila kutafakari sasa unaji 'contradict'.
 
Bila kuuma maneno waislam wanaisupport ccm kwa sababu ya uislam wa Jk. Baada ya kura za maoni ccm urais 2015 utaona watakavyo rudi cuf kwa speed. Jaribuni kusoma matamko yao mwone, ukiyasoma kwa makini wanasema uonevu waliowahi kuupata na kudhulumiwa haki yametoke wakati wa mwl K. Nyerere na utawala wa Mkapa na walivyo na dhalau na jaziba wanadhiliki kuwaita Mkapa na Nyerere kuwa ni mapadre, . Lakini enzi za Jakaya wanataja waziri fulani mkristu alivyowahi kuwabania. Utaona ni dhahiri kabisa waislam anapotawala mwenzao weakness zake wanavunga hawazioni wanasubili achagulie mkristu waanze kulaum. Na mimi nawashauri wafight miaka hii minne iliyobaki wapate haki zao kama mahakama ya kadhi,kujiunga jumuiya ya kiislam na madai mengine ili akiingia mkristu wasilete kisingizio. Na wanajua fika lazima ajae awe mkristu wamtumie Jk ambaye wanamsupport kutimiza adhima yao hata sisi tumechoka kutishwa.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom