Well food of thought! Tulipofika sasa mwana siasa akianza kusema mambo ya umoja na mshikamano unamuangalia kama yuko serious maana wao wenyewe, wakidhani hawaonekani wanayoyafanya, wamesaliti huo umoja na mshikamano kwa kuwa tayari, kuiuza nchi kwa watu wasio wazalendo na wala rushwa wakubwa.
Imefika mahali sasa lazima tutofautiane katika fikra. Naamini sio watu wote wanaonufaika na upuuzi huu ambao wanasiasa wanaufanya. Kama spark ya mabadiliko ya kweli ikionekana, tutashuhudia jinsi watu wachache wanaoamini kuwa wanauwezo wa kututawala wote kwa hila hila watwkavyoshika vichwa kwa kushuhudia kushindwa kwao.
Tunaposhindwa sasa ni sehemu moja...bado hatuna chama wala wanasiasa wenye agenda serious ya kututoa huku kwenye shimo ambalo hawa wajanja wachache wametutumbukiza.Hawapo, na hata kwenye vyama vya upinzani pia hawapo!Kama wapo basi ni tone moja la maji ndani ya bahari.
Je amani na utulivu utakuja wakati mwenzio ana Bilioni 1.3 katika account wewe huna hata 200 katika account?. Je umoja utakuwapo wakati kipato cha aliyenacho na asiyenacho kipo katika kiwango cha kutisha!!! Je umoja utakuwapo wakati the society is a lawless society. Je amani na utulivu itakuwapo wakati serikali ni unjust na haki anapewa yule asiyedeserve.
Marekani tunayoiimba sasa hivi haikuja hivi hivi bali ilipitia misukosuko na mitikiso mikubwa. St Augustine aliwahi sema kuwa an unjust law is similar to no law. That is why unakuta watu ni mafisadi but wanaitwa watukufu na waadilifu wengine wanawaita hata wanaume wa shoka!!!! Kimsingi nakubaliana na MM but swali langu je tufanye nini ili haki ipatikane. Serikali ishukuru mmungu watanzania ni waoga (mabingwa wa kusema tu) ingelikuwa Kenya au Uganda ingelikuwa stori nyengine. But waswahili wana msemo wao kuwa mwenye njaa hugeuka kuwa mnyama wakati fulani. Kimsingi mabadilko ya chama mbadala yanatakikana maana CCM si chama cha wanyonge tena!!!!