Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Bila Kamanda Kamuhanda kusimamishwa kazi na kuunganishwa katika kesi ya mauaji ya Daud Mwangosi hatua yoyote dhidi ya askari waliokuwa chini yake itakuwa ni ya uonevu. Na yeye apandishwe kizimbani kama mshirika wa mauaji. Ni mtu pekee aliyekuwepo eneo la tukio ambaye angeweza kuzuia mauaji lakini hakufanya hivyo.
Alitakiwa awe na yeye amesimamishwa kazi na kutokuwa sehemu ya uchunguzi wa polisi isipokuwa kama mtuhumiwa na mshukiwa wa mauaji ya Mwangosi. Kutomshtaki au kujaribu kutengeneza mashtaka nje ya yale yanayowakabili askari waliokuwa chini yake.
Naweza hata kwenda mbali zaidi - mtu pekee ambaye anatakiwa awe wa kwanza kutiwa pingu na kushtakiwa kijeshi kwanza ni Kamanda Kamuhanda. Avuliwe kwanza vyeo vyake vyote halafu atiwe pingu kusimamishwa katika mahakama ya kiraia...
Alitakiwa awe na yeye amesimamishwa kazi na kutokuwa sehemu ya uchunguzi wa polisi isipokuwa kama mtuhumiwa na mshukiwa wa mauaji ya Mwangosi. Kutomshtaki au kujaribu kutengeneza mashtaka nje ya yale yanayowakabili askari waliokuwa chini yake.
Naweza hata kwenda mbali zaidi - mtu pekee ambaye anatakiwa awe wa kwanza kutiwa pingu na kushtakiwa kijeshi kwanza ni Kamanda Kamuhanda. Avuliwe kwanza vyeo vyake vyote halafu atiwe pingu kusimamishwa katika mahakama ya kiraia...