Ni kweli viongozi wetu wengi ni wagonjwa?

Dah mkuu FM ES,

Maneno makubwa haya, hii ni 2009 maneno hayo yalitamkwa 2006 ....je, tunaweza kupata update ya mambo yalivyo sasa!...angalia hapo kny bold!


ARVs zimesaidia mkuu. Hao waliokuwa watarajiwa sasa wamenona kama tembo!!!! Wanasubiri tu kuanguka ghafla tuambiwe ni shinikizo la damu. Do we know that ARVs are silent killers???!! Ukiziwahi hutakufa kwa sumbufu wa magonjwa nyemelezi!!!! unaugua ghafla na kufa ghafla!!!
 
Ukimwi unauwa na hauna dawa. Nchi zilizo kusini mwa jangwa la sahara Tanzania mojawapo ndizo zinazoongoza kwa maambukizo na vifo vya gonjwa hili. Mwenye ugonjwa huu anakuwa na hawezi tena kutoa maamuzi yaliyotulia, hutawaliwa na hasira na maamuzi angamizi.

ni kweli sio vizuri kuwatenga, ila wenye fedha wakiwanao wanatabia ya kuwagawia masikini. sasa kama wabunge wanao na nina amini ni zaidi ya kumi ama thelathini au zaidi kwani kule dodoma ndiko jikoni wakati wa vikao kama sasa unaona hapa wapo akina dada kibao wametokea sehemu mbali mbali hasa dar je ni wabunge au lobbyist no ni wakina nani sote tumekodoa macho tunajiuliza, ila kiza kikizama wote wanawashikaji na washikaji ni wabunge ambao wameacha wake na wototo majimboni mwao.

Scenerio nyingine ni wabunge wanawake huwa wanajipatia kata kiu kwa wabunge wenzao au wanaendeleza libeneke kwa ajili ama ya kusaidiwa kurudi bungeni au kukeep status, nao wakirudi makwao wanawaume zao kazi kwenda mbele. kama kumi umehakikisha wanao baada ya miaka mitanao kila mmoja akiambukiza mmoja na kila aliyeambukizwa akimuambukiza mwenzi wake na mwenzi akimuambukiza chori wake do maths.

Elimu ya ukimwi na wenye uelewa waelewe huu ugonjwa ni hatari, na unadhoofisha sio tu uchumi bali hata kutesa familia husika. Waliobahatika kupata elimu ya darasani hasa wabunge na wanafunzi, lawyers nk wangekuwa mstari wa mbele kuelimisha jamii sio tu kwamba ugonjwa huu unauwa bali ni kuiachia jamii yako msiba mkubwa na mateso. Inafaa kabla na baada ya bunge kuwe na kama saa zima la madhara ya ukimwi kwa wabunge na ionyeshwe nchi nzima, lazima waonyeshe mazingira ya hapa dodoma na jinsi yanavyoweza kubadili mwelekeo wa mmbunge na mwananchi kwa maamuzi yake anapokuwa dodoma. Waelezwe wazi kuwa wao ni kioo cha jamii na mbunge bila ukimwi inawezekana na mwananchi vilevile, kwani yanayofanyika hapa ni aibu.

nimeshuhudia vifo vingi vya watu maarufu na amabao wanahitajika sana kwenye jamii kama madaktari, lawyers na waalimu muhimu wameondolewa mapema na gonjwa hili. Vilevile linaongoza mzigo mkubwa sana kwenye bajeti ya nchi. na Tanzania ndio nchi ya ajabu kwani wenye uelewa na elimu na uwezo ndio wanakufa sana. wakati umefika tutangaze ugonjwa unao uwa ili kujua jinsi ya kujiepusha nao badala ya kubatiza magonjwa yasiyohusika kwa marehemu.

Tusaidiena kuangamiza UKIMWI, UNAUWA, NI HATARI NA HAUNA KINGA WALA DAWA.
 
Nafikiri ni wakati wa kuweka kipengele kwenye maadili ya viongozi kuwa mwenye ugonjwa wa kuambukiza na akaambukiza kwa kusudi atashitakiwa kwa misingi ya sheria.

sheria kama hizo zikiwepo japo kuwa zinaweza kuwa katika upana wake zisitumike, lakini japo mtu mmoja tu akitokea kushitakiwa kwa hilo, wengine wanaweza kupunguza.

kama hatuwezi kulindwa na viongozi wetu, kuna faida gani ya uwepo wao?
 
hapa kuna weza kuwa na ukweli!

Inasemekana ukiwa mgonjwa hata maamuzi yako yanaweza kuwa mabaya. Akili haitulii! na baadhi yao labda wanahusika katika kufanya maamuzi ya hovyo hovyo tu katika mikataba ya taifa letu!

Maana mikataba na deal nyingine kwa kweli zinatia kichefuchefu labda ni wagonjwa wanaotuamulia na kutia sahihi!

Ninasema kuna haja ya kufikiria mara mbili! labda wagonjwa wanaojulikana wasihusishwe katika maauzi mazito ambayo madhara yake yanakuja baadaye!


Ndugu nakuunga mkono asilimia mia..!!

Hapa panatia shaka sana..!! ukisha jua kesho kutwa unakufa..hivi kweli utakuwa na uchungu wa kumsaidia yule atakaebaki ? Ndio...kwa wachache sana na si VIONGOZI WA KITANZANIA.

Kawa wanaweza kuwanyanganya mali waziwazi maskini wa kitanzania wata shindwa kweli kusaini bomu la nyuklia kulipuliwa Tanzania ?

Je ji ulize kama mbuge anaweza kwenda nyanganya ardhi safi yenye rutuba ya wananchi na kulazimisha wananchi hao wahamishiwe ktk maeneo ambayo ni Malaria epidemic. Kweli tuna kwenda wapi na hawa watu..!

Nilipata tetesi kwamba hata baba yetu wa sasa nae ana maambukizi ya vvu..!

Kazi kweli kweli.
 
This thread is inappropriate (OK, thats's just a politically correct euphimism for a toned down wrong) on so many levels.

1. Matters of health, especially to already elected officials, are to be private among civilized societies, unless the person afflicted deem it necessary not to make these very matters private.

2. Addressing these health issues in isolation from addressing the very same issues in the general population can be said to be harboring discrimination, favoritism or political machinations.

3. Elected officials are a mirror of our society.To object or discuss in any way that can be interpreted as objecting MPs with HIV is in a way denying representation in the parliament for HIV + Tanzanians. We do have an albino MP, I have not heard anyone raising the spectre of that condition incapacitating even mildly the MP. Are we really concerned about these MP's performance or is this insinuation merely masking the stigma that HIV/AIDS has acquired in our society? If we are concerned about performance is this the most pressing issue regarding MPs performance? How come I did not hear about Bujiku Sakila when he was terminally ill?

4. I gather small-mindedness on the part of some of us will never allow us to consider that the infection of HIV is not a death sentence, and may allow the infected to fully contribute to society.What if we reach HIV levels of Botswana and Swaziland, would we write off a quarter of our population just to satisfy our holier than thou attitudes?

5. Before pointing fingers at the MPs, have we checked ourselves? Are we completely positive that our behaviors are tantanimous with an HIV free society? Have we ensured that all the uncommon means of transmission cannot infect us? Are we imposing standards we cannot keep up with?
 
UKIMWI ni changamoto kubwa pengine kuliko zote zilizowahi kumpata mwanadamu:
Hauchagui msomi, asiyesoma,tajiri, maskini, kijana, mzee, kiongozi, mfuasi, mwanamke,mwanaume,mrembo,.......listi inaweza kuwa ndefu unavyoweza kufikiria.Kwasasa uelewa kwa kiasi kikubwa upo wa kutosha hasa mijini, na cha ajabu wale wale waelewa ndiyo wenye kufanya uzembe zaidi kwenye kupuuza kutumia kinga.Humu humu JF kuna watu bado wanazungumza kuuza mechi kisa kaona mwanamke mzuri kupindukia, kuna wenye kutafuta ushauri baada ya kuwapa ujauzito wanawake ( girlfriend, housegirl)..hii inatuambia nini?
Kuna kitu kinasemwa kuwa ni kukosekana kwa ile nia ya kubadili tabia....mtu pamoja na uelewa bado anakuwa mgumu ama kuacha kujamiiana kizembe, kuwa mwaminifu,n.k
Mkizungumzia viongozi - nao wako kwenye kundi la wasiotaka kubadili tabia.... hata ije sheria, tamko, vitisho...haitasaidia kama watu hawabadiliki.
 
Bado niko palepale, viongozi ni kioo cha jamii, wametoka katika jamii hii hii, hawajatoka mwezini!
 
UKIMWI ni changamoto kubwa pengine kuliko zote zilizowahi kumpata mwanadamu:
Hauchagui msomi, asiyesoma,tajiri, maskini, kijana, mzee, kiongozi, mfuasi, mwanamke,mwanaume,mrembo,.......listi inaweza kuwa ndefu unavyoweza kufikiria.Kwasasa uelewa kwa kiasi kikubwa upo wa kutosha hasa mijini, na cha ajabu wale wale waelewa ndiyo wenye kufanya uzembe zaidi kwenye kupuuza kutumia kinga.Humu humu JF kuna watu bado wanazungumza kuuza mechi kisa kaona mwanamke mzuri kupindukia, kuna wenye kutafuta ushauri baada ya kuwapa ujauzito wanawake ( girlfriend, housegirl)..hii inatuambia nini?
Kuna kitu kinasemwa kuwa ni kukosekana kwa ile nia ya kubadili tabia....mtu pamoja na uelewa bado anakuwa mgumu ama kuacha kujamiiana kizembe, kuwa mwaminifu,n.k
Mkizungumzia viongozi - nao wako kwenye kundi la wasiotaka kubadili tabia.... hata ije sheria, tamko, vitisho...haitasaidia kama watu hawabadiliki.

WOS,Kauli kwamba UKIMWI hauchagui sijui tajiri masikini etc zimeshazoeleka,lakini ni kauli tu za waafrika za kufarijiana nk.
Ukweli ni kwamba hakuna jambo ambalo mwanadamu hulifanya kwa kasi ama mara nyingi wakati hawana kazi ama la kufanya kama ngono....Mara nyingi watu waliko bored huishia kufanya ngono,hilo liko wazi....Na ndio maana nchi masikini zimeathirika zaidi,hilo ni mbali na elimu ya namna ya kujikinga,elimu ambayo ofcourse inatolewa mara nyingi maeneo yenye watu ambao shughuli za kichumi zipo na zinaendelea kuwa keep wananchi hao busy.

Sasa ukiangalia kutokana na mada hii,inawezekana viongozi wetu wako soo bored na kazi yao ni kulala na ngono,tumeshaona wazi kwenye vikao muhimu vya bunge kama bajeti nk.

Kwa upande wa masikini,ni the same,hawana kazi na huishia kwenye mambo kama ulevi,utumiaji wa madawa ya kulevya na above all...Ngono.
Mfano uliotoa ni mzuri kuhusu watu wenye uelewa especially kwenye nchi kama TZ,yes viongozi na wanataaluma ndo wene kuikwaa miwaya ukiachilia mbali umasikini,hilo ni tofauti na nchi zilizoendelea ambapo masikini ndio wanaukwaa zaidi ya viongozi nk.

Hata hivyo hushangazwi na madaktari ambao nao wako well knowledgable kuhusu madhara ya sigara na pombe lakini wengi wao ndio wa kwanza ku abuse alcohol na ndo watumiaji wakubwa wa fegi?

La kujifunza hapa ni kwamba kama mtu ameshindwa kujitake care,then ni kivipi apewe majukumu ya kuwacare wananchi?

Je inawezekana kutokujali kwa viongozi hao kunasababishwa ukweli kuwa wanajuwa kuwa ni waathirika na hivyo kufanya maamuzi yasiyozingatia hasara na faida za vizazi vijavyo...Nadhani hii ni changamoto.
 
Ukija kwenye swala la ukimwi pia, ni maoni yangu kuwa, socia economic factors play a much bigger role than scientist have recently acknowledged. Si kweli kwamba sisi wa Afrika ni wajinga zaidi ya nchi zingine ndio maana tunaendelea kula ngono bila kujali na kupata huu ugonjwa, na wala si kwamba sisi ni wapenda ngono kuliko mataifa mengine, HAPANA! Ila the social economical state of our countries plays almost as large a role as the virus itself!
Ndio tunaambiwa ukimwi hauchagui tajiri wala maskini but this is on an individual basis (naomba nibadilishe stesheni) on a larger scale the rate of disease spread does depend on the social standing of that society at large. Advantages not only rest on the improved immune system as a result of good diet (a subject at which I could hand you numerous studies of cases that have shown individuals not contracting AIDS despite having intercourse with an infected partner) but also affect the mental state of the people in a community.
Ni miaka karibu miwili tangu thread hii muhimu kuanzishwa hapa JF. Ila ni lazima nikubali kuwa katika thread hii nimejifunza kitu muhimu sana na kujihakikishia ukweli wa baadhi ya niliyokuwa nikiyaamini tangu awali.

Nyamgluu ameweka points muhimu sana kuhusiana na sababu zisizotanjwa ambazo zinachangia katika kuongezeka kwa maambukizi ya VVU katika jamii yetu. Badala yake, watu wengi hudhani ujinga peke yake ndiyo sababu kubwa inayopelekea maambikzi haya.

Ni kweli kabisa kuwa maisha tunayoishi ni moja ya vigezo vinavyosababisha maambukizi haya kuwa vigumu kuyaepuka ama kuyapunguza kama tunavyotamani.

Asilimia kubwa sana ya watu Afrika na hasa Tanzania wanaishi katika squarters mijini na vijijini. Ninaamini sana kuwa katika maeneo ambayo watu huishi wengi, kwa pamoja na/au katika hali duni, maambukizi ya UKIMWI huwa makubwa zaidi. Maana wazazi pia hushindwa kuhakikisha watoto wao wako salama muda wote. Ubakaji, ufuska huongezeka sana kwenye makazi ya namna hiyo. Vitisho hutumika sana kufanya wazazi na wanaofikwa na majanga ya ubakaji na/au kulawitiwa kubaki kimya kwa kuhofia maisha yao. Ni katika mazingira kama hayo pia watoto na vijana wengi hujiingiza katika uvutaji bangi, madawa ya kulevya, ufuska, ujambazi, wizi na uhalifu wa kila namna.

Inabidi ufike wakati serikali ishirikiane na wananchi kuhakikisha inapunguza makazi ya namna hiyo ili kuweka ustawi bora zaidi kwa watu wake, kupunguza maambukizi ya UKIMWI na kurahisisha huduma mbalimbali za jamii.

Sehemu nyingine ambapo naamini pia kuwa maambukizi mengi hutokea ni kwenye ma-Bar, na sehemu nyingine kama hizo. Kuna msemo kuwa, mwanaume anapofika Bar, huwaona ma-Barmaid wote ni watu wa kawaida na duni. Baada ya kunywa beer chache, huanza kuwaona kuwa ni watu wazuri tu. Kadiri anavyoendelea kunywa, huwaona kuwa ni wazuri zaidi na inafikia kupania kuondoka nao atakapotaka kuondoka. Bar nyingi huwa hawalipi wahudumu wake ujira mzuri na nyingine huwa hawawalipi kabisa. Hivyo wahudumu huponea kwenye mabaki ya pesa za wateja (kwa kukata panga), au kutegemea wateja wawape pesa kwa makubaliano ya ngono. Mara nyingine, wahudumu hao hujipendekeza kiasi kwamba mteja huona kabisa kuwa nia ya mhudumu ni kutoka nae. Hii ni balaa ambayo inabidi jamii na serikali iweke utaratibu wa kuikabili.

Vile vile kuna guest houses nyingi sana ambazo hutumika zaidi kwa ngono kuliko hata kulaza wageni kama zilivyokusudiwa. Nyingi ya guest houses hizo hutoza pesa ndogo sana kwa wateja wao na hivyo kuwavutia kuzitumia zaidi kila wanapopata nafasi ya kufanya ngono. Urahisi huu wa sehemu za kufanyia ngono, ni sababu nyingine ya uenezwaji wa UKIMWI kwa urahisi zaidi. Katika guest houses hizo, inatakiwa wateja watakiwe kujiandikisha majina yao, sehemu wanazotoka, wanazokwenda n.k. Ili utaratibu huu uwe na maana, inabidi sasa wateja watakiwe kuonyesha uthibitisho kuwa kweli jina aliloliandika kwenye daftari la wageni ni sahihi (kwa kuonyesha kitambulisho kinachokubalika). Hii haifanyiki hivyo, na wengi wa wateja hudanganya majina yao. Ikifanyika inavyotakiwa, watu wenye nia ya kutumia guest houses/ hotel hizo kwa makusudi ya ngono wangesita au kupata tabu ya kufanya ngono kwa urahisi na inawezekana wakashindwa kutimiza haja yao hiyo.

Kwenye nchi kama China, mtu akienda hotelini kwa nia ya kulala na akiwa ameongozana na mtu wa jinsia tofauti kwa lengo la kulala nae, atatakiwa kuthibitisha kuwa mtu huyo aliekwenda nae ni mke/mume wake, kwa vielelezo. Nadhani utaratibu huo ni mzuri kufuatwa na nchi kama zetu, ili kupunguza ngono mahotelini na kwenye guest house.

Kwa kumalizia, nadhani urahisi wa kupata faragha za kufanya ngono nchini ni sababu kubwa sana ya maambukizi ya HIV/AIDS nchini. inabidi kuwe na utaratibu ngumu zaidi ya kuweza kufanikisha upatikanaji na utekelezaji wa ngono ili kuhakikisha usalama wa watu wetu (walau kwa kiasi kikubwa). Elimu ya UKIMWI peke yake haitoshi. Imeshatolewa sana na maambukizi yanaongezeka kila kukicha. Kondom zinagawiwa lakini hazitumiki inavyopasa na sidhani kama zinasaidia sana kuzuia UKIMWI.

Ukimwi unatakiwa uchukuliwe kama janga la Taifa,
umeua wengi, unaua wengi sana na utaua wengi zaidi ukiachiwa kutekelezwa kwa uhuru kama sasa.
 
La kujifunza hapa ni kwamba kama mtu ameshindwa kujitake care,then ni kivipi apewe majukumu ya kuwacare wananchi?

Je inawezekana kutokujali kwa viongozi hao kunasababishwa ukweli kuwa wanajuwa kuwa ni waathirika na hivyo kufanya maamuzi yasiyozingatia hasara na faida za vizazi vijavyo...Nadhani hii ni changamoto.
Mkuu jmushi, ulichosema katika post yako ni sahihi kabisa. Ningependa kujibu tu kwa kiasi maswali yako uliyouliza hapo juu.

Kiongozi ambae anajua kuwa ameathirika na anajua pia kuwa asipoweza kuwa na pesa nyingi afya yake itaharibika na kupoteza maisha haraka atafanya kila hila ili aweze kujilimbikizia mali na ndio sababu kubwa ya Ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka, wizi wa mali ya umma n.k. Mtu huyo hana la kuhofia zaidi ya kuogopa kifo anachoona kinamkaribia. Ukimwi ukimshika mtu kisawasawa, unamfanya wakati mwingine arukwe na akili, apoteze ustaarabu na mara nyingi kuwa mbinafsi.
 
Me nadhani suala la kujadili afya za watu halina mantiki sana.Maana hii ni nchi huru na kila raia ana uhuru wa kuishi anavyotaka ili mradi haingilii haki za raia mwingine.
 
Me nadhani suala la kujadili afya za watu halina mantiki sana.Maana hii ni nchi huru na kila raia ana uhuru wa kuishi anavyotaka ili mradi haingilii haki za raia mwingine.

Hao "Watu" sio watu tu,ni viongozi,kuna tofauti. Fuatilia mkuu,suala la afya za viongozi linapewa kipaumbele kwasababu wao ndio kama idols na ndo maana JK alisema wazi hata kwenye ile interview kuwa alikwenda kupima yeye na mkewe ili kuwahamasisha wananchi nao wakapime nk.
Hapa ni mjadala tu maana kuna mambo hao "watu" wanayafanya ambayo hayazingatii utashi wa kawaida wa watu wa kawaida wenye akili timamu especially inapokuja kwenye ufisadi,kama vile wale wenye virusi wanaposemekana wanafanya makusudi kuvispread huwa hawajali na wanaponda tu bila kujali kesho,hiyo ni kwenye uongozi tunafananisha na watu kama hao na ndio maana mleta hoja akasema kama kwa kuuliza kuwa je "Ni kweli viongozi wetu wengi ni wagonjwa?" kuna waliotoa hoja za tofauti lakini bottom line mjadala huu si wa kujadili tu "watu" Bali ni kwanini viongozi wetu wanafanya maamuzi ambayo ni sawa tu na watu wasiojali kuhusu next generation,na sio tu kuwa hawajali the next generation,bali hata the current one wanai abuse.
 
Hao "Watu" sio watu tu,ni viongozi,kuna tofauti. Fuatilia mkuu,suala la afya za viongozi linapewa kipaumbele kwasababu wao ndio kama idols na ndo maana JK alisema wazi hata kwenye ile interview kuwa alikwenda kupima yeye na mkewe ili kuwahamasisha wananchi nao wakapime nk.
Hapa ni mjadala tu maana kuna mambo hao "watu" wanayafanya ambayo hayazingatii utashi wa kawaida wa watu wa kawaida wenye akili timamu especially inapokuja kwenye ufisadi,kama vile wale wenye virusi wanaposemekana wanafanya makusudi kuvispread huwa hawajali na wanaponda tu bila kujali kesho,hiyo ni kwenye uongozi tunafananisha na watu kama hao na ndio maana mleta hoja akasema kama kwa kuuliza kuwa je "Ni kweli viongozi wetu wengi ni wagonjwa?" kuna waliotoa hoja za tofauti lakini bottom line mjadala huu si wa kujadili tu "watu" Bali ni kwanini viongozi wetu wanafanya maamuzi ambayo ni sawa tu na watu wasiojali kuhusu next generation,na sio tu kuwa hawajali the next generation,bali hata the current one wanai abuse.

Hao unaodai wanakuwa abused,je,ni kwa ridhaa yao ama wanalazimishwa?they know what they get.and believe it,kama watu wanajulikana wameadhirika,then wanajulikana kwa hiyo hao wanaojirusha nao,ndio wa kuhojiwa!
 
Tatizo ni kwamba ikiwekwa sheria ya kuzuia tatizo hili inaweza kuwa implimented? maana kwa wenzetu kama Marekani ukimuambukiza mtu VVU kwa makusudi ni kosa la jinai linalo beba adhabu ya fine na hata kifungo. Je sheria kama hii ikiwepo nyumbani inaweza kutekelezeka? Tuna rasilimali za kutosha za kuchunguza tukio kama hili? Tatizo lingine ni kwamba hapa una wagusa hao hao viongozi. Je wata weka sheria ambayo itawabana wao wenyewe? Njia zipo za kuzuia tatizo hili lakini tatizo ni kama tuna hiyo nia na kama tunaweza kuchunguza kesi kama hiyo mpaka haki ipatikane.
 
Hao unaodai wanakuwa abused,je,ni kwa ridhaa yao ama wanalazimishwa?they know what they get.and believe it,kama watu wanajulikana wameadhirika,then wanajulikana kwa hiyo hao wanaojirusha nao,ndio wa kuhojiwa!

Mkuu si tu "Hao wanaojirusha nao" Ni mikataba inayosainiwa utadhani mtu anakufa kesho.
 
Tatizo ni kwamba ikiwekwa sheria ya kuzuia tatizo hili inaweza kuwa implimented? maana kwa wenzetu kama Marekani ukimuambukiza mtu VVU kwa makusudi ni kosa la jinai linalo beba adhabu ya fine na hata kifungo. Je sheria kama hii ikiwepo nyumbani inaweza kutekelezeka? Tuna rasilimali za kutosha za kuchunguza tukio kama hili? Tatizo lingine ni kwamba hapa una wagusa hao hao viongozi. Je wata weka sheria ambayo itawabana wao wenyewe? Njia zipo za kuzuia tatizo hili lakini tatizo ni kama tuna hiyo nia na kama tunaweza kuchunguza kesi kama hiyo mpaka haki ipatikane.

Mkuu, penye nia pana njia.

Kinachotakiwa ni kuchukua hatua halafu mapungufu yatakayojitokeza likiwemo ulilolitaja yatafanyiwa kazi kwa uwezo uliopo. Sidhani kuwa ni vyema kuacha kuchukua hatua muhimu kwasababu hatuna rasilimali za kutosha. Lini tutakuwa nazo rasilimali hizo? Baada ya watu wote kuangamia? Tunasita kwa mambo mengi mno na ya muhimu. Hatua ya kwanza kuchukua ndio hatu ya muhimu kuliko zote.

Haiingii akilini kuwa mtu anasita hata kuoa eti kwa kuwa hana utajiri wa kutosha kutunza familia wakati hajui ataupata lini utajiri huo, na kutunza familia kuna gharimu kiasi gani. Angalia, panga, amua, tekeleza....hii lazima iwe motto ya mtekelezaji yeyote. Hakuna kusita. Tutarekebisha makosa kadiri yatakavyojitokeza.

Ni kweli kuwa itakuwa vigumu sana kwa uongozi unaoendekeza ngono kupitisha sheria za kuwabana wao au wanaoendekeza ngono kama wao. Nadhani inabidi ipitishwe ndani ya Katiba kuhusu sheria za mambo yanayotamkwa kama "Janga la Taifa". Kama Katiba inataka Bajeti ya serikali ipitishwe la sivyo Bunge linavunjwa na uchaguzi mpya unaitishwa, kwanini sheria za majanga ya Taifa nazo zisipewe kipaumbele kama hicho?

 
This thread is inappropriate (OK, thats's just a politically correct euphimism for a toned down wrong) on so many levels.

1. Matters of health, especially to already elected officials, are to be private among civilized societies, unless the person afflicted deem it necessary not to make these very matters private.

2. Addressing these health issues in isolation from addressing the very same issues in the general population can be said to be harboring discrimination, favoritism or political machinations.

3. Elected officials are a mirror of our society.To object or discuss in any way that can be interpreted as objecting MPs with HIV is in a way denying representation in the parliament for HIV + Tanzanians. We do have an albino MP, I have not heard anyone raising the spectre of that condition incapacitating even mildly the MP. Are we really concerned about these MP's performance or is this insinuation merely masking the stigma that HIV/AIDS has acquired in our society? If we are concerned about performance is this the most pressing issue regarding MPs performance? How come I did not hear about Bujiku Sakila when he was terminally ill?

4. I gather small-mindedness on the part of some of us will never allow us to consider that the infection of HIV is not a death sentence, and may allow the infected to fully contribute to society.What if we reach HIV levels of Botswana and Swaziland, would we write off a quarter of our population just to satisfy our holier than thou attitudes?

5. Before pointing fingers at the MPs, have we checked ourselves? Are we completely positive that our behaviors are tantanimous with an HIV free society? Have we ensured that all the uncommon means of transmission cannot infect us? Are we imposing standards we cannot keep up with?

Jamani Pundit yupo wapi?
 
Dawa ipo kaka na dada zangu. naomba muwasiliane nami katika email yangu. nimewasaidia wengi mno hapa afrika ya mashariki. ni dawa imetayarishwa na wanasayansi waliobobea kutoka marekani na israel. niandikie katika ; dawamashariki@yahoo.com
 
Dawa hii nitakupa maeleza vile ya kuitumia na inaota virusi vyote vilivyomo katika damu kwa mda mchache sana. wiki mbili au tatu unaanza kurudia afya yako. yeyote atakaye agiza namtumia kwa kutumia dhl alafu itamfikia. hii ni dawa ambayo sasa hivi inatumika na mawaziri na watu wakubwa serikalini zetu hizi za afrika mashariki na asilimia mia kwa mia wamepona. nipate kwa email yangu, dawamashariki@yahoo.com
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom