Ni kweli Tanzania haihitaji takwimu hizi?

Ralph Feksi

Member
May 5, 2012
16
3
Wana JF.

Miongoni mwa babari zilizogonga vichwa vya habari leo ni kuhusu umuhimu wa kupata idadi ya waumini wa dini mbalimbali katika sensa ijayo. Ingawa serikali na baadhi ya vingozi wanasema si muhimu kuwa na takwimu hizo lakini hivi ni kweli hazihitajiki? Kweli si vema kujua Tanzania kuna Wazungu wangapi, Wahindi, Waaarabu, na kila kabila lina idadi ya watu wangapi? Hivi ni sahihi kusema kuwa na takwimu hizi itahatarisha amani ya nchi!

MY TAKE: Ninaamini watafiti wa sayansi jamii, wanasaikolojia, viongozi wa dini nk wangependa kupitia sensa ya taifa wapate takwimu hizi.

Ninawasilisha.
 
Ukweli ni kwamba hizi takwimu ni muhimu sana tu ili kujua mgawanyiko wa Watz ktk makundi tofauti. Ila sasa inapokuja issue ya maendeleo hatuhitaji kujua dini wala kabila la watu ili kuwapatia huduma muhimu, na hii ni kwa sababu watz tumechanganyikana kwa kila aina unayoweza kuifikiria. Tatizo kubwa ni kuna watu wachache wanataka kuitumia nafasi hii kisiasa au kwa maslaji binafsi, kama makanisa au misikiti inataka kujua idadi ya waumini wao si wakahesabu wenyewe!!! Na je ukishajua wepi wengi inasaidia nini??? Wapi huduma za kiserikali zinatolewa kwa misingi ya dini au kabila???? Mie nina ndg waislam, wakristo na wapagani na tumeoa na kuolewa na makabila kutoka kila kona na nje ya TZ, je hapa idadi ya kikabila inasaidia nini esp mtu kama mimi ambaye najua kiswahili labda na English tu na sifungamani na kabila lolote!!!!!!!
 
Kwaupande wangu sioni Tatizo lolote kwa Tanzania Kuwa na Takwimu hizo kwani Vyovyote iwavyo wakristo watakuwa wakristo na waislam watabaki kuwa waislam mwisho wa siku na Watanzania watabaki kuwa watanzania Hoja hapa ni Utanzania na sio DINI,tuwe nazo tu takwimu kwani hazitoathili chochote
 
Dhehebu linalotaka kujua idadi ya waumini wake linashindwaje kuwahesabu lenyewe mpaka lipitie kwenye mgongo wa sensa ya taifa? Hawa waumini wetu mbona tunao kwenye nyumba zetu za ibada karibu kila siku? Mambo kama haya ni kuleta misuguano isiyokuwa na lazima katika jamii.
 
Wana JF.
Miongoni mwa babari zilizogonga vichwa vya habari leo ni kuhusu umuhimu wa kupata idadi ya waumini wa dini mbalimbali katika sensa ijayo. Ingawa serikali na baadhi ya vingozi wanasema si muhimu kuwa na takwimu hizo lakini hivi ni kweli hazihitajiki? Kweli si vema kujua Tanzania kuna Wazungu wangapi, Wahindi, Waaarabu, na kila kabila lina idadi ya watu wangapi? Hivi ni sahihi kusema kuwa na takwimu hizi itahatarisha amani ya nchi!
MY TAKE: Ninaamini watafiti wa sayansi jamii, wanasaikolojia, viongozi wa dini nk wangependa kupitia sensa ya taifa wapate takwimu hizi.

Ninawasilisha.
wafanye wenyewe na kwa g'harama zao,si sadaka zinatolewa???acha mabo ya ajabu bwana.
 
Kwaupande wangu sioni Tatizo lolote kwa Tanzania Kuwa na Takwimu hizo kwani Vyovyote iwavyo wakristo watakuwa wakristo na waislam watabaki kuwa waislam mwisho wa siku na Watanzania watabaki kuwa watanzania Hoja hapa ni Utanzania na sio DINI,tuwe nazo tu takwimu kwani hazitoathili chochote
Wazo lako ni zuri, lakini mawazo ya wenzako wale wa "matamko" ni kwamba wanataka pato la taifa ligawanywe kufuata uwiano wa idadi ya watu kidini na nafasi za uongozi wa taifa vile vile. Kwa mantiki hiyo, wasukuma ambao ni 20% ya idadi ya watanzania wote nao watakuwa na haki ya kudai kupata 20% ya pato la taifa. Mwisho wa siku sijui tutafika wapi!
 
Wazo lako ni zuri, lakini mawazo ya wenzako wale wa "matamko" ni kwamba wanataka pato la taifa ligawanywe kufuata idadi ya watu kidini na nafasi za uongozi wa taifa vile vile. Kwa mantiki hiyo, wasukuma ambao ni 20% ya idadi ya watanzania wote nao watakuwa na haki ya kupata 20% ya pato la taifa. Mwisho wa siku sijui tutafika wapi!
Comrade liweke sawa hilo neno lilo colored wa "matamko" sio wenzangu, wenzangu mimi ni wajamaa,Comrade wajua tatizo ni Serikali kutotaka mabo haya kujadiliwa kwa uwazi kwa sababu huenda hata wale wa Umsho hawana sababu za msingi lakini kwa sababu hamtaki kuwasikiliza wanaonekana nao wanasababu Tuwaache watanzania wazungumze lakini si kila watakachokisema basi kichukuliwe,ni hayo tu Comrade
 
Kwaupande wangu sioni Tatizo lolote kwa Tanzania Kuwa na Takwimu hizo kwani Vyovyote iwavyo wakristo watakuwa wakristo na waislam watabaki kuwa waislam mwisho wa siku na Watanzania watabaki kuwa watanzania Hoja hapa ni Utanzania na sio DINI,tuwe nazo tu takwimu kwani hazitoathili chochote

Kwa nini tuwe na kitu ambacho hakina maana wala athari? kama ulivyosema?
Huoni kama nikupoteza nguvu kwa jambo lisilo la kimaendeleo?
Kama halina athari hakuna haja ya kuwa na hizi TAKWIMU.
 
vitu kama kama vinahitajika kwa ajili ya dini kwa nini makanisa na misikiti wasihesabiane huko huko??
kuna watu wengi tu hapa bongo hawana dini kwa nini muanze kuingiza dini kwenye suala la kitaifa??
hata kwa suala la makabila si nyeti sana kama watu wanavyodhani
 
Dhehebu linalotaka kujua idadi ya waumini wake linashindwaje kuwahesabu lenyewe mpaka lipitie kwenye mgongo wa sensa ya taifa? Hawa waumini wetu mbona tunao kwenye nyumba zetu za ibada karibu kila siku? Mambo kama haya ni kuleta misuguano isiyokuwa na lazima katika jamii.

Mkuu
Ni kweli na nina amini kwamba kila dhehebu linajua au lina idadi ya waumini wao.
Lakini serikali inatakiwa kujua hilo zaidi. (itatokana na jinsi unavyojua umuhimu wa kuwa na tarakimu)
 
Ukweli ni kwamba hizi takwimu ni muhimu sana tu ili kujua mgawanyiko wa Watz ktk makundi tofauti. Ila sasa inapokuja issue ya maendeleo hatuhitaji kujua dini wala kabila la watu ili kuwapatia huduma muhimu, na hii ni kwa sababu watz tumechanganyikana kwa kila aina unayoweza kuifikiria. Tatizo kubwa ni kuna watu wachache wanataka kuitumia nafasi hii kisiasa au kwa maslaji binafsi, kama makanisa au misikiti inataka kujua idadi ya waumini wao si wakahesabu wenyewe!!! Na je ukishajua wepi wengi inasaidia nini??? Wapi huduma za kiserikali zinatolewa kwa misingi ya dini au kabila???? Mie nina ndg waislam, wakristo na wapagani na tumeoa na kuolewa na makabila kutoka kila kona na nje ya TZ, je hapa idadi ya kikabila inasaidia nini esp mtu kama mimi ambaye najua kiswahili labda na English tu na sifungamani na kabila lolote!!!!!!!
brother kwani sensa ni nini? je senza inapofanywa huwa ni kwa matumizi ya maendeleo ya selikali tu?je unafahamu umuhimu wa sensa wewe? mfano kuna kabila moja hapa tanzania linahitaji uangalizi na mahitaji maalu je usipojua idadi yao selikali itapangaje bajeti kwa ajiri ya kuwahudumia hawa watu?, kuna watu wa mahitaji maalum kama albino je usipojua idadi yao utawasaidiaje?, but pia sensa ndo source of information, watu wote na taasisi ndo tunatakiwa tutoe huko data.
 
Back
Top Bottom