Ni kweli NnauyeJr hawajui Mbowe, Slaa?

Donyongijape

JF-Expert Member
May 28, 2010
1,497
811
Nimesoma katika gazeti la Tanzania Daima na kukutana na hii kali ya mwaka, Eti Nape Hawajui Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Katibu wake, Dk. Willbrod Slaa katika duru za siasa nchini. Alikuwa akijubu tuhuma dhidi ya chama chake juu ya kile kilichodaiwa kuwepo kwa mipango ya kuwabambikizia kesi baadhi ya viongozi wakuu wa CHADEMA kwa lengo la kuwadhoofisha wao binafsi na chama kwa ujumla.Nape alisema hawezi kujibu madai yasiyokuwa na maana na pia hawajui hao wanaoitwa Mbowe na Slaa.

"Nimesahau kama wapo Dk. Slaa na Mbowe ndiyo unanikumbusha wewe," alisema na kuongeza kuwa viongozi wa CCM hawajakutana mahali popote kuzungumzia suala hilo na kueleza kuwa huo ni upuuzi usiokuwa na mashiko.


Nape alidai kuwa viongozi wa CCM hawana muda wa kuwafikiria CHADEMA, kwani si chama chenye maana kinachoweza kuwasumbua wala kuwapotezea muda.
"Uchaguzi umekwisha, hatuna muda wa kuwafikiria viongozi wa CHADEMA, kwanza si chama, sasa tunafikiria kutekeleza ilani ya chama chetu,'" alisema.

Alisema kuwa viongozi wa CHADEMA ndio wenye muda wa kuwafikiria viongozi wa CCM na kusema, "Wao ndiyo wanafikiria, ‘tumfanyeje Nape na JK'."


Majibu ya Nape yamekuja siku mbili tu baada ya kutoa matusi mazito katika mkutano wa hadhara uliofanyika jijini Mwanza.


 
Kumjadili Nape ni kumpa umaarufu usio wake. Kitendo chake cha kuporomosha matusi Jukwaani kimenifanya nimuone kama kiongozi mwehu na kuanzia sasa sitajadili lolote limhusulo Nape. Ni kupoteza muda tuu.
 
Kwani Nape akiwajua Slaa na Mbowe inawasaidia nini?
Kwani kazi zao hazitatekelezwa kwa kuwa Nape hawajui?
Mi' nadhani siasa zetu za majitaka kwa viongozi wa aina hii
ndizo zilizotufikisha hapa...
 
Hatumshangai huyo nepi mbona hamtambui hata baba yake mzazi ?Atuambie lini alienda kumuona Profesa huko India anakougulia?
 
Kadri siku zinavyokwenda, uwezo wa kufikiria wa huyu kijana mwenzetu unashuka kwa kiwango kikubwa. Kwa sasa umefikia lever ya Makamba Snr!(Uropokaji nakusahau alichoong Baada ya mwaka nafikiri atakuwa lever ya Kingendu ( msanii mchekeshaji asiye na mvuto)
 
Mimi nadhani imefika wakati wa kusitisha kuandika habari yoyote inayomhusu nape. Maana mwenzetu tunashindwa kuelewa kama ndo siasa hizo au lipo tatizo la msingi. Naogopa tusije onekana wote kama yeye.

MOD: tafadhali naomba thread yoyote inayomhusu nape ipige chini.
 
Kajitahidi kuwa muwazi kwa kutangaza upumbavu wake, iliyobaki ni sehemu yetu kujua kama anahitaji kusaidiwa na kwa kiwango kipi au lah.....
 
mbona wanaomtukana Rais hapa JF tunaendelea kuwasikiliza kwa nini kwa NAPE tusimsikilize akitukana matusi
 
Kwani kuna umuhimu gani Nape kama Nape kuwatambua viongozi wa chama chochote cha upinzani ( including Mbowe na Slaa).

Wananchi wanawatambua. Kwisha.
 
Ni kweli mkuu tusimpe umaarufu nape a.k.a vuvuzela la CCM. Huyo ni mtu mdogo sana kumzungumzia.
Kumjadili Nape ni kumpa umaarufu usio wake. Kitendo chake cha kuporomosha matusi Jukwaani kimenifanya nimuone kama kiongozi mwehu na kuanzia sasa sitajadili lolote limhusulo Nape. Ni kupoteza muda tuu.
 
Nape anamjua huyu kamanda tu
284361_186626591367378_100000601150906_593838_6922930_n.jpg
 
Dogo anashangaza,hata kama ni dharau ni zaidi.kwa nafasi yake ya kiuongozi chamani huwezi sema humtambui mtu ambaye aligombea urais na kumtoa jasho vilivo JK,wala kutomfahamu mtu ambaye pia ni mbunge wa Bunge la Tanganyika/tanzania na kiongozi wa kambi ya upinzani. All in all atambue asitambue hali ni moja tu
 
kuna mtu aliniambia kila anayetamani kushikisha wenzao ukuta ni hasira za yeye kushikishwa ukuta akiwa mtoto,sasa huyu dogo msimlaumu sana labda akili ilidumaa kwa sababu ya hiyo kitu kupigwa sana.
tumwombee alikuwa mlokole alituimbia kanisani hapa singida kumbe masikini ya mungu alikuwa ameshaathirika kisaikolojia,alikuwa anasubiri akue apate madaraka ili aje kulipiza visasi ila namshauri kama ni visasi awalipie hao wazee wa ccm waliomlaghai na kumshikisha hiyo kitu.
masini yule mzee na uadilifu wake alifikiri ndani ya chama ni wa\zee wenzake kumbe wanamuharibia mtoto.
 
Back
Top Bottom