GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,278
- 6,672
Habarini wana JF, Nimekuwa nikisikia kwa watu mbalimbali kuwa kuna wakati mwanamke akiwa mjamzito basi ile misukosuko ya mimba ikiwa ni pamoja na uchungu, kichefuchefu humkuta mwanaume pia. Kwanza naomba Mungu kama ni kweli hali hiyo isinikute. Pili nataka kujua kutoka kwenu kama mmewahi kushuhudia kitu kama hicho! kama ni kweli kuna anayefahamu inatokana na nini?