Sitaki kuzungumzia kuhusu kushuka kwake maana hilo lipo wazi na wala halihitaji mtu mwenye digrii ya muziki ili kung'amua jambo hilo. Ukweli ulio wa haki muziki wa huyu jamaa ni mwepesi sana ukilinganisha wasanii wengine wa kariba yake japo si wote. Kama wewe ni miongoni mwa wanaofikiria kuwa siku moja Diamond atakuja kuwika anga za kimataifa basi utakuwa hujui dunia inahitaji muziki upi. Wapo watakaosema mbona Ngololo imeshika namba moja Trace Tv ila nikuambia hiyo imetokana na uwepo wa Davido katika wimbo huo. Ladha za nyimbo nyingi za Diamond ni bazoka, utamu unaisha fasta, na dunia haitaki aina hiyo ya muziki. Sikilizi le wimbo wa Nikupe ulioimbwa na akina Mandojo kisha fananisha na Ngololo labda ndo utadhibitisha kuwa mashairi ya Diamond ni mepesi. Diamond huu ni mwanzo wa mwisho wa zama zako!!!!!
Mkuu tuletee mrejesho.. Unaonaje kijana kashapote? au mganga wako alifariki?