Balantanda
JF-Expert Member
- Jul 13, 2008
- 12,476
- 4,752
Salama wakuu wangu wapenda michezo....
Kwa muda mrefu nimegundua kwamba TFF ya Leodgar Chilla Tenga imekuwa ikifanya jitihada kuhakikisha kwamba Michael Richard Wambura kwa namna au njia yoyote ile hashiriki shughuli za TFF.......Je tatizo ni nini hasa?.......Wanamuogopa?.......Ni kwa nini mara zote wamekuwa wakimuwekea mizengwe kiasi cha kukataa hata Rufaa zake mara anapoenguliwa katika kugombea uongozi,mfano juzi jina lake lilienguliwa katika kugombea nafasi ya Uenyekiti wa chama cha soka cha mkoa wa Mara na jana alipojaribu kupeleka rufaa yake kupinga uamuzi huo watendaji wa TFF pale Ilala walikataa katakata kuipokea Rufaa hiyo.............Kunani?
Kwa muda mrefu nimegundua kwamba TFF ya Leodgar Chilla Tenga imekuwa ikifanya jitihada kuhakikisha kwamba Michael Richard Wambura kwa namna au njia yoyote ile hashiriki shughuli za TFF.......Je tatizo ni nini hasa?.......Wanamuogopa?.......Ni kwa nini mara zote wamekuwa wakimuwekea mizengwe kiasi cha kukataa hata Rufaa zake mara anapoenguliwa katika kugombea uongozi,mfano juzi jina lake lilienguliwa katika kugombea nafasi ya Uenyekiti wa chama cha soka cha mkoa wa Mara na jana alipojaribu kupeleka rufaa yake kupinga uamuzi huo watendaji wa TFF pale Ilala walikataa katakata kuipokea Rufaa hiyo.............Kunani?
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limekataa kupokea rufani ya mgombea nafasi ya uenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Mara (FAM), Michael Wambura kwa maelezo kuwa hakuna mamlaka yenye uwezo kusikiliza shauri lake nchini.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Wambura alisema anashangazwa na hatua ya TFF kwani alifika kwenye ofisi za shirikisho hilo Uwanja wa Karume, Ilala jana mchana kuwasilisha rufani
yake kwa Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF lakini alikataliwa.
Nimekaa kwa zaidi ya saa mbili, najaribu kuwaeleza wapokee rufani yangu lakini hawataki,
inaelekea kuna maelezo kutoka juu wamepewa hawa watu wa mapokezi wasipokee rufani ya
Wambura, inasikitisha sana, alidai.
Wambura alieleza kuwa baada ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF kumuengua alitaka kukata rufani Kamati ya Nidhamu inayoongozwa na aliyepata kuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Alfred Tibaigana.
Juzi Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliondoa jina la Wambura kwa madai kuwa aliwahi kupeleka masuala ya soka mahakamani kinyume na Katiba ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), TFF na FAM.
Akizungumzia suala hilo, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alikiri jambo hilo kutokea na
kwamba waliamua wasipokee sababu kulingana na kanuni za TFF, Kamati ya Uchaguzi ndiyo
yenye mamlaka ya mwisho kwa hapa nchini.
Alisema Wambura anaweza kukata rufani kwenye Mahakama ya Rufaa ya Michezo (CAS) iliyopo Lausanne, Uswisi.
Alisema TFF ilizifanyia marekebisho kanuni zake na kuwa chombo ambacho kinaweza kutengua maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ni CAS na si Kamati ya Nidhamu ya TFF.
Hata hivyo, Osiah alisema pamoja na Wambura kuelezwa hivyo alingangania fomu zake
zipokelewe, lakini si rufani ila iwe kama barua, hivyo akawaagiza wafanyakazi wake kuipokea kama barua ya kawaida na kuwataka wasipokee ada ya rufani.
Lakini Wambura akizungumzia maelezo hayo ya Osiah, alisema ni ya kushangaza na
hayapaswi kutolewa na kiongozi kama yeye kwani sio msemaji wa Kamati ya Nidhamu.
Mimi nawashitaki TFF, sasa yeye anawasemea Kamati ya Nidhamu, TFF wao wanachopaswa ni kupokea rufani yangu, kisha Kamati ya Nidhamu ndiyo itasema haina uwezo wa kusikiliza.
Hata mahakamani, kesi inafika kwanza huko hata iwe ya mauaji, inaweza kuanzia mahakama
ya kawaida, baadaye shauri linapelekwa Mahakama Kuu, ila huwezi ukasimama pembeni
ukasema usilete kesi hiyo.