Jina limeleta zogo, butege umeisha wema,
Mbona hilo bado dogo, kubwa u bado kusema,
Nahisi wewe kigogo, wameza bila kutema,
hata usiwe rijali, sikufichi miye misi
misi ni lao wazungu, sie kwetu mlimbwende,
adimu kama uvungu, hupati hata upinde,
japo uwinde kwa rungu, miye napiga umande,
hata usiwe rijali, sikufichi miye misi
vipi usome picha, watesa yako akili,
wakodoa hadi kucha, eti Judi mkali,
heri kutafuna kucha, ukwepe yangu makali,
hata usiwe rijali, sikufichi miye misi
bado kufikwa umama, hilo nalo naringia,
bikira yangu ni njema, wengi wanaizingia,
heri wajua mapema, japo huwezi sogea
hata usiwe rijali, sikufichi miye misi
bUtege kama wewe samaki basi ni ngisi
kila nikikusoma unatema risasi
umemshindwa cheusi
sasa uko kwa misi
uwe mwangalifu lina miba hilo nanasi
kwa nini wajita wasiwasi
na mambo ya kuhisi
utaonekana kama kamasi
mbele ya kadamnasi
uwe mwangalifu lina miba hilo nanasi
hizi wala sio tetesi
ni ukweli usio na kesi
butege huyo kweli ni miss
kwa vipimo vya TBS
uwe mwangalifu lina miba hilo nanasi
mbona warusha mazito, maneno yaso hekima,
hata ungetoa bito, bikira huwezichuma,
sitamani hata vito, nalinda yangu heshima,
ubikira wangu wito, kwa ndoa yenye heshima,
tunza zako milioni, au zitoe hisani,
sio kwake sokoni, bidhaa huna yakini,
wawezatupa shimoni, bila wapa masikini
ubikira wangu wito, kwa ndoa yenye heshima,
Hapa tumeingia kwa mama mkwe,
Sie tusio na tunzi wala vina tutatumia lugha gani wajameni?
Naona MMU imefikia TBS!!!
Babu DC
Nyote niwategaji.
Mishipi ndani ya maji.
Miss J na na muulizaji.
Mwajaribu kupima maji.
Nyote mwavinjali
Miss Judy na Rijali.
Munaanza na maswali.
mwisho mwavua suluali.
Hapo hakuna mwali
hapo hakuna rijali.
mwaeleza zenu siri.
mwatafuta yafahari.
peaneni namba ifichuke siri.
kutaneni tujue yupi mkweli
Sisi siwazungu ni waswahili.
Tumeshaelewa yenu mashairi.
Musisahau mwevuli.
Muendako mbali.
Muvalishane vizuri.
musijepata homa kali.
Mimi si mshairi,bali msema kweli.
Maneno simsumari,kamanimekosa nitakiri.
Munisamehe washairi,Miss J na Rijali.
Musinione dalali,nilitaka toa tu tahadhari.
uwiiiiii
mie nilikua wapi,kuona hizi tenzi,
nahangaika na kwingine,ilhali hapa bayana,
kweli fani ni yetu halisi,kuenzi zetu tungo,
kweli nimewachwa hoi,watu kumendea vya watu.
kwanini umendee vya watu,hadharani kujimwaga,
kama kweli u-rijali mnona waonyesha woga,
kuiita kadamnasi,hapa jf kujieleza,
hizo ni dalili za woga,pasi kwenda pm.
kwanini hujenda pm,mlimbwebde kumsabahi,
ni jambo lililo la kheri,siri yako kuhiifadhi,
sema nae kwa sirini,labda utaipata yako tunu,
Kashaija ulifikiri nini,mlimbwende haanikwi.
mlimbwende haanikwi,hadharani kama mahindi,
mafunzo ya mama yakini,ya sirini ndio majibu,
rijari hufata nyumbani,wazazi wake kujitosa,
ongoza lako guu,upate lake kwa heri...
ha ha ha nilikuwa wapi siku zote hizi???