Kashaijabutege
JF-Expert Member
- Oct 20, 2010
- 2,696
- 740
Judi nijibu swali, kwa nini unaitwa 'Misi'?
Ni mwembamba yako hali, au mrembo tausi?
Ulimi wako asali, wa tamaa kama fisi?
Ni kweli wewe ni 'Misi', nijuze mie rijali.
Pichani sio kigoli, iweje uitwe 'Misi"?
Hulandani nao wali, kuna vitu vinamisi,
Hauna ndoa halali, ni kwanini 'Misi' basi?
Ni kweli wewe ni 'Misi', nijuze mie rijali.
Judi nakiri mkali, usotishwa naye pusi,
Ingawa nakwona mbali, nimekuchunguza nyusi,
Wewe ni mama halali, sioni wako 'umisi',
Ni kweli wewe ni 'Misi', nijuze mie rijali.
Ni mwembamba yako hali, au mrembo tausi?
Ulimi wako asali, wa tamaa kama fisi?
Ni kweli wewe ni 'Misi', nijuze mie rijali.
Pichani sio kigoli, iweje uitwe 'Misi"?
Hulandani nao wali, kuna vitu vinamisi,
Hauna ndoa halali, ni kwanini 'Misi' basi?
Ni kweli wewe ni 'Misi', nijuze mie rijali.
Judi nakiri mkali, usotishwa naye pusi,
Ingawa nakwona mbali, nimekuchunguza nyusi,
Wewe ni mama halali, sioni wako 'umisi',
Ni kweli wewe ni 'Misi', nijuze mie rijali.