Ni kutunishiana misuli kwa mihimili au kuna siri ndani yake?

harakati83

Member
Aug 5, 2010
61
5
Ndugu wanajamii wenzangu, naomba kuleta hoja hii mezani kama wanaharakati tuijadili,tuone tatizo na pia tutoe Altenatives.
Ni kuhusu suala la Jairo, Serikali ambayom kimsingi kabisa sisi ndio mabosi wake,kwa niaba yetu nayo ili kazi ziende ikamwajiri Luhanjo naye kama wakala akamwajiri Jairo,kwa upande mwingine mabosi wa serikali ya tz ambao ni sisi tumeweka wawakilishi wetu(WABUNGE) kuisimamia serikali:-

  • Naunga mkono Jairo kufutwa kazi kupitia waziri mkuu
  • Napinga kwa Nguvu zangu zote Jairo kufukuzwa bila mawaziri wake Ngeleja&Malima kufutwa(sio kujiuzulu) uwaziri
  • Kama mkicheki kwa umakini Luhanjo alifanya kitu kama kuwakumbusha wabunge kuwa Hatukatai wabunge(P.M kama sehemu ya wabunge)kumfuta Jairo(ambaye ni mtendaji)kazi ila kwanini wabunge wanakuwa Bias kwa Kuamua kabisa kwa makusudi kujadili mtendaji (Jairo) katika issue ambayo ana bosi wake (mwanasiasa/waziri lakin zaidi mbunge) ambao ni Ngeleja&Malima, kama ni kuwajibisha ilifaa iwe wote.
  • kwa kutambua hilo akaamua kufanya kinachoitwa kulindana( yaan wabunge si wanawalinda wabunge wenzao(malima & ngeleja)ambao ni wanasiasa,basi wacha namienimlinde mtendaji mwezangu Jairo.
  • Ushauri wangu wote wafutwe kazi (jairo,luhanjo kwa upande mmoja na Malima&ngeleja kwa upande mwingine.
Naomba kuwasilisha hoja
 
Kila mtu anayo haki ya kikatiba ya kupata utetezi. Unaposhauri Ngeleja, Malima Jairo wafutwe kazi ukubali kufanya kazi ngumu ya kukusanya ushahidi ambao hautakuwa na mashaka yoyote kuwashtaki hao watuhumiwa. Vinginevyo mimi nakuona kama chura tu anayepiga makelele bwawani kuzuia ng'ombe wasinywe maji.
 
inatakiwa kuandaa ushahidi wa kuonyesha kwa undani zaidi wa wao kufutwa kazi ... ki kawaida hatuna utamaduni wa kujiuzuru pindi mambo yanapokuwa si mambo hata kwa kutuhumiwa...
 
BTW, who's Jairo? wezi serikalini wako wengi na wanapeta lakini ukiona wanasiasa wamemshupalia mmoja wao ujue kuna jambo! hapa sitashangaa kuna mtu wa karibu na huyu Jairo anachimbiwa shimo; je, atakuwa nani huyo?
 
Kila mtu anayo haki ya kikatiba ya kupata utetezi. Unaposhauri Ngeleja, Malima Jairo wafutwe kazi ukubali kufanya kazi ngumu ya kukusanya ushahidi ambao hautakuwa na mashaka yoyote kuwashtaki hao watuhumiwa. Vinginevyo mimi nakuona kama chura tu anayepiga makelele bwawani kuzuia ng'ombe wasinywe maji.

Mwita Tata Ningakhe? Leo nimeamua nikujibu maana sio kila siku ushahidi usio kuwa na mashaka... kumbuka hata circumstancial au ushahidi wa kimazingira unakubalika...

Kama Jairo ni katibu mkuu wa wizara X na mabosi wake ni mawaziri au manaibu waziri wa wizara x ina maana atafanya kazi ya kuchangisha michango au kufanya kitu chochote kile bila ya wao kuambiwa au ku-aproove hayo anayofanya?

Ndio maana Jairo hakuwa Mjinga na kuyafanya yote aliyoyafanya kwa maandishi ili aje kuwa na back up ya ushahidi maana ina maana kwamba hiyo circular ilifika pia kwenye desk la waziri na naibu wake .Na kama jibu NI ndio, ndio KWAMBA WALI-APROOVE action zake... MWITA...Ni ushahidi gani unaoutaka tena?

Mtu wa chini akiharibu ni bosi wake inafaa achuke manyanga yake na kujiudhuru... full stop... unless kama tukichukua doctrine ya Agent- Principal relatinship kwamba a principal cannot be held responsible for illegal actions of his agent if he (PRINCIPLE) was unware of the illegal act carried on his name or behalf ..

Hata kama akina Ngereja na Malima watasema kwamba hawakujua nini Jairo alichokuwa anafanya au ni kama za masjala za kupanga mafaili tu bila kujua ni nini kilichomo?

Ambe tata uhoye....
Lakini kumbuka Ngereja na Malima wasilete amang'ana ya Walisi maana tangu lini abhalisi wakangangata e kyalo?
 
Ushaidi gani mnaongelea, wakati tunajua kabisa Jairo na Malima na ngaleja walikiwa wanachangisha pesa kama za harusi kutoka department mbalimbali za wizara- barua alituonyesha mhe Shelukindo- na pesa hizo zilikuwa kwa ajiri ya kuhonga wabunge ili bajeti ipite-hii ni kashfa tosha ya kumfukuza kazi waziri, naibu waziri na katibu. Wawakilishi kuhongwa!!! Tanzania tunakwenda wapi?
 
Back
Top Bottom