Ni kubota au khubota?ufisadi mwingine wa power tila.

jerry monny

Member
Dec 6, 2010
94
0
hii serekali ya sisiemu kweli ni uoza mtupu,jana kwenye taarifa ya habari saa mbili usiku walionyesha tena ujuzi wao wa kuwadanganya wapiga kura wao wakulima ni kwa namna gani ni ma mbumbumbu,wamewaletea power tiller feki zenye jina khubota badala ya kubota.serekali ilishasema hakuna bidhaa itaingia nchini ikiwa hana viwango vya kimataifa,sasa inakuaje tena wao ndio wanakua mstari wa mbele katika kuagiza hizo bidhaa feki?hivi hawa wakulima wataendelea kufanywa hamnazo mpaka lini jamani.?kingine kinachotia kichefuchefu ni kuona vijana tena wasomi wanaipa sapoti ubadhilifu kama huo,wizi wa waziwazi alafu msomi anakua mstari wa mbele kuipa sapoti jambo kama hilo.inasikitisha sana kama pia elimu inatumika katika kudidimiza haki na maendeleo ya taifa lake na wananchi wake.kweli kuishi katika uongo na unafiki ni ngumu sana alakini kwa wengine huonekana ni jambo jepesi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom