Toa maoni yako kwenye huu uzi kuhusu chochote ambacho ungependa kiwepo au kisiwepo kwenye katiba mpya ili tutakapokutana na Tume tutoe maoni yanayofananafanana.
Wazee wote kuanzia miaka 65 wasitaafu na ambao hawakuwa watumishi kwa ujumla watunzwe na serikali kama kundi maalumu
Watumishi waruhusiwe kupewa haki ya kufanya siasa mfano ktk uchaguzi na wawe huru kuendelea na kazi zao za awali endapo hawakupata kuchaguliwa ktk nafasi za kisiasa
Rais apunguziwe madaraka ya kuteua vyeo kibao! Viti maalumu viwe maalumu kweli mfano,walemavu,wazee,vijana,albino,wanawake baasi kila chama kitoe viti sawa!! RC,DC,Mawaziri,wakurugenzi wa idara mbalimbali/wilaya/mkoa,Makatibu wa wizara na wote wanaoteuliwa na prezda wote wawe wanaapply position hizo na qualification husika strictly degree/master/phd etc
mbunge aweze kuadabishwa na wananchi sio lazima afikishe miaka mitano na akiondolewa mshindi wa pili ashike kiti(kuepuka gharama za uchaguzi)
Mfanyakazi wa umma waziri,mkurugenzi,katibu na vyeo vinavyofanana na hvyo akila rusha au akiliingizia hasara taifa shurti afilisiwe na apate mvua zisizopungua 10
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.