tatanyengo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2011
- 1,134
- 280
Kuna sababu nyingi zinazowafanya watu kutoka nje ya ndoa zao. Moja ya sababu ni kutoridhishwa na mwenza katika kufanya tendo la ndoa. Hali hii hutokea pale wanandoa wanaposhindwa kuwa wazi kwa maana ya unataka ufanyiwe nini mnapokuwa faragha. Sababu nyingine ni kutojaliana (caring).Jambo hili hutokea wanandoa wanaposhidwa kujali mambo ambayo pengine tunafikiri ni madogomadogo kwa mfano kupeana pole au hongera kwa kutenda/kutotenda jambo fulani.Hivyo tunashauriwa kuwa wazi na pia kuendelea kujifunza zaidi kuhusu mahusiano.