gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,274
- 20,673
wapendwa wana mmu. habari za jumapili? natumai ni njema sana kwani wengine mko kwenye sherehe za vipaimara na wengine mko na mechi ya spain na italy. yote ni heri tu katika kujipa raha.
Leo nimekuja tena na mada hapa nataka tuidadavue kuhusu mahusiano yetu na wenzi wetu.
Hivi ni kwanini wapenzi tunazoeana sana kiasi kwamba tunashindwa kabisa kudumisha mapenzi yetu? kwa nini inakuwepo dhana ya kuzoeana sana kuliko pitiliza kunakopelekea kuona mwenzi wangu ni mtu wa kawaida tu?
mathalani mama/binti akishakaa na mwenzi wake baada ya muda hakuna tena hata kuflirt nae, akimtumia sms kama ni mchana basi ni ile ya kawaida tu ambayo haionyeshi kujali au haimuhamasishi mpenzi wako. Pia na wanume nao hivyo hivyo. kwanini?
miye kungwi wenu kwa usukununu wangu nimegundua kuwa wanaotuibia wapenzi wetu wako makini sana mara zote anatuma sms kwa mpenzi kumbembeleza, kumsifia na wengine wanakumbushia hata mchezo walivyofaidi ili hali sisi tulioko ndani tumekaa kimya tunajua ni wangu tu, kwanini nimvizie na manati....lol jamani turudi nyuma tena tuanze kuweka vizuri mapenzi yetu.
mwenye masikio na asikie neno hili.
Leo nimekuja tena na mada hapa nataka tuidadavue kuhusu mahusiano yetu na wenzi wetu.
Hivi ni kwanini wapenzi tunazoeana sana kiasi kwamba tunashindwa kabisa kudumisha mapenzi yetu? kwa nini inakuwepo dhana ya kuzoeana sana kuliko pitiliza kunakopelekea kuona mwenzi wangu ni mtu wa kawaida tu?
mathalani mama/binti akishakaa na mwenzi wake baada ya muda hakuna tena hata kuflirt nae, akimtumia sms kama ni mchana basi ni ile ya kawaida tu ambayo haionyeshi kujali au haimuhamasishi mpenzi wako. Pia na wanume nao hivyo hivyo. kwanini?
miye kungwi wenu kwa usukununu wangu nimegundua kuwa wanaotuibia wapenzi wetu wako makini sana mara zote anatuma sms kwa mpenzi kumbembeleza, kumsifia na wengine wanakumbushia hata mchezo walivyofaidi ili hali sisi tulioko ndani tumekaa kimya tunajua ni wangu tu, kwanini nimvizie na manati....lol jamani turudi nyuma tena tuanze kuweka vizuri mapenzi yetu.
mwenye masikio na asikie neno hili.