Wakumwitu
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 370
- 82
Ngoja NE na mm nikuambie. Maisha ni safari ndefu sana kuna miba, mabonde , mito, milima nk. Lakini katika safari hiyo pia kuna vikwazo vingene ambavyo unakumbana navyo. Ukiwa katika kundi la watu unatakiwa uishi vile wewe unataka kuishi na wala usishawishiwe na mtu ama watu. Michango yako japo kuwa ww unaona inawaudhi watu, kumbuka kuna wale ambao huwa hawachangii na wanajifunza kitu kutoka kwako. Mfano nakumbuka umewahi kupost jinsi ulivyo mzimikia mume wa jirani yako. Ukweli ni kwamba, ww ulisema ukweli, lakini katika jamii haya hayapo???? kuna watu wanajifanya watakatifu humu lakini ukweli ndiyo wanayoyafanya. Kufikisha ujumbe kwa jamii siyo lazima ww utende, lakini ukaufikisha na watu ukawagusa. Kuna watakao uponda kuona haiwezekani, na kuna watakaoguswa na kuuchuna. Ushauri wangu kwako ni kama ifuatavyo. Jukwaa lina watu wa kila aina, kuna waliowazuri wa saisa, biashara nk. Na mm nadhani ni mzuri na unatambulika kwa upande wako. Kama hizo thread zako zisingekubalika basi ungekuwa uzuiwa na moderator siku nyingi. USIONDOKE KWANI NA WW UNA UHURU WA KUCHANGIA MAWAZO YAKO NA KUELIMISHA KUTUMIA UZOEFU WAKO.