Amavubi
JF-Expert Member
- Dec 9, 2010
- 30,140
- 13,215
Wanajamvi,
Japo huenda ninahitaji kupata fasiri yakinifu ya neno nje ya ndoa na japo waswahili wanasema kitanda hakizai haramu, ningependa kushirikisha hii kadhia ya watoto wanaoitwa wanaharamu!! wenzangu hii imekaaje??
kuna perspective nyingi kuhusiana na majaliwa/mustakabali wa watoto hawa, kwa mujibu wa sheria za Tanzania, Mtoto wa aina hii anaweza kurithi pale tu aidha atakapokuwa amehalalishwa katika familia husika au mzazi kuacha wosia, kwa kimila inategema na uhalalishaji wa huyo mtoto kwa kufuata mila na desturi husika na kuna baadhi ya dini ambapo hawana haki kabisa ya kurithi (HARAMU)
lakini tunapoona ongezeko kubwa la watoto katika mitaa (si wa mitaani) n.k naomba utoe maoni yako kuhusu mada hii, haijalishi kama wewe ni mmojawapo au la!! Mimi ni mmojawapo amabye anakerekea sana na unyanyaswaji wa kundi hili.
Nawasilisha
Japo huenda ninahitaji kupata fasiri yakinifu ya neno nje ya ndoa na japo waswahili wanasema kitanda hakizai haramu, ningependa kushirikisha hii kadhia ya watoto wanaoitwa wanaharamu!! wenzangu hii imekaaje??
kuna perspective nyingi kuhusiana na majaliwa/mustakabali wa watoto hawa, kwa mujibu wa sheria za Tanzania, Mtoto wa aina hii anaweza kurithi pale tu aidha atakapokuwa amehalalishwa katika familia husika au mzazi kuacha wosia, kwa kimila inategema na uhalalishaji wa huyo mtoto kwa kufuata mila na desturi husika na kuna baadhi ya dini ambapo hawana haki kabisa ya kurithi (HARAMU)
lakini tunapoona ongezeko kubwa la watoto katika mitaa (si wa mitaani) n.k naomba utoe maoni yako kuhusu mada hii, haijalishi kama wewe ni mmojawapo au la!! Mimi ni mmojawapo amabye anakerekea sana na unyanyaswaji wa kundi hili.
Nawasilisha