Prodigal Son
JF-Expert Member
- Dec 9, 2009
- 1,067
- 696
Wadau,
Hiki kitu nimekuwa nacho moyoni nadhani huu ni mwaka watatu sasa,
Kwa tuliowengi tunajua Malengo ya kuanzishwa kwa SOKOINE UNIVERSTY - MOROGORO ni nchi iwe na wataalamu wakutosha wa kilimo, ni wazo jema kabisa, ila kilichonishangaza ni hao wasomi wa chuo hicho kuanzisha televison( SUA TV) nadhani ni Tv ya kwanza kumilikiwa na chuo kikuu hapa Tanzania, moyoni najiuliza ni kwanini wasingeanzisha kiwanda cha maziwa na nyama?
Naamini pesa mlizotumia kuanzishia hiyo TV zingetosha sana tu kwa hilo lengo, mtajitetea na kusema ni pesa za wafadhili na jiuliza mlishindwaje kuwa na hilo wazo kama mlitaka kuonekana SEREKALI si ina TV yake ambayo mgeingia nao mkataba wawe wanaonyesha mambo mliyokuwa mnataka jamii iyaone?
Hamkuona kiwanda cha maziwa hata baadae cha nyama kingekuwa na manufaa zaidi kiliko hiyo TV naamini nyie ndo mlikuwa watu wa kwanza kuwa na mashamba ya mfano na hicho kiwanda ambacho naamini hakingewagharimu pesa nyingi kihivyo kuliko hiyo TV. Mbona wakenya wameweza? Chuo kikuu cha Egerton ni chuo cha kilimo kama nyie wameweza kuanzisha shamba la ngome na wana kiwanda cha maziwa ambacho kinatumika kama sehemu ya wanafunzi kujifunzia na maziwa yao wanayauza miji mbalimbali kya kenya kwa kupitia mawakala.
Wananzuoni wa SUA badilikeni, hata hiyo TV yenu haionekani maeneo yote ya morogoro mngekuwa mnatuzalishia maziwa naamini yangesambaa karibu TZ yote na kutoa fursa kwa wanafunzi kujifunza.
Wadau nawakilisha?
Hiki kitu nimekuwa nacho moyoni nadhani huu ni mwaka watatu sasa,
Kwa tuliowengi tunajua Malengo ya kuanzishwa kwa SOKOINE UNIVERSTY - MOROGORO ni nchi iwe na wataalamu wakutosha wa kilimo, ni wazo jema kabisa, ila kilichonishangaza ni hao wasomi wa chuo hicho kuanzisha televison( SUA TV) nadhani ni Tv ya kwanza kumilikiwa na chuo kikuu hapa Tanzania, moyoni najiuliza ni kwanini wasingeanzisha kiwanda cha maziwa na nyama?
Naamini pesa mlizotumia kuanzishia hiyo TV zingetosha sana tu kwa hilo lengo, mtajitetea na kusema ni pesa za wafadhili na jiuliza mlishindwaje kuwa na hilo wazo kama mlitaka kuonekana SEREKALI si ina TV yake ambayo mgeingia nao mkataba wawe wanaonyesha mambo mliyokuwa mnataka jamii iyaone?
Hamkuona kiwanda cha maziwa hata baadae cha nyama kingekuwa na manufaa zaidi kiliko hiyo TV naamini nyie ndo mlikuwa watu wa kwanza kuwa na mashamba ya mfano na hicho kiwanda ambacho naamini hakingewagharimu pesa nyingi kihivyo kuliko hiyo TV. Mbona wakenya wameweza? Chuo kikuu cha Egerton ni chuo cha kilimo kama nyie wameweza kuanzisha shamba la ngome na wana kiwanda cha maziwa ambacho kinatumika kama sehemu ya wanafunzi kujifunzia na maziwa yao wanayauza miji mbalimbali kya kenya kwa kupitia mawakala.
Wananzuoni wa SUA badilikeni, hata hiyo TV yenu haionekani maeneo yote ya morogoro mngekuwa mnatuzalishia maziwa naamini yangesambaa karibu TZ yote na kutoa fursa kwa wanafunzi kujifunza.
Wadau nawakilisha?