Ni halali CCM kufanyia vikao Ikulu?

Halafu watakanusha wakati nimewabamba

8D6U2336%5B1%5D.JPG
 
Rais kikwete si Rais wa kwanza kufanya vikao vya chama Ikulu hata waliomtangulia walifanya hivyo lakini pia Katiba yetu inaruhusu kufanya vikao Ikulu kwa maana ya kisheria kwamba katiba iko kimya kwa jambo hilo au haijasema lolote....si kosa.

Hata hivyo, Rais kufanya kikao Ikulu na chama kinachotawala sio jambo geni katika siasa za dunia, hata pale chama kingine kikishika dola ni ruksa kufanya vikao vyake Ikulu na CCM haitakuwa na ruksa hiyo kama hakitakuwa chama tawala. Ni vigumu sana wakati mwingine kutenganisha kofia ya urais na shughuli za chama hii ni kwa sababu serikali iliyoko madarakani inatekeleza ilani ya uchaguzi ya chama kinachotawala. Tukumbuke kuwa moja ya agenda za mikutano ya chama ni pamoja na kujadili utekelezaji wa shughuli za serikali kama ilivyoagizwa na chama.

Hata hivyo, bado suala hili linazungumzika endapo sheria itaamua vinginevyo. Maoni ya watanzania kuhusu suala hili ni muhimu lakini bila sheria si vema kulaumu.
 
Ikulu inaweza kuonekana kama ni mahala pa serikali tu lakini kiongozi (Rais) anaekaa humo anatokana na chama cha siasa. Mathalan, kama Rais akiitisha mkutano na vyama vya upinzani katika kumbi za Ikulu hatuwezi kusema kwa nini Rais anafanya mikutano na vyama vya siasa Ikulu.
 
JK amejiruhusu kuwa rais rojorojo, ambae amezungukwa na watu dhaifu ambao hawamsaidii, hata kuliona hilo na lenyewe ni jambo lakuhitaji ushauri wa Bana.
kweli tutaona mengi mpaka huyu Mkwere atakapoondoka Ikulu.

ni kweli....

wakati mwingine huwa najiuliza hivi huyu mkwere ni chaguo la mungu yupi kutuletea mtu mzembe namna hii????????????
 
Rais kikwete si Rais wa kwanza kufanya vikao vya chama Ikulu hata waliomtangulia walifanya hivyo lakini pia Katiba yetu inaruhusu kufanya vikao Ikulu kwa maana ya kisheria kwamba katiba iko kimya kwa jambo hilo au haijasema lolote....si kosa. Hata hivyo, Rais kufanya kikao Ikulu na chama kinachotawala sio jambo geni katika siasa za dunia, hata pale chama kingine kikishika dola ni ruksa kufanya vikao vyake Ikulu na CCM haitakuwa na ruksa hiyo kama hakitakuwa chama tawala. Ni vigumu sana wakati mwingine kutenganisha kofia ya urais na shughuli za chama hii ni kwa sababu serikali iliyoko madarakani inatekeleza ilani ya uchaguzi ya chama kinachotawala. Tukumbuke kuwa moja ya agenda za mikutano ya chama ni pamoja na kujadili utekelezaji wa shughuli za serikali kama ilivyoagizwa na chama.

Hata hivyo, bado suala hili linazungumzika endapo sheria itaamua vinginevyo. Maoni ya watanzania kuhusu suala hili ni muhimu lakini bila sheria si vema kulaumu.

Labda kwa mtazamo wako ni kama vile tunazungumzia hivyo viti na meza walizotumia kufanyia kikao chao. Hebu tufikiri mbali kidogo. Rais ni mwenyekiti wa chama kinachotawala lakini na wajumbe wote wa kamati Kuu ya chama chake nao pia ni marais wa nchi yetu? Bill za umeme na maji watakayotumia CCM itachangia kiasi gani au ndiyo itatoka kwenye fuko kuu la hazina?

Gharama za kuitunza Ikulu zinalipwa na watanzania wote si sahihi kwa watu wa chama kimoja kuitumia kwa kisingizio cha kuwa chama tawala.
 
Kwani ni mwanzo?
Wakati wamezuiliwa kutumia magari ya serikali kwa shughuli za chama kwa ujinga wao wanabandua namba za serikali kwenye magari ya uma na kuweka namba bandia za kiraia ikiwemo za pikipiki.

Shida ya viongozi wetu wamepungukiwa sana utii wa viapo vyao kiasi kwamba sitaki kuwaamini tena kwa wasemayo na hata ahadi zao zinanitia kinyaa. Nchi isiyofuata sheria inakuwa ni nchi isiyo tawalika na mwisho inaweza kutuletea matatizo sana.
We need new government. Nimechoka na sisi m.
TUMCHAGUE DR SLAA NA KUMPA UONGOZI WA NCHI YETU. KWA NINI TUENDELEE KUWAACHIA NCHI YETU WAHUNI HAWA NA FAMILIA ZAO?
 
nahisi hawa jamaa wanajua kabisa wanapindisha mambo ila wanafanya makusudi coz wanajua hakuna wa kuwafanya kitu,wanajifanya wapo juu ya sheria na taratibu,nafikiri siku upinzani unachukua nchi wengi wataikimbia hii nchi kwa hofu ya makosa yao ya makusudi kwa umma wa tz!
 
Nakaa jirani na waziri mmoja gari lake amebandua nambaa yuko bize sasa hivi kumkampenia mgombea ubunge wa Ubungo wa CCM
 
Wanafanyia Ikulu ili kuzuia uwezekano wa waandishi wa habari kunasa wanachopanga. Maji yako shingoni. Mwaka huu watabarehe mara ya pili
 
Wana Jf,
Ninaomba mnisaidie ufafanuzi. Nimesoma kwenye magazeti leo mwananchi.co.tz nikaona kuwa CCM inafanya mchujo wa wagombea umeya katika kikao kitakachofanyika DSM leo.

Nanukuu..... "Katibu Mkuu wa CCM Yusuph Makamba, jana aliliambia gazeti hili kwamba CC itakutana Ikulu chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, kwa ajili ya kupitisha majina yasiyopungua matatu kupeleka kikao cha chama cha madiwani"

Kwa vile mimi najua iKULU ni mali ya serekali(wananchi walipakodi), je ni sahihi kikao cha chama kufanyika humo na kutumia rasilimali zilizopo kwa ajili ya matakwa ya chama chao?"

nawakilisha!
 
Ni Tanzania pekee duniani fedha za walipa kodi hazilengi kumsaidia
mlipa kodi bali wachache. Vivyo hivyo walipa kodi wa Tanzania ndio
walipa kodi pekee duniani hawahoji hela zao zimetumika vipi kwa maslahi yao.
 
Kufanyia kikao cha ccm Ikulu ni kukiuka maadili ya uendeshaji wa serikali. Ikulu ni ofisi za Rais wa Jamhuri ya Tanzania na si ofisi ya mwenyekiti wa CCM; hivyo basi Kikwete anainajisi Ikulu kwa kuifanya kama ofisi ya chama.
 
TZ ni nchi ya ajabu hivyo hayo unayoyaona wala hayana tatizo hadi hapo nchi hii itakapowekwa sawa. Hamkumbuki kuwa wakati wa kampeni mgombea wa CCM alitumia rasmali za ikulu katika kampeni? Tena hamkumbuki Bashe alienguliwa kwenye nafasi ya kugombea ubunge ndani ya vikao vya CCM kwa sababu si raia wa Tz wakati uhamiaji wakisema ni raia? Hapo majukumu ya Serikali yalifanywa na CCM.

Watanzania tupo hovyo kuliko wananchi wa nchi zingene katika suala la mgawanyo wa madaraka, majukumu nk. Tuondelee kudai haki ya kuwa na katiba mpya itakayotusaidia kupata dira mpya kuliko hii ya sasa ambapo inatufanya tuchanganyikiwa.
 
Usishangae kama JK alitumia helikopta za mabepari wa Barrick,Salma akatumia Ndege ya Serikali,Ridhiwani akatumia magari ya serikali,na CCM wakatumia magari,ofisi na rasilimali watu wa serikali kwenye kampeni zao wakiwa IKULU kitu gani kitawazuia wasifanye mkutano huko mmh unajiuliza jibu
 
Back
Top Bottom