Nguvu umma yamtesa Pinda Mwanza, azomewa, awa mbogo!

Dawa ni kuwazomea popote wanapopita mpaka waache kutumia polisi kuua watanzania wasio na hatia.Hongereni wana Mwanza.
 
Naungana na watanzania wenzangu kulaan kitendo cha utovu wa nidhamu kilichoonyeshwa na Mh.Wenje kipindi cha ziara ya waziri Mkuu Mh.Pinda

Mh.Wenje amekua si mngwana na ameonesha kutokomaa kisiasa,imetusikitisha sana wana Mwanza hasa sisi watu wa Nyamagana na tunajuta sana kumpeleka Bungeni bwana Wenje.

Mtu anapokuwa waziri mkuu huyu ni mtendaji mkuu wa serikali na ni mtumishi wa watanzania wote,bila kujali itikadi ya Chama kitendo cha Mh.Wenje kuwapatia posho wamachinga na kuanza kuimba peoples' si uungwana kabisa.

Tunaahidi kwamba uchaguzi ujao Chadema hawatakuwa na nafasi tena Jimbo la Nyamagana.

teh teh teh! Huwa hamkosi visingizio,yaani watu wote waliokuwepo ni machinga? Mi mwenyewe nilikuwepo nikazomea lakini sio machinga.ukweli ni kwamba ccm tumeichoka mpaka hamna maelezo nayoweza kukupa kwa jinsi tulivyowachoka NYINYIEM.
 
Hakika pinda ni mvumilivu sana angekuwa mtu kam Nchimbi ange agiza polisi wazitumie hizo silaha za kivita papo hapo.

Kweli pinda amekutana na visiki vya mpingo!


PINDA ni vyema akazomewa, kuna mengi kanda ya ziwa yamekuwa kero.Kwanza bei ya pamba kuteremka huku PINDA akichukulia ni kuteremka kwa bei ya soko duniani, j serikali haina mkono wake kuwalinda wakulima hawa?kwann kwenye mdororo wa uchumi duniani serikali ilitia mkono wake na pesa hiyo haijulikani ilifanya kazi gani hasa kwenye viwanda vya pamba.Pia bei ya soko la samaki kudorola na kuteremka, PINDA akamtuma waziri wake , akarudi bungeni na ripoti ya blabla.na hivyo kuhitimisha mjadala kwa kuuzima kwa kauli dhaifu.Kwahiyo kutokujali kwa pinda kuhusu kero hizo nilitegemea sana azomewe karibu kanda yote ya ziwa.
 
Chezea ngosha weye!!!!!! wameamka kuona wamebakiwa na mashimo hela za dhahabu zoote canada na katika akaounti za uswisi.

Wakusini wamegutuka -- hawataki yawapate yaliyowapata akina Ngosha.
 
Back
Top Bottom