hakika umenena.Nadhani kuwe na TUITION kwa new babies.....! MANAKE NI AIBU....!
Naomba niwatoe kwenye mada kidogo.... juzijuzi kuna wajeshi waliua!!! tuliacha mada na kushambulia jeshi, leo suka kaua, naona tunapeana nasaha za maana zaidi
Ushauri wangu ni kwamba tuwaangalie watu kama watu na si kama wawakilishi wa watu wengine
HASIRA HASARA REGARDLESS WEWE NI NANI KATIKA JAMII... POLE WAFIWA NA TUJIFUNZE KUTOKANA NA MAKOSA, SI KILA ATEMBEAYE NI MZIMA
Wacha afe manaake wao wakiwa wanaendesha daladala huwa wanatutesa sana madereva wa magari mengine madogo, wacha rife
Naona huko home watu kupigana kama kuku wanaona ndiyo dili sana au ndiyo kuonyesha ubabe, mara askari wamepiga wameua, ooh mwalimu kapiga mtoto shuleni kaua, mara mama wa kambo kamchoma mtoto makalioni na sehe mu za siri, mara dereva wa daladala.
Jamani unaruhusiwa kupigana pale tu unapokuwa unatetea uhai wako na siyo hasira zako. Hata wezi wakikuvamia kama wanachotaka ni mali wachukue waende zao lakini kama wanataka uhai huo usiwape kirahisi lazima zipigwe.
Sasa barabarani ukiwa na hasira za hivyo utaendeshea gari kwenye bedroom yako? Maana hayo matukio ni mengi kama mchanga wa bahari barabarani. Inabidi ukubali kuyazaoea na kuvumiliana nayo.
Wewe Godliving Severini uliyeua mwenzako hivi ungeshuka unipige ngumi mimi ingekuaje? Hizo hasira zenu za kijinga kuna siku mtakuja kuzifanya kwa Ninja halafu muone matokeo yake.
'' A true man is identified not by showing his temper but by his control of it". Mtu yeyote asiyeweza kudhibiti hasira zake hajakamilika kiumeni.
Duh!! Bonge la point mwana, nimepunguza hasira zangu ghafla baada ya kusoma hii post yakoHasira ni hasara,na biblia pia ikasema Hasira ya mwanadamu haitendi haki ya Mungu,juzi alikuja rafiki yangu amefura hasira eti katoka huko alikotoka anaenda kugombana na mtu,ilibidi nimwulize kwanza sababu aliponieleza sababu kwanza nilicheka,nilipocheka hasira yake ndo ikapanda zaidi,ikabidi nimweleze sbbu za mimi kucheka,alipoelewa nikaanza kumpa darasa nikamwambia mtu akikukorofisha nenda kaongee nae kirafiki kabisa atakuelewa kuliko kwenda kishari,nashukuru alinielewa na akaufanyia kazi ushauri.
My point is pale tunapohisi hatukutendewa haki ni vizuri kutulia kwanza na kutafakari cha kufanya mambo ya kukurupuka si mazuri,huwa nawambia rafiki zangu siku hizi watu wanatembea wamekufa anasubiri sababu tu,unaweza ukagombana na mtu pressure ikapanda akaanguka utaambiwa umeua,kwa hiyo ni vizuri tujifunze kudhibiti hasira zetu.