Laptop01
JF-Expert Member
- Nov 29, 2009
- 1,365
- 796
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu nyenendo za Ngoyai Lowasa ambae kufuatia sakata la Richmond Development Co.LLC alilazimika kupima na kubwaga manyanga UWAZIRI MKUU. Nimebaini kuwa ukiacha kilichoonekana kuwa ni kupenda kujilimbikizia kila kiitwacho mali, mtu huyu ni mtaalam wa kusoma nyakati zinazoweza azaliwe upya katika siasa za Tanzania.
Katika suala la mabomu alitoa kauli yake nzito
Katika suala la uchumi nimemsikia leo akitoa kauli kwamba paundwe tume ya kuchunguza namna bora ya kulishughulikia suala hili, target yake katika hili imekuwa ni kulilenga kundi la wafanya kazi.Kauli zake ni nzito na zenye maana kuliko zile za mkuu wa nchi katika kutatua matatizo ya kitaifa
Hitimisho langu likawa ni kwamba huyu mtu ni fundi wa kutumia matukio yanayojiri kitaifa ili kujiinua kisiasa. Lakini pia Ngoyai ni mchapa kazi na hutembea katika kauli zake. Nakumbuka suala la maji ya ziwa victoria na vikwazo vya wasudani na wamisri, suala la shule za sekondari za kata, suala la bandari kavu (despite the implementation failure)
Ushauri wangu kwake: kwakuwa giza linaendelea kuitafuna nchi na uchumi wake, Ngoyai toa kauli yako pia katika hili. Toa kauli yako Ngoyai katika malipo ya serikali ya taifa lako kwa DOWANS.
Katika suala la mabomu alitoa kauli yake nzito
Katika suala la uchumi nimemsikia leo akitoa kauli kwamba paundwe tume ya kuchunguza namna bora ya kulishughulikia suala hili, target yake katika hili imekuwa ni kulilenga kundi la wafanya kazi.Kauli zake ni nzito na zenye maana kuliko zile za mkuu wa nchi katika kutatua matatizo ya kitaifa
Hitimisho langu likawa ni kwamba huyu mtu ni fundi wa kutumia matukio yanayojiri kitaifa ili kujiinua kisiasa. Lakini pia Ngoyai ni mchapa kazi na hutembea katika kauli zake. Nakumbuka suala la maji ya ziwa victoria na vikwazo vya wasudani na wamisri, suala la shule za sekondari za kata, suala la bandari kavu (despite the implementation failure)
Ushauri wangu kwake: kwakuwa giza linaendelea kuitafuna nchi na uchumi wake, Ngoyai toa kauli yako pia katika hili. Toa kauli yako Ngoyai katika malipo ya serikali ya taifa lako kwa DOWANS.